Rashda Zunde
JF-Expert Member
- May 28, 2022
- 291
- 281
Serikali imesema nyongeza ya mishahara 23% iliyotangazwa mwaka huu 2022, inawalenga watumishi kati asilimia 75 hadi 78 wanaopokea mishahara midogo, na siyo wenye mishahara mikubwa kama vile Mawaziri, Makatibu Wakuu na Wakuu wa Mikoa.
Ufafanuzi huo umetolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo tarehe 29 Julai 2022 na kusema kwamba ni kweli kwamba 23% iliyotamkwa haijalipa watu wote na ni kwasababu wa kanuni inayotumika katika kutamka viwango vya mishahara na kinapotamkwa wanaonufaika si wote mpaka wa mishahara mikubwa, wanaonufaika ni wale wa kada ya chini.
Na huku juu kwa watumishi wenye mapato makubwa hawapati ile percentage (asilimia) ilivyo kwasababu ukiwalipa kwa ile 23 watakuwa wameenda mbali zaidi ya hawa wachini kwahiyo gap (nafasi) litakuwa kubwa zaidi.
Ufafanuzi huo umetolewa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo tarehe 29 Julai 2022 na kusema kwamba ni kweli kwamba 23% iliyotamkwa haijalipa watu wote na ni kwasababu wa kanuni inayotumika katika kutamka viwango vya mishahara na kinapotamkwa wanaonufaika si wote mpaka wa mishahara mikubwa, wanaonufaika ni wale wa kada ya chini.
Na huku juu kwa watumishi wenye mapato makubwa hawapati ile percentage (asilimia) ilivyo kwasababu ukiwalipa kwa ile 23 watakuwa wameenda mbali zaidi ya hawa wachini kwahiyo gap (nafasi) litakuwa kubwa zaidi.