A deep analysis of yanga vs Silver Strikers..

A deep analysis of yanga vs Silver Strikers..

Its Pancho

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
16,748
Reaction score
28,138
I salute you kinsmen
Tumevuka makundi, tumeshinda
Lakini kuna namna tujipange mapema sana huko mbele pagumu sana

Dakika 45 za kwanza Yanga walionesha mchezo ambao tofauti kabisa na ule uliofanyika Malawi wiki iliyopita

1: Kulikuwa na kasi ya mchezo sana
Wachezaji hawakukaa na mali ilikuwa inaguswa tuondoke. 🔥

2: Umakini wa pasi hasa kwenda mbele
Kazi ilifanywa vyema na Duke abuya. Mo doumbia japo huyu alipoteza baadhi ya mipira sana, hana fitness nzuri. Ila ana akili ya mpira na uwezo mzuri wa kuutuma mpira anakosa kimoja tu ni fitness yake

3: Uzuiaji wa counter attacks ulikuwa mzuri
Duke abuya, dickson Job, bacca walifanya kazi vizuri sana huku Dube na wenzie mbele wakipress sana.

4: Kushinda mipambano yao uwanjani
Silver Strikers wanapenda kugongana sana hili yanga walilijua na walikuja wamejipanga.

Silver Strikers uzuiaji wao wa 4-4-2 bila mpira , ilikuwa ni suala la Job , Bacca na Diarra watafanikiwa vipi kuwatafuta na kuwapata viungo wao wawili wa kati ( Abuya & Mudathir / Maxi )

ambao mara nyingi walikuwa wanaombe mpira nyuma ya mstari wa ushambuliaji wa wapinzani wao ( na ndio ilikuwa inawasaidia kufika haraka kwenye lango la Silver Stikers hasa Doumbia naye akiongezeka akitokea nyuma ya mstari wa kiungo wa Silver )

Silver Strikers nguvu yao kubwa ni ' Short Passing game ' na mara kadhaa ambazo walikuwa wanajaribu kufanya hivyo walikuwa :-

A) Wanatunza sana mpira hasa kuanzia nyuma na kiungo
mara kdahaa walifanikiwa kuondoka na mpira na kufika kwenye box la yanga

B) Wanawafanya Yanga kuutafuta sana , na kupunguza energy level ya Yanga
ikafikia wakati Dube akachoka kuzunguka mbele pale peke yake tu.

C) Wanasogea juu kwa pamoja wakiwa wengi
na hii iliwacost mara kadhaa kwani ubutu wa Dube na Edmund john ulifanya wqkasalimika otherwise chuma nne zilikuwepo nyavuni leo.


D) Shida yao ilikuwa moja tu : Maamuzi sahihi katika nyakati sahihi na kulazimisha mipira mirefu ambayo kwa Yanga ilikuwa rahisi kwao na kuishia vichwani kwa bacca na job tu na kurudishwa kwa kiungo cha yanga

✍Kipindi cha pili Yanga walionekana level ya Fitness kuwa chini ( kwa wachezaji kadhaa ) ambayo inaathiri kwa kiasi chake utendaji wa timu nzima : Maana yake ile intensity ya uzuiaji ikashuka na kushambulia wanakuwa wachache ( licha ya nafasi bora sana walizotengeza kipindi cha pili )

Hapa kocha wa viungo wa yanga ana la kujibu
Team iko down na inakata moto kipindi cha pili
While yanga ya mwanzo ilikuwa kipindi cha pili ndio kama wanaanza mechi!
Hii sio yanga tuliyoizoea.

MUHIMU..

1: Silver Strikers wana uwezo mzuri wa short passing game na rotations ya wachezaji kupata spaces kwa urahisi sana hata kipa wao yupo vizuri sana mguuni. Shida iko kwa maamuzi mbele pale, bado wana wachezaji wenye mentality ndogo.

2: Job na Bacca kwenye kuzuia kama waki switch one wanakuwa hodari sana
Kiwango kizuri sana

3: Abuya energy yake na intensity kwenye kuzuia na kusogea juu inawapa Yanga uimara He is my best player tangu anakuja yanga 🔥 mtoto wa Tate Mkuu

4: Yanga kama utulivu ungekuwa mkubwa basi 4-0 zingekuwepo leo
dube aache mawenge na bahati mbaya anayechukua nafasi ni boyeli naye maji kupwa maji kujaa.
Dube ilibidi tu aombe kubadilishwe mwenyewe baada ya kukosa ile nafasi ambayo kama ile ile pacome alifunga yeye pia akakosa mwanzo first half

6: Pacome : Yanga wanahitaji huyu awe fit sana msimu mzima huu. He is so good 🔥 anafanya vitu vitokee hata kwa lazima na leo ameibeba mechi mwenyewe
Wamemnyima sana assist wenzie wakina Dube na kina Edmund.

Yanga watahitaji mzize arudi haraka sana uwanjani

Tumkaribishe kocha Pedro sasa na kumuacha ajenge team kwa sasa,
Yanga hakuna kocha kwa sasa Mabedi amekaimu tu pale.

NB: Kuna team haijafuzu mjue bado? Zaidi kuna mchezaji kawakimbia na walimtabiria mabaya leo kaanza mechi nzima na kafuzu makundi🤣
1761408075482.jpg


Its Pancho
 
Leo Duke Abuya ameondoa kitendawili kilichomshinda Romain Folz! Mpaka anafukuzwa, aliamini Yanga haina kiungo mkabaji zaidi ya Aziz Andabwile!!

Huko aliko atakuwa amejionea mwenyewe namna Uchizi alivyofanyiwa uchizi na Mchizi mwenzake kutoka Kenya. Hakika leo wachezaji wametirejeshea furaha.

NB:- mpaka muda huu ni timu ya simba pekee ndiyo bado haijafuzu kuingia makundi. Timu nyingine 3 zinasubiria tu droo itakayo chezeshwa Jumatatu.
 
Umetazama vipi mpira hata kuona kama Doumbia amecheza mchezo wa kawaida.

kwangu mimi, Doumbia ni bonge la Player kwa umri wake. Leo kwangu waliotubeba ni Abuya, Doumbia na Pacome.
Sikufichi leo ukiniambia nikutajie mchezaji aliyeubonda na kutubeba basi Doumbia.

Huyo jamaa ninemfatilia sana leo ni bonge moja la mchezaji.

Ni football brain kali sana.

Changamoto kubwa ni fitness tu.
 
Umetazama vipi mpira hata kuona kama Doumbia amecheza mchezo wa kawaida.

kwangu mimi, Doumbia ni bonge la Player kwa umri wake. Leo kwangu waliotubeba ni Abuya, Doumbia na Pacome.
Elewa between lines
Doumbia nimesema hana fitness angalia vizuri mkuu

Anakosa stamina nzuri ana akili ya mpira sana na uwezo ila hana fitness nzuri
Kumbuka hakucheza mwaka mzima

Sijasema mbaya nionyeshe.
 
Sikufichi leo ukiniambia nikutajie mchezaji aliyeubonda na kutubeba basi Doumbia.

Huyo jamaa ninemfatilia sana leo ni bonge moja la mchezaji.

Ni football brain kali sana.

Changamoto kubwa ni fitness tu.
Yes mkuu hiki ndio nakisemea haoa soma hapo kwenye analysis yangu nilichosema jamaa hana fitness nzuri

Hakucheza mwaka before hajaja yanga ila nashangaa jamaa mwenzangu anasema nimesema mchezaji.wa kawaida eti

Doumbia ni mashine
 
Edmund sio mchezaji wa kawaida mkuu, ni mchezaji mzuri sana sana.
Ana papara sana akitulia tu mbona hapo mchezaji yupo

Ila tusidanganyane imagine leo una mechi na alhy ahly utampanga aanze? Hapana unahitaji heavyweight kama mzize
 
Sikufichi leo ukiniambia nikutajie mchezaji aliyeubonda na kutubeba basi Doumbia.

Huyo jamaa ninemfatilia sana leo ni bonge moja la mchezaji.

Ni football brain kali sana.

Changamoto kubwa ni fitness tu.
Dakika 10 za mwanzo zinatosha kabisa kukwambia Doumbia ni tishio. Tungeanza na kocha mzuri toka msimu kuanza, tungemuona katika kiwango chake bora kabisa.
 
Leo Duke Abuya ameondoa kitendawili kilichomshinda Romain Folz! Mpaka anafukuzwa, aliamini Yanga haina kiungo mkabaji zaidi ya Aziz Andabwile!!

Huko aliko atakuwa amejionea mwenyewe namna Uchizi alivyofanyiwa uchizi na Mchizi mwenzake kutoka Kenya. Hakika leo wachezaji wametirejeshea furaha.

NB:- mpaka muda huu ni timu ya simba pekee ndiyo bado haijafuzu kuingia makundi. Timu nyingine 3 zinasubiria tu droo itakayo chezeshwa Jumatatu.
Na hapo bado Duke namba sita sio namba yake halisi anacheza tu akipangwa popote

Jamaa anajituma sana mpaka uchizi vunga kafanyiwa sub sio kazi ndogo
Duke yuko fit sana
Fitness ya Duke angekuwa nayo Doumbia leo mbona ingekuwa balaa

Doumbia anahitaji sana stamina yake irudi hajacheza mechi za ushindani muda mrefu
Jamaa anaubonda sana na ana akili ya mpira sana
 
Umetazama vipi mpira hata kuona kama Doumbia amecheza mchezo wa kawaida.

kwangu mimi, Doumbia ni bonge la Player kwa umri wake. Leo kwangu waliotubeba ni Abuya, Doumbia na Pacome.
Sio mchezaji mbaya changamoto yake ni ana stamina ndogo tu hajacheza mechi za ushindani muda mrefu mwaka mchezo nini?

Akikaa sawa ndio tutampenda zaidi ya hapa
 
Na hapo bado Duke namba sita sio namba yake halisi anacheza tu akipangwa popote

Jamaa anajituma sana mpaka uchizi vunga kafanyiwa sub sio kazi ndogo
Duke yuko fit sana
Fitness ya Duke angekuwa nayo Doumbia leo mbona ingekuwa balaa

Doumbia anahitaji sana stamina yake irudi hajacheza mechi za ushindani muda mrefu
Jamaa anaubonda sana na ana akili ya mpira sana
Sahihi kabisa. Doumbia anahitaji mazoezi maalum ya kumuongezea utimamu wa mwili na kasi awapo uwanjani. Ana kitu. Ila shida iko kwenye hivyo vitu viwili.

Dube naye anahitaji sana utulivu na akili ya haraka kwenye maamuzi yake. Papara, kutojiamini, na kukosa akili ya kufanya maamuzi ya haraka; kunapunguza sana uwezo wa kujiamini kwa mshambualiaji.
 
Dakika 10 za mwanzo zinatosha kabisa kukwambia Doumbia ni tishio. Tungeanza na kocha mzuri toka msimu kuanza, tungemuona katika kiwango chake bora kabisa.
Hata sio swala la kocha pekee mkuu
Issue ni Doumbia anahitaji mechi zaidi ili kurudisha utimamu wake wa mwili mechi kama hizi ndio anahitaji zaidi

Nakuhakikishia hii ni nusu ya uwezo wake tu, ngoja akae vizuri tutamuimba sana mpaka na studio watu watamtungia wimbo
 
Sahihi kabisa. Doumbia anahitajo mazoezi maalum ya kumuongezea stamina na kasi awapo uwanjani. Ana kitu. Ila shida iko kwenye hivyo vitu viwili.

Dube naye anahitaji sana utulivu na akili ya haraka kwenye maamuzi yake. Papara, kutojiamini, na kukosa akili ya kufanya maamuzi ya haraka; kunapunguza sana uwezo wa kujiamini kwa mshambualiaji.
Kweli kabisa naunga mkono hoja mkuu

Doumbia akiwa fit mbona Tanzania hii tutamsahau na aziz ki kabisa?
Fikiria tu mpaka aziz anamrecomend Doumbia kwa injinia kuwa jamaa anajua unadhani uongo hapo? Doumbia bado hawezi kucheza dakika 90 full kama kina Duke lazima atoke tu dakika za 70 ila jamaa anaujua sana sana sana mpira.

Dube sijui anakumbwa na nini? Naona anacheza kwa pressure sana inamfanya anakuwa na kitete mguuni sana
Hebu angalia pasi ile pacome, pale Dube alikuwa anatap in tu pale ila akataka atulize na alikuwa karibu na goli vile??

Ninachokiona jamaa ana pressure sana hasa hizi za mitandaoni
Arudishiwe kujiamini kwake kama Miloud alivyomuamini

Hakupaswa kutoka pale hata kama aliomba sub kiuhalisia imemuumiza sana pale nje hata sisi mashabiki tumeumia sana
 
Kabisa mimi nlishangaa sana alivyotoka.

Huyo jamaa ni suala la wakati tu tutaanza kumuimba kama tunavyomuimba Pacome sasa hivi.
Doumbia hawezi kumaliza mechi kumbuka pale jopo linaangalia fitness yake kwenye vile vi vidude wanawekewaga mgongoni kwenye vile ci catapult vile

Jamaa anahitaji kucheza mechi za usbindani nyingi hapa mbona bado sio Doumbia mwenyewe? 🤣

Subiri mpaka katikati ya msimu utaona mbona mpaka pacome tutamsahau? Doumbia ni mali sana
 
Back
Top Bottom