Qualifier
JF-Expert Member
- Dec 14, 2012
- 1,252
- 407
Habari za mchana wa jf. Ni kisa kilicho tokea hivi karibuni pale Nyololo kule Mufindi. Nilikuwa nasafiri kwa basi kutoka Mbeya kuelekea Dar, tulipofika nyololo basi lilisimama, kama kawaida ya wachuuzi wa biashara ndogondogo walikimbilia basi na kujaa madirishani huku wengine wakigonga madirisha kuwaashiria abiria wafungue madirisha yaliyo fungwa. Dirisha lililo kuwa mbele yangu alikaa abiria ambaye inaonekana alikuwa anahoma, mgonjwa huyo alipojisikia kutapika akafungua dirisha haraka wale wachuuzi wakakimbilia na kuelekeza biashara zao kwa kugombania mmoja wao aliyebeba sinia la samaki waliokaangwa akawazidi nguvu wenzie na kulielekeza sinia la samaki karibu sana na kichwa cha mgonjwa ambaye sasa alikuwa tayari anatapika na matapishi kujaa kwenye sinia lenye samaki. Ni kisa cha kusikitisha sana kwa sababu mwenzetu alikuwa anahoma na bado yule mchuuzi akaharibiwa biashara yake ambayo ninaamini mqlengo yake kwa siku hiyo yaliharibika. Pamoja na abiria kucheka lakini hizi ni changamoto zinazo wakumba wachuuzi kwenye vituo vya mabasi .