2020 CCM inafutika na kubaki historia

2020 CCM inafutika na kubaki historia

Mathias Raymond Nyakapala

JF-Expert Member
Joined
Mar 1, 2017
Posts
2,181
Reaction score
1,494
Create Date: 1/18/2018 14:59
KWA MATOKEO YA UCHAGUZI MDOGO HUU NAONA 2020 KAZI NI NYEPESI SANA SANA.......

Na;Mathias Raymond Nyakapala

Naandika haya kwa kalamu yangu ya mia mbili kutokea katikati ya Nchi yetu ya Tanzania,Katikati ya Kanda ya Kati,Katikatika ya Mkoa wa Dodoma na pia ni Katikati ya Wilaya ya Dodoma Mjini.Tukiwa tunaishi kwenye obwe la Mipasuko na usumbufu kwasababu za Kisiasa,Kijamii na Kiuchumi na ukisema kweli hali sio shwari pande zote ndo maana sishangai kuona Mbunge wa Chemba anataka muda uongezwe maana anaogopa Uchaguzi hana alilotekeleza wala la kuonyesha kama Ahadi alizotoa wakati wa Kampeni na hali ipo hivyo karibia majimbo yote yaliyopo chini ya Chama Cha Manunuzi(CCM).

Poleni na majukumu Watanzania wenzangu tulio na jambo kwenye mioyo yetu na tunafahamu tutalitoa siku moja 2020 kutokana na majibu,Kero kubwa tunazokutananazo kwenye maisha yetu ya kila siku,hii yote ni baada ya CHAMA CHA MANUNUZI kuona vipaumbele vyao ni kutengeneza Propaganda na kununua Viongozi,bendera,wanachama na wafuasi wa vyama vya upinzani pia kuwanunua na Wananzuoni wenye misimamo ili kuteka vyombo vya habari na kuvihamisha kwenye Ajenda za msingi ambazo ni kuwaletea maendeleo Watanzania LAKINI MATOKEO YA UCHAGUZI HUU MDOGO UKIANGALIA IDADI YA WAPIGA KURA WALIOPO MAENEO HUSIKA NA WALE WALIOPIGA KURA.........ukiona watu hawajajitokeza kupiga kura ujue Wamejiuliza wanampigia kura nani maana ya kutokupiga kura wameona hakuna sababu na wanasubiri 2020.lakini naomba na wewe ujiulize Kwanini tunapiga KURA na weka uhusiano na matukio yanayoendelea sasa kisha ukipata majibu.......unaisaidiaje jamii?

MIMI NIMEJIULIZA.......

00.Nimejiuliza kwanini tunapiga kura baada ya Uchaguzi mkuu kila baada ya miaka Mitano kupita baada ya Uchaguzi mmoja,nadhani majibu hayatakuwa na uhusiano na Manunuzi ya Viumbe hai dhaifu hawa wanaonunuliwa siku hizi ambao kimsingi ukijiuliza MTU AMECHAGULIWA NA WANANCHI HAO HAO NA KUSHINDA UCHAGUZI KWA SHIDA SANA SEHEMU NYINGINE IMEPELEKEA WATU KUUMIA AU KUUWAWA WAKIMPIGANIA LEO ANAAMUA KUJITOA NA KWENYE NAFSI HIYO KWA KUNUNULIWA NA CCM SIKU CHACHE ANARUDISHWA TENA KUOMBA NAFSI ILE ILE ALIYOJIHUDHURU KWENYE JIMBO AU KATA ILE ILE mmesahau nini au Wapiga kura kwenye eneo husika mmewadharau kiasi gani nyinyi CCM?

01.Ukijiuliza kwanini tunapiga kura hautakuta uhusiano wa moja kwa moja na Hautakuta kuna uhusiano wowote na Viongozi kukamatwa na polisi, hautakuta uhusiano wowote na Wananchi kuuwawa au kupotea,Hautakuta uhusiano na Machinga kubomolewa na kusumbuliwa haswa Dodoma Mjini.

02.Ukijiuliza kwanini tunapiga kura hautakuta uhusiano na Risasi wanazopigwa Viongozi wetu(viongozi wenye ufuasi mkubwa)mfano wa LISSU zaidi utakuta kuna uhusiano mkubwa wa Wananchi kuikataa CCM kwenye maeneo ambayo viongozi wao wamepatwa na madhara hayo.lakini naomba nikumbushe Abraham's Lincoln alivyowahi kusema nanukuu.

"BALLOT IS STRONGER THAN THE BULLET"

03.Ukijiuliza kwanini tunapiga kura Hautakuta uhusiano wowote na Zuio la mikutano ya Hadhara na Kuingiliwa kwa Mahakama na Bunge,hautakuta uhusiano wowote na Waandishi wa habari kupotezwa na kutekwa pia hautakuta uhusiano wowote na Vitisho na kuwafirisi Viongozi wa Vyama vya Siasa na Wafanyabiashara.

JE CCM HAWAJUI KWANINI TUNAPIGA KURA NA NANI WANATAKA AWAAMBIE KWANINI TUNAPIGA KURA? MBONA WAMEACHA YALIYO MAMBO YA WANANCHI NA WANAJIFANYIA YA KWAKO TENA MENGI HAYANA MAANA YOYOTE MFANO KUNUNUA VIONGOZI NA KURUDIA UCHAGUZI KWA GHARAMA KUBWA BILA SABABU?

[HASHTAG]#2020tukutaneballot[/HASHTAG]

Mtazamo wangu"Serikali yoyote Duniani ikikosa VIPAUMBELE NA NAMNA YA KUVISIMAMIA itajikuta imedharisha Masikini wengi kwenye Jamii husika lakini pia UKIZALISHA MASIKINI wengi kwenye jamii maana yake AMANI imekaribia kutoweka".

Endeleeni kuwafanya Matajiri wawe masikini na Masikini kuwa Masikini zaidi siku zinahesabika.
 
20180118_145302.png
 
Makala yako uliyoandika kwa kalamu ya 200, nimeielewa vema yani kuna mambo huwa yananisumbua katika kichwa nikiamua kuyaandika mtachoka kusoma,nawe nimeona umehoji endelea kuhoji, ila usifikiri wanayofanya hawajui, wanajua vizuri.
 
Makala yako uliyoandika kwa kalamu ya 200, nimeielewa vema yani kuna mambo huwa yananisumbua katika kichwa nikiamua kuyaandika mtachoka kusoma,nawe nimeona umehoji endelea kuhoji, ila usifikiri wanayofanya hawajui, wanajua vizuri.
Ni kweli mkuu najua wanafahamu wanafanya nini lakini nimeamua kusema maana NENO LINAUMBA
 
Mleta mada ukiwa na mawazo hayo ndio maana wanasiasa wanafanikiwa kuwachezea akili watu. Unaambiwa kakae mita 200 juani eti unalinda kura au kuna barua inatoka ICJ ya kuzuia Jpm kuapishwa!
Mkuu mwananchi huru anaruhusiwa kidogo kijieleza na kusema hisia zake kwenye hii Nchi
 
Ukiota ndo utume sms ya kumtukana RC Gambo?

Siku hizi Mbona haoti Tena ?
Ndoto aliyootaga Lema hakutuma sms kwa mtu ila alitueleza Watanzania wenzake lakini walimkamata ikiwa na maana wanatulazimisha mpaka kuota iwe wapendavyo wao!
 
Mi nikiona mtu bado anaandika mambo ya kununua viongozi namuona kama shi..le. Kwani kama unamke umeoa alafu jirani akimpa vichipsi tu anaachia goli ndiyo utakuja kutusumbua mtaa mzima kwa sasabu ya tabia ya mke wako.
Tusikurupuke na mahaba fikiria kidogo.
Mkuu wewe ulichoona kwenye hiyo makala ni kununua Viongozi tu?au ndo jambo unaweza kulieleza kwa uelewa wako?
 
Back
Top Bottom