A Hero who Managed to Manipulate Women!

A Hero who Managed to Manipulate Women!

JF2050

JF-Expert Member
Joined
Sep 25, 2010
Posts
2,085
Reaction score
45
Ilikuwa mwaka jana mwezi wa January nilipotua katika kijiji kimoja kilichopo mkoani Singida, jina la kijiji ni mdida. Nilikuwa katika harakati za kutafuta data kwa ajili ya kukamilisha utafiti fulani. Katika mazungumzo mbalimbali yasiyokuwa rasmi kati ya mimi na mwanakijiji mmoja tulijikuta tukiongelea mambo yanayohusu mahusiano ya kimapenzi baina ya wakazi wa kijiji hicho.

Mwanakijiji huyo aliniambia ni vigumu kukuta katika kijiji hicho wazee hasa wa miaka ya 50 na 60; na baadhi ya vijana wa makamo ambao wameoa mke mmoja tu. Alinionya ya kwamba nisishangae kuona au kusikia kuna wanaume wameoa wake 2-3.

Alienda mbali zaidi aliponiambia ya kwamba kuna mzee mmoja, jina lake ni "Ahmedi Mimbi" maarufu kama Mzee Mrii, kuwa ana wake 12, na mke wake wa mwisho amezaliwa mwaka wa 1978! Nilishtuka lakini alifanya kila jitihada ili kunishusha Munkari.

Nilipata hamu sana ya kujua, kulikoni! "How this guy succeeded to manipulate this bunch of wives".

Nilimwuuliza kama kulikuwa na nguvu au uwezo wowote wa ziada ambao ulimwezesha huyo mzee kumiliki idadi hiyo ya wanawake; jamaa aliendelea kusimulia:

"Mzee Mrii ni tajiri mkubwa wa ng'ombe, ana wake 12, wake 8 wapo katika kijiji hiki cha mdida, na wengine 4 wanaishi katika kijiji fulani kinaitwa Kijota. Kila mke ana watoto kadhaa - wapo wenye watoto hadi kumi na zaidi. Pia Kila mke amejengewa kaya/mji wake. Sifa kubwa ya huyu mzee ni uwezo wake wa kuweza kutoa mahari na kuoa kwa sababu ana ng'ombe wa kutosha, vilevile anajitahidi kuhudumia wake zake kwa mahitaji kadri anavyoweza".

Alidai kuwa, kwa sasa hao ng'ombe wamepungua lakini miaka ya nyuma inakadriwa alikuwa akimiliki ng'ombe elfu kadhaa".

Nilitaka kujua ni kwa namna gani anaweza kuwaridhisha wake hao 12 hasa ikija swala la mapenzi?

Mwanakijiji huyo alidai kuwa kwa kawaida huyo mzee huwa hafanyi kazi nyingine zaidi ya kufanya ziara za kutoka kaya moja hadi nyingine kwa ajili ya kuwahudumia wake zake kimapenzi. Alidai hata hivyo, watoto wake wengi wanafanana naye - ishara nzuri ya matunda ya kazi yake, lakini pia kuna wengine ambao huwezi kuthibitisha moja kwa moja kama ni wa kwake au lah!

Nilimwuuliza je kuhusu swala la kuwasomesha?

Jibu lilikuwa ni kwamba mzee huyo amefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuwasomesha watoto wake hadi kiwango cha shule ya msingi! Ilidaiwa kuwa, watoto kadhaa wa mke wa pili (seniority) katika orodha hiyo wamefanikiwa kuonja elimu ya sekondari na wengine chuo.

Simulizi zaidi zilidai kuwa huyo mzee ana watoto wanaokadriwa kufika 100 (achilia mbali nyumba ndogo). Umri wake kwa sasa ni mkubwa, kwani msimuliaji alinieleza kuwa huyo mzee ana umri mkubwa kuliko wa baba yake ambaye alizaliwa mwaka wa 1945.

Nilitaka kujua kama anawatambua vizuri watoto wake!

Mwanakijiji aliendelea kufunguka na kudai kwamba, mara nyingi huyo mzee huingia mkenge pale mtoto anapomdai hela kwa ajili ya malipo fulani - hasa michango ya shuleni. Kwani kinachotokea ni kwamba, mtoto yeyote hata wa jirani anaweza kumwibukia na kumwambia naomba hela nikanunue daftari au hela ya mchango, nadaiwa shuleni, kwa sababu ya wingi wa watoto imekuwa ni vigumu yeye kuwafahamu wote - kwa hiyo mara nyingi amelazimika kutoa hela kwa mtindo huo.

Imedaiwa kuwa, hivi karibuni ameunda kamati maalumu inayojumuisha watoto wake kadhaa ambao anawaamini - hiyo kamati kazi yake ni kumhakikishia kama kweli mtoto yeyote anayedai malipo yanayohusiana na malezi ni wa kwake kweli! Pia ili kuepuka "fraud" ya aina yoyote na utapeli wa mara kwa mara. Malipo mengine kama michango ya shule, hulazimika kwenda kuuza ng'ombe na hatimaye kuondoka na fuko la hela kuelekea shuleni kwa ajili ya kulipa michango mbalimbali wanayodaiwa watoto wake. Pia kila mwanamke amegawiwa ng'ombe kadhaa kwa ajili ya kuendesha maisha yake na ya watoto wake.

Imedaiwa kwamba, hivi karibuni amefanya majaribio kadhaa ya kuoa wake wengine, lakini watoto wake hasa wakubwa wamekuwa wakiwawekea ngumu wanawake wanaotaka kuolewa na mzee huyo. Mara nyingi watoto wake huwachimba mkwara au kutishia kuwadhuru wanawake iwapo wataolewa na baba yao - cha ajabu imedaiwa kuwa watoto hawana ubavu wa kukabiliana moja kwa moja na baba yao.

Msimuliaji aliongeza kuwa, watoto wake karibu wote waliofikia umri wa kuoa wana wake zaidi ya mmoja na huenda wana mpango wa kuongeza wengine hapo baadaye. Alibaini kwamba ni mtoto mmoja tu wa rika la juu ambaye ameamua kuwa mkristo na ameoa mke mmoja tu.

Msimuliaji aliniambia ya kwamba hajawahi kuona, kuhisi au kusikia hali yoyote inayoashiria usaliti wa wake hao dhidi ya huyo mzee.

Taarifa zaidi zilieleza kwamba, wanawake/kaya karibu zote zinahasimiana, lakini cha ajabu yeye ameweza kuwadhibiti wake wote 12 na wote wanakiri na kumtambua asilimia 100 kama mume wao!

Overview/comments/questions/

1. Je huyu mzee anatoa wapi nguvu ya kuwaridhisha wake zake wote 12 na mahawara wengine, wakati tunaona na kusikia kila leo hasa hapa mujini Darisalama watu wenye mwanamke mmoja tu wanakimbiwa na wake zao kwa tatizo la kushindwa kuwaridhisha?

2. Ni kwa nini wanawake waendelee kumkubali na kuolewa na mzee Mrii wakati tayari wakijua kuna msururu wa wanawake wengine ambao tayari alikuwa amewaoa?

3. Kwa nini hapakuwa na ugomvi dhahiri kati ya Mzee Mrii na wake zake badala yake wake zake tu ndio wanaogombana? Ndio tuseme alitumia mbinu ya "divide and rule"?

4. Je, hii dhana na uhalisia wa nyumba ndogo au kuoa wake wengi iliyoasisiwa vijijini; na kurithishwa, hasa mijini, ni mwendelezo uleule wa kuwa na wake wengi lakini kwa kificho? Au hii ni "trend" tofauti?

5. Je, tunaweza kusema ya kwamba huyu mzee ameamua kuondoa kabisa unafiki na kuweka mambo wazi, akiashiria na kuitangazia dunia ya kuwa mwanaume kutokana na nature yake hatosheki na mke mmoja? Je, kwa mustakabali huu "is he a hero"?

Kwa kweli nina maswali mengi ambayo nimejiuliza lakini niishie hapa. Wadau bila shaka na nyie mtajiuliza maswali mengi na sote kwa pamoja tunaweza kujadili.
 
Last edited by a moderator:
mambo ya kijijini hayo
ngo'mbe is every thing
babu yangu mwenyewe alikuwa na wake watano(5)
na mke wa mwisho alimwoa akiwa in his late 70s na wakaza mtoto mmoja
wanawake wa kijiji kuridhishwa kimapenzi its not a big deal
na kuna adhabu kali za ku cheat ikiwamo kuwa outcasted (na refer kijijin kwentu)

hawa wa mujini wameshjua kuna orgasm utawambia nini?
 
Ungefanya la maana sana kama ungemtafuta Mzee Mrii ukaongea naye...
 
Mkuu Simplicity. mimi naamini kwa mke mmoja tu kulingana na imani yangu lakini baba yangu ana wake zaidi ya watano.

Siku moja tukiwa kwenye moja moto moja baridi, zikawa zimepanda kichwani. Akapita mtoto mkali msure akamtolea macho(Mzee wangu anakaribia 70), nikamchimba mkwara msure akacheka sana akaniuliza swali ambalo kila nikitafakari najikuta natabasamu tu;

Kuna vijiji viwili, kimoja kina wanaume 100 na mwanamke 1 na kingine kina mwanaume 1 na wanawake 100, kipi kiko fertile? Wapi maisha yanaweza kuongezeka kwa urahisi?

Nikajiuma uma paleeee,, akaniambia tunywe bia mwanangu!!!
 
Last edited by a moderator:
mambo ya kijijini hayo
ngo'mbe is every thing
babu yangu mwenyewe alikuwa na wake watano(5)
na mke wa mwisho alimwoa akiwa in his late 70s na wakaza mtoto mmoja
wanawake wa kijiji kuridhishwa kimapenzi its not a big deal
na kuna adhabu kali za ku cheat ikiwamo kuwa outcasted (na refer kijijin kwentu)

hawa wa mujini wameshjua kuna orgasm utawambia nini?

Ina maana hawaridhishwi mkuu?
 
Zamani maisha hayakuwa magumu kama sasa hivi. Kuwa na familia kubwa ni mzigo hasa kama uwezo wako kiuchumi ni mdogo.
 
huyu ni cha mtt, kuna mzee wa kimasai maeneo ya umasaini sikumbuki vizuri jina la kijiji yeye anakijiji kabisaaa manake ana wake zaid ya 15 na ana watoto usipime kiasi kwamba ilibidi ajengewe shule ya kusomesha wanawe na mpaka leo wanawe tuu ndi wanaosoma hapo kwenye hiyo shule.

huyo ni mmoja mwingine nimjuaye ambaye ana wake zaid ya 5 ni Dr Bake yeye ni surgeon wa orthopedic huwa anaoa vibnti vizuri usipime na kila mke anajengewa nyumba na uhakika wa maisha, sasa jiulize dr kama yule ana mke mtoto wa 20's unategemea nini??

muda mwingine ni kwamba wanaume wanaopenda kuoa wake wengi wanaambatana na uwezo wao ulio juu ya uwezo wa mwanadamu, si hivi hivi jamani manake inekuwa ni kama kawaida basi wanaume wengi tuu wangekuwa na wake weng namna hiyo. naamin ni watumiaji wazuri wa madawa ya kuongeza nguvu sio uwezo wa kibinadamu kabisa
 
Unajua mie nawaza maisha ya sasa huku mjini na mtu akaoa wake 10 ......

Maisha yanabadilika sana na perception pia towards things zinabadilika..........
 
Lamarkisim theory state that kadri kiungo unavyokitumia na ufanisi wake unaongezeka na usipokitumia kinakuwa dhaifu na kinaweza kutoweka kabisa ila kuna habari nilisoma kuwa kuna Mzee mmoja Nigeria ana wake 86 na mahakama ya kidini imeshindwa kuwaachanisha,
 
naomba nijibu no. 2, kuoa wake wengi ni mila na tamaduni za Africa ukiangalia kabila kama wasukuma wenyewe bado wanaoa mke zaidi ya mmoja na hawaoneani wivu wao huoa kwa ajili ya kuzalisha mali, kuna mzee mmoja msukuma Tabora ana wake wa nne na nitajiri kila mke anayemuoa anakabidhiwa shamba na mifugo na watoto wanaozaliwa huangalia mali na kuziendeleza. walipokuja wamissionary walihamasisha ndoa ya mke mmoja so this is about mila na tamadun ambazo makabila mengine Africa yanaziendeleza
 
.....

Overview/comments/questions/

1. Je huyu mzee anatoa wapi nguvu ya kuwaridhisha wake zake wote 12 na mahawara wengine, wakati tunaona na kusikia kila leo hasa hapa mujini Darisalama watu wenye mwanamke mmoja tu wanakimbiwa na wake zao kwa tatizo la kushindwa kuwaridhisha? kumbuka mzee kasema hana kazi zaidi ya kuzunguka nyumbani kwa wakeze kuwaridhisha. this isn't applicable darisalama.

2. Ni kwa nini wanawake waendelee kumkubali na kuolewa na mzee Mrii wakati tayari wakijua kuna msururu wa wanawake wengine ambao tayari alikuwa amewaoa? he is rich and can provide security na matunzo for them na watoto wao. its the same as wadada wanaojilengesha kwa mapedeshe

3. Kwa nini hapakuwa na ugomvi dhahiri kati ya Mzee Mrii na wake zake badala yake wake zake tu ndio wanaogombana? Ndio tuseme alitumia mbinu ya "divide and rule"? mke kijijini ni vigumu kugombana na mumewe 'kwa dhahiri'. pia 'hawajaharibiwa' na dhana ya 1man+1woman

4. Je, hii dhana na uhalisia wa nyumba ndogo au kuoa wake wengi iliyoasisiwa vijijini; na kurithishwa, hasa mijini, ni mwendelezo uleule wa kuwa na wake wengi lakini kwa kificho? Au hii ni "trend" tofauti?

5. Je, tunaweza kusema ya kwamba huyu mzee ameamua kuondoa kabisa unafiki na kuweka mambo wazi, akiashiria na kuitangazia dunia ya kuwa mwanaume kutokana na nature yake hatosheki na mke mmoja? Je, kwa mustakabali huu "is he a hero"?

Kwa kweli nina maswali mengi ambayo nimejiuliza lakini niishie hapa. Wadau bila shaka na nyie mtajiuliza maswali mengi na sote kwa pamoja tunaweza kujadili.
couldn't answer 4&5
 
naomba nijibu no. 2, kuoa wake wengi ni mila na tamaduni za Africa ukiangalia kabila kama wasukuma wenyewe bado wanaoa mke zaidi ya mmoja na hawaoneani wivu wao huoa kwa ajili ya kuzalisha mali, kuna mzee mmoja msukuma Tabora ana wake wa nne na nitajiri kila mke anayemuoa anakabidhiwa shamba na mifugo na watoto wanaozaliwa huangalia mali na kuziendeleza. walipokuja wamissionary walihamasisha ndoa ya mke mmoja so this is about mila na tamadun ambazo makabila mengine Africa yanaziendeleza

Kwa hiyo mkuu huu mfumo wa kimissionary wa kuoa mke mmoja ndio huenda unatusumbua, maana inaonekana sio asili ya mwafrika kabisa? Si unajua kuiga kitu ambacho hujakulia nacho inavyokuwa shida, au unasemaje?
 
dah, hawa wazee wana nguvu kama za scania!
 
Last edited by a moderator:
Jamani ni msingi walojenga kwa chakula halisi wakati ule. Wanaweza ndo maana wake huridhia. Punguzeni ukisasa wakati huu.
 
Back
Top Bottom