Nurdin Muhochi
Member
- Oct 17, 2018
- 17
- 11
Aliekuwa Rais wa Zanzibar,kwa yeyote mwenye kujua maisha yake ya kisiasa (the rise and fall)ya huyu mzee alietangulia mbele ya haki atujuze .
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Alizaliwa Juni 14, 1940 huko Mkamasini Ngambo, Zanzibar. Alisomea shule ya Ben Bella hadi mwaka 1942 . Mwaka 1943 hadi 1945 alikuwa Chuo Kikuu Makerere akisomea ualimu na alifuzu na kupewa stashahada ya Ualimu. Baada ya hapo alifundisha somo la Baiolojia katika shule ya Mnazi mmoja na Lumumba tangu 1946 hadi 1960.
Alikuwa mwanachama wa ASP tangu 1957, mwaka 1960 hadi 1964 alikuwa mjumbe wa Baraza la kutunga Sheria akiwa Kiongozi wa Upinzani. Baada ya Mapinduzi aliongoza kwa Muda mfupi Wizara ya Mambo ya Ndani ya Zanzibar. Baada ya Muungano aliteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais. Baada ya Kuuwawa kwa Karume alikuwa Rais wa Zanzibar na Makamu wa Rais wa JMTz.
Wakati akiwa Rais wa Zanzibar alisaidia kuleta mabadiliko makubwa kwa kufanya mabadiliko katika sheria ili kuondoa nguvu ya Baraza la Mpinduzi ambalo liliendesha nchi kibabe. Alitoa nafasi kwa Wanafunzi wa Zanzibar kujiunga na UDSM na baada ya kuhitimu baadhi walipewa nafasi serikalini, watu kama Maalim Seif Sharif Hamad na Juma Duni Haji. Pia alifanikiwa kuanzisha Baraza la Wawakilishi na Kurekebisha Mfumo wa Mahakama.
Mwaka 1977 alifanikisha uanzishaji wa Chama Cha Mapinduzi na akawa Makamu wa Mwenyekiti. Mwaka 1984 aliandika barua kwa Rais Nyerere, katika barua ile alitanabahisha kuwa Kulikuwa na Ukiukwaji wa Mkataba wa Muungano pamoja na Sheria yake ya mwaka1964 na Sheria ya Baraza la Kutunga Katiba ya mwaka 1965. Barua hiyo iliibukia mikononi mwa Nyerere ambapo aliitisha kikao cha NEC Januari 24, 1984 ambako alituhumiwa kwa kuchafua hali ya siasa katika Zanzibar, na akajiuzulu vyeo vyake vyote. Baada ya hapo alipelekwa uhamishoni Mji Mwema Kigamboni Dar es Salaam
Usichanganye Ali Mwinyi na Abdu Jumbe Mwinyi mkuu,Napinga, Jumbe kazaliwa Bara na si Zanzibar. CV zakutengenezewa mazingira izo.
Sijachanganya kabisa. Nakifahamu ninachokizungumza.Usichanganye Ali Mwinyi na Abdu Jumbe Mwinyi mkuu,
Haya leta historia yakeSijachanganya kabisa. Nakifahamu ninachokizungumza.
Ni mzaliwa wa Mjimwema. Unguja kahamia tu kama wanampinduzi wenziwe.
Kwenye mwaka wa kuzaliwa kuna kosa kidogo hapoAlizaliwa Juni 14, 1940 huko Mkamasini Ngambo, Zanzibar. Alisomea shule ya Ben Bella hadi mwaka 1942 . Mwaka 1943 hadi 1945 alikuwa Chuo Kikuu Makerere akisomea ualimu na alifuzu na kupewa stashahada ya Ualimu. Baada ya hapo alifundisha somo la Baiolojia katika shule ya Mnazi mmoja na Lumumba tangu 1946 hadi 1960.
Alikuwa mwanachama wa ASP tangu 1957, mwaka 1960 hadi 1964 alikuwa mjumbe wa Baraza la kutunga Sheria akiwa Kiongozi wa Upinzani. Baada ya Mapinduzi aliongoza kwa Muda mfupi Wizara ya Mambo ya Ndani ya Zanzibar. Baada ya Muungano aliteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais. Baada ya Kuuwawa kwa Karume alikuwa Rais wa Zanzibar na Makamu wa Rais wa JMTz.
Wakati akiwa Rais wa Zanzibar alisaidia kuleta mabadiliko makubwa kwa kufanya mabadiliko katika sheria ili kuondoa nguvu ya Baraza la Mpinduzi ambalo liliendesha nchi kibabe. Alitoa nafasi kwa Wanafunzi wa Zanzibar kujiunga na UDSM na baada ya kuhitimu baadhi walipewa nafasi serikalini, watu kama Maalim Seif Sharif Hamad na Juma Duni Haji. Pia alifanikiwa kuanzisha Baraza la Wawakilishi na Kurekebisha Mfumo wa Mahakama.
Mwaka 1977 alifanikisha uanzishaji wa Chama Cha Mapinduzi na akawa Makamu wa Mwenyekiti. Mwaka 1984 aliandika barua kwa Rais Nyerere, katika barua ile alitanabahisha kuwa Kulikuwa na Ukiukwaji wa Mkataba wa Muungano pamoja na Sheria yake ya mwaka1964 na Sheria ya Baraza la Kutunga Katiba ya mwaka 1965. Barua hiyo iliibukia mikononi mwa Nyerere ambapo aliitisha kikao cha NEC Januari 24, 1984 ambako alituhumiwa kwa kuchafua hali ya siasa katika Zanzibar, na akajiuzulu vyeo vyake vyote. Baada ya hapo alipelekwa uhamishoni Mji Mwema Kigamboni Dar es Salaam
Ni kweli ni mwaka 1920, nimerekebisha, AhsanteKwenye mwaka wa kuzaliwa kuna kosa kidogo hapo
Haya leta historia yake
Ingefaa utie nyama kidogo, mathalan alihamia lini Unguja?Historia ndo unapa weye. Mie nimekosoa tu nilipoona pana tatizo kama alivyokosoa mwenzangu.
Haya leta historia yake
Wakati wa mapinduzi hata Karume na Babu walijifichaWakati mapinduzi yanafanyika Unguja, Yeye Alikuwa chooni kajificha. Alikwenda kuchukuliwa na Aboud Mmasai kwake ndani amejichimbia akapelekwa raha leo. Maana baada tu ya kupata fununu za mapinduzi ndipo alipojikomelea milango ndani.
Alioa mke kwa nguvu bila ya ridhaa yake wala waazee wake baada ya mapinduzi kama wanamapinduzi wenziwe wengi walivyofanya.
Wakati wa mapinduzi hata Karume na Babu walijificha