Abiria Mabasi ya Mikoani

Abiria Mabasi ya Mikoani

zeus

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2009
Posts
213
Reaction score
55
Kuna jambo moja linanishangaza na kuudhi. katika barabara nyingi ziendazo mikoani- up country- kuna vituo vya mizani kupima uzito wa magari -mabasi ya abiria na magari ya mizigo. sasa utakuwa wenye mabasi ya abiria yaendayo mikoani wanajaza abiria kupita kiasi halafu wakifika karibu na mizani wanashushwa watu waliokaa viti vya nyuma ili kuhadaa watu wa Measurement. Abiria hao wataambiwa watangulie mbele kwa miguu au watatafutiwa kausafiri fulani wakutwe kule mbele. gari inapita kwenye mizani na wataenda kupakiwa huko mbele. Huu ni upumbavu kiasi gani? hivi hii si kuhatarisha maisha yako mwenyewe na kwa faida ya nani?. kwa nini wasikatae halafu mwenye gari awe penalised ili asirudie?. Ajali ikitokea kwa sababu ya overloading nani alaumiwe? sijui abiria hawa wakoje.
 
hiyo ndio Tanzania, unakuta mtu anasafiri kwa nauli ya kuungaunga, anapewa masharti ya kukaa kiti cha nyumba na kusumbuliwa kila kwenye Mizani, mimi sidhani kama umekata tiketi yako safi na upo humo na heshima zako kuna mtu atayeweza kukuambia utembee kwa miguu watakupakia mbele
 
habari ndo hiyo tunaangamia kwa kutumia maarifa unlike scripture stipulated
 
Huu ni ujinga wetu wenyewe wasafiri ambao hatujui haki zetu. Kwanini utoe nauli halafu uadhibiwe?

Madereva wanaendesha kwa spidi kali barabarani abiria wamenyamaza kimya ndani, ikitokea ajai tu basi haoooo kila mtu ooooooh dereva alikuwa anaendesha mwendo wa kasi. Kwa nini wasiseme wakati dereva anaendesha?
 
Huu ni ujinga wetu wenyewe wasafiri ambao hatujui haki zetu. Kwanini utoe nauli halafu uadhibiwe?

Madereva wanaendesha kwa spidi kali barabarani abiria wamenyamaza kimya ndani, ikitokea ajai tu basi haoooo kila mtu ooooooh dereva alikuwa anaendesha mwendo wa kasi. Kwa nini wasiseme wakati dereva anaendesha?

Yani nimepanda dar express leo ilivyokuwa inakimbia, nilitamani nishuke na kutembea japo sijui ningefika nini niendapo!..
Kuhusu spidi unakuta abiria tunataka kuwahi kufika lakini unaweza kuta hatufiki tuendapo zaidi ya ajali halafu hamna ushirikiano wa abiria kukemea spidi kali!
 
CHADEMA,CUF,CCM,CCK,TLP,WAKRISTO,WAISLAMU,TAKUKURU,POLISI,WANAFUNZI,MANESI,RUBANI,WAANDISHI,WANA-JF,WANA-SIMBA,WANA-YANGA...........wote hawa hupanda mabasi hayohayo na wao ndiyo hushushwa na kupandishwa vipanya kuhadaa mizani........!MABADILIKO YAANZE KWANGU ,KWAKO,KWAKE,KWAO,KWETU NA KISHA TUAMBUKIZE JAMII NZIMA
 
Back
Top Bottom