ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,017
- 7,220
Bei ya ngozi yaporomoka
Na Mwandishi wetu
21st May 2009
Bei ya ngozi imeporoka kutoka Sh 2,000 kwa kilo hadi Sh.500, imefahamika.
Hayo yalisemwa jana na Naibu Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Nelson Kilongozi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya zao la ngozi yanayotolewa kwa wataalam 25 wa ugani nchini yanayofanyika katika Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Tengeru.
Kilongozi alisema alisema bei ya ngozi hiyo kavu imeporoka kwa kasi katika soko la ndani na nje ya nchi na kusababisha wafugaji kukosa mapato ya kutosha.
Alisema ngozi mbichi nayo bei yake imeporomoka kutoka Sh 1,200 kwa kilo hadi kufikia Sh 300.
Hata hivyo, Kilongozi alisema wameunda kikosi kazi kinachotarajiwa kushirikiana na wadau wengine nchini kuinusuru sekta ya ngozi na kwamba utaoji wa mafunzo kwa maafisa ugani hao ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati huo.
Alisema mafunzo hayo yamemepewa kipaumbele kikubwa kwa sababu yanatarajiwa kutolewa kwa wagani kutoka halmashauri 75 nchini.
Alisema awamu ya kwanza ya mafunzo hayo yanayotolewa kwa wagani wa halmashauri 25 katika Chuo hicho yatagharimu zaidi ya Sh. Bilioni 50 .
Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isdore Shirima alisema sekta hiyo inaendelea kukabiliwa na changamoto ikiwamo ya kushuka kwa bei ya ngozi na kunakochangiwa na sababu mbalimbali ikiwamo ya mtikisiko wa uchumi duniani
Shirima alisema mtikisiko huo pia umeathiri soko la mazao ya mengine ya mifugo yakiwamo maziwa lililokuwa limeanza kuwanufaisha wakazi wa Mkoa wa Arusha kwa kuuza bidhaa hiyo kwenye hoteli za kitalii .
Alisema serikali inaendelea kukabiliana na changamoto hizo na kuwataka wadau wa sekta hiyo kuendelea kuhamasisha soko la ndani la mazao ya mifugo.
CHANZO: NIPASHE
Na Mwandishi wetu
21st May 2009
Bei ya ngozi imeporoka kutoka Sh 2,000 kwa kilo hadi Sh.500, imefahamika.
Hayo yalisemwa jana na Naibu Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Nelson Kilongozi wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya zao la ngozi yanayotolewa kwa wataalam 25 wa ugani nchini yanayofanyika katika Chuo cha Maendeleo ya Mifugo Tengeru.
Kilongozi alisema alisema bei ya ngozi hiyo kavu imeporoka kwa kasi katika soko la ndani na nje ya nchi na kusababisha wafugaji kukosa mapato ya kutosha.
Alisema ngozi mbichi nayo bei yake imeporomoka kutoka Sh 1,200 kwa kilo hadi kufikia Sh 300.
Hata hivyo, Kilongozi alisema wameunda kikosi kazi kinachotarajiwa kushirikiana na wadau wengine nchini kuinusuru sekta ya ngozi na kwamba utaoji wa mafunzo kwa maafisa ugani hao ni sehemu ya utekelezaji wa mkakati huo.
Alisema mafunzo hayo yamemepewa kipaumbele kikubwa kwa sababu yanatarajiwa kutolewa kwa wagani kutoka halmashauri 75 nchini.
Alisema awamu ya kwanza ya mafunzo hayo yanayotolewa kwa wagani wa halmashauri 25 katika Chuo hicho yatagharimu zaidi ya Sh. Bilioni 50 .
Akifungua mafunzo hayo, Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Isdore Shirima alisema sekta hiyo inaendelea kukabiliwa na changamoto ikiwamo ya kushuka kwa bei ya ngozi na kunakochangiwa na sababu mbalimbali ikiwamo ya mtikisiko wa uchumi duniani
Shirima alisema mtikisiko huo pia umeathiri soko la mazao ya mengine ya mifugo yakiwamo maziwa lililokuwa limeanza kuwanufaisha wakazi wa Mkoa wa Arusha kwa kuuza bidhaa hiyo kwenye hoteli za kitalii .
Alisema serikali inaendelea kukabiliana na changamoto hizo na kuwataka wadau wa sekta hiyo kuendelea kuhamasisha soko la ndani la mazao ya mifugo.
CHANZO: NIPASHE