A serious question: Rais huwapata wapi anaowateua?

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Teua/tengua aifanyayo Rais na Mwenyekiti wangu Dr. John Pombe Magufuli haina taswira nzuri. Huonesha na kutonesha 'udhaifu' katika teuzi. Kitendo cha Mteule 'kuchongewa' mbele za Mteuwa wake na Mteuwa kumtumbua siku inayofuata si chema. Nasisitiza, hiki si kitendo chema. Kitendo cha Mteule kukosea mbele ya Mteuwa wake na kutumbuliwa hima si kizuri.

Wakati nikiwa kwenye mifumo ya Serikali na chama, nilifahamu kuwa Wateule hupatikana kwa utaratibu maalum ingawa huteuliwa na Mteuwa. Huchujwa na kuchujika; kuchunguzwa wakachunguzika na kufuatiliwa na wakafutilika. Hujulikana uimara na udhaifu wao. Huteuliwa kwenye nafasi zinazoendana na uimara na udhaifu wao. Na husaidiwa kiserikali au kichama.

Kwasasa nimebaki chamani na sipo tena Serikalini kulipo na uteuzi. Nimebaki kama kada mwandamizi wa CCM lakini nisiye na maamuzi yoyote. Nabaki kustaajabishwa na aina ya viongozi wanaoteuliwa na kutumbuliwa. Wapo wanaolalamikiwa lakini wanachuniwa. Wapo wanaonyamaziwa lakini wanatangaziwa. Mambo yamebadilika. Mambo yamekuwa mambo!

Ndiyo maana najiuliza, Rais huwapata wapi anaowateuwa? Walikuwa timu moja wakati wa harakati zake za 2015 hata kama ni sirini? (maana nawajua waliokuwa naye kuanzia Ukumbini na kwenye kampeni zake wakimuunga mkono waziwazi). wanaletwa na utaratibu unaowachuja na kuwawasilisha kwake? Anawapataje hasa kwasasa? Naichukia tabia ya kumchongea kiongozi waziwazi mbele ya Mteuwa wake.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
 
Mzee tupa tupa, tumia uzee wako vizuri baba Kwasababu huna mamlaka ya kumhoji Rais, ni Kama kijana wako ukisikia anakuuliza tarehe uliyolala na mama yake Ndo yy akapatikana, tulia Mzee, JPM is not simple Like how your ego drives you to believe
 
Alituaminisha kachukua muda mrefu kupanga safu yake na kusoma mafile ya kila mmoja halali anakesha na mafaili usiku kucha afu mwisho wa siku 0=bashite kazi kweli kweli
 
Ni wazi anawateua asiowajua vizuri au wanaoletwa na wapambe na wengine sifa kuu ni kuhama kutoka upinzani na kuingia ccm kama akina Waitara
 
Mzee tupa tupa, tumia uzee wako vizuri baba Kwasababu huna mamlaka ya kumhoji Rais, ni Kama kijana wako ukisikia anakuuliza tarehe uliyolala na mama yake Ndo yy akapatikana, tulia Mzee, JPM is not simple Like how your ego drives you to believe

Kabudi na ww unajua kuweka firewall watu wakianza kuchimba ulivyopata cheo!! Kweli ulaji sio mchezo, mnakuwa wakali vibaya sana watu wakisogelea sahani zenu.
 
Propesa Kabudi kasema jana alitolewa jalalani..!! Ila mm nilijua kabla ya kuwa Waziri, Kabudi alikuwa UDSM..!! Kumbe UD ni jalalani? 🤔

Acha tu bata wanazopiga hao jamaa, ngoja sisi tubangaize tu na jua na mvua ipo siku yetu
 
Utaratibu maalum upi ambao wengine hatukuujua kipindi hiko wewe ukiwa serikalini na chamani?
 
Teua/tengua aifanyayo Rais na Mwenyekiti wangu Dr. John Pombe Magufuli haina taswira nzuri. Huonesha na kutonesha 'udhaifu' katika teuzi. Kitendo cha Mteule 'kuchongewa' mbele za Mteuwa wake na Mteuwa kumtumbua siku inayofuata si chema. Nasisitiza, hiki si kitendo chema. Kitendo cha Mteule kukosea mbele ya Mteuwa wake na kutumbuliwa hima si kizuri.

Wakati nikiwa kwenye mifumo ya Serikali na chama, nilifahamu kuwa Wateule hupatikana kwa utaratibu maalum ingawa huteuliwa na Mteuwa. Huchujwa na kuchujika; kuchunguzwa wakachunguzika na kufuatiliwa na wakafutilika. Hujulikana uimara na udhaifu wao. Huteuliwa kwenye nafasi zinazoendana na uimara na udhaifu wao. Na husaidiwa kiserikali au kichama.

Kwasasa nimebaki chamani na sipo tena Serikalini kulipo na uteuzi. Nimebaki kama kada mwandamizi wa CCM lakini nisiye na maamuzi yoyote. Nabaki kustaajabishwa na aina ya viongozi wanaoteuliwa na kutumbuliwa. Wapo wanaolalamikiwa lakini wanachuniwa. Wapo wanaonyamaziwa lakini wanatangaziwa. Mambo yamebadilika. Mambo yamekuwa mambo!

Ndiyo maana najiuliza, Rais huwapata wapi anaowateuwa? Walikuwa timu moja wakati wa harakati zake za 2015 hata kama ni sirini? (maana nawajua waliokuwa naye kuanzia Ukumbini na kwenye kampeni zake wakimuunga mkono waziwazi). wanaletwa na utaratibu unaowachuja na kuwawasilisha kwake? Anawapataje hasa kwasasa? Naichukia tabia ya kumchongea kiongozi waziwazi mbele ya Mteuwa wake.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kilosa, Morogoro)
Sisi wastahafu wa utumishi wa serikali tulishuhudia chanzo cha serikali kuwa tawi la COM katika utawala wa awamu ya pili.
Matokea yake sasa tumefika mbali utawala ni wa genge fulani na masilahi yao huku CCM wakiwa kama punda waliobeneshwa mizigo waufikishe.
Mimi sipati tabu na mteuzi; napata tabu na wateuliwa kukubali kuteuliwa bila kujua sababu za kuteuliwa kwao. Nina maana bila ya wateuliwa kuelewa wanakwenda kufanya nini chini ya nani na kufanikisha nini?
 
Propesa Kabudi kasema jana alitolewa jalalani..!! Ila mm nilijua kabla ya kuwa Waziri, Kabudi alikuwa UDSM..!! Kumbe UD ni jalalani?

Ukitaka kujua kweli ni jalalani angalia Kabudi alipokuwa anafundisha jinsi alivyokuwa amepauka, linganisha na sasa anavyomsifia Magu uone alivyotakata. Wakati ule ulikuwa ukimuita anageuza shingo haraka kama mwanajeshi, sasa hivi anageuza shingo kama ana jipu.
 
Ukimtoa Nyerere, marais wengine wote wameongoza kwa kutegemea magenge yao. Kama wewe si mmoja wa genge la rais anayekuwa madarakani unatumbuliwa haraka sana bila kujali umefanya kosa gani. Mfano halisi wa sasa ni yaliyomkuta Nape, na anavyolindwa Makonda.
Rais Magufuli hana undugu au ushkaji kwenye masuala ya nchi. Hilo tumeliona tangu akiwa Waziri na hadi kuwa Rais. Siri kubwa kwake ni mtu kutimiza majukumu yake...huyo ndiye rafiki na mshkaji wake. Makonda anajitahidi kutimiza wajibu wake.
 
Back
Top Bottom