Balali kasalitiwa?

Kithuku

JF-Expert Member
Nov 19, 2006
1,395
207
Nimetafakari wasifu wa aliyekuwa Gavana wa BoT Dr. Daudi Timoteo Saidi Balali, na sijaweza kuona sababu ya mtu aliyekuwa na wasifu na kipato kizuri sana (hata kabla ya huo ugavana) kujihusisha na wizi wa aina yoyote. Nahisi kuna usaliti aliofanyiwa, na inawezekana siku zote ambazo tulikosa habari zake kuna watu walizizuia kwa makusudi.

Hiki kipande hapa chini nimekinakili kwenye ripoti iliyoandikwa mwaka juzi tu, 2006. Haiingilii akilini kuwa mtu anayezungumziwa hapa anaweza kuwa fisadi kwa kiwango tunachosadikishwa. Simjui huyu mtu, simtetei kwa chochote, natafakari tu kwa kutumia habari zilizopo kumhusu:

"The Bank of Tanzania's unassuming and diminutive governor is 64-year old Mr. Daudi Balali. Having worked for the IMF in Washington for 21 years and headed missions to Kenya, Ghana, Lesotho, Somalia, Swaziland, Ethiopia, Sierra Leone, and South Africa, Governor Balali was handpicked for the job in 1998 by former President Benjamin Mkapa. Mkapa had watched the younger Balali achieve significant results in both Ghana and Ethiopia. The post represented a return to the BOT for Governor Balali, who had previously held the position of Director of Research at the Bank of Tanzania before he joined the IMF. However, whilst the Governor's experience on the continent has proved an invaluable resource for the Tanzanian government, it was his connections with the IMF and World Bank which tipped the scales in Tanzania's favor. Tanzania has not only shed the basket case image it was burdened with in the 1990's – it is now regarded as one of the best managed economies on the continent, and has excellent relations with the development partners, largely because of the relationships which the Governor has been leveraging during his tenure. The Governor's family has remained in Washington, a city to which he is a frequent visitor. All this is a very far cry from Mr. Balali's humble beginnings. The Governor was one of the first Tanzanians to win a scholarship to study in the United States, where he studied at Harvard, after making his first trip by boat across the Atlantic Ocean".

Ripoti hiyo kwa kina zaidi hii hapa: [media]http://www.smlstrategicmedia.com/pdf/Tanzania_report.pdf[/media]

Fumbo hili linatatulika?
 
mmmhhhhh! hii ngoma nzito.lakini, ofcourse upotevu wa pesa nyingi vile ni lazma kuwe na collusion
 
1.
Nimetafakari wasifu wa aliyekuwa Gavana wa BoT Dr. Daudi Timoteo Saidi Balali, na sijaweza kuona sababu ya mtu aliyekuwa na wasifu na kipato kizuri sana (hata kabla ya huo ugavana) kujihusisha na wizi wa aina yoyote.

Mwizi ni mwizi, na kiongozi yoyote asiyekuwa mwizi hujitenga na tuhuma za wizi kwa kusema ukweli tena at the right time, kama Balali hakuwa mwizi alikuwa na kila haki ya kusema ukweli, sasa hivi tayari runajua kuwa kuna hela nyingi sana zilizoibiwa huko BOT kwa ruhusa yake,

Ninazo dataz zote hata alivyojaribu kujiweka sawa kwa kuwapa wabunge wawasha moto hela za bure kutoka huko, ili wanyamaze, mmojawapo akiwa Mzindakaya, ambaye according to the dataz ni kwamba origianlly alikuwa na deni la shillingi billioni 9 toka benki ya Standard, ambazo alishindwa kulipa kabisa wakati ulipowadia wa malipo tena ya kwanza, alipoona wanamjia juu Mzindakaya, akaamua kumfuata Balali, ambaye pamoja na kushindwa kwake kuwalipa Standard bank, Balali akaamua kumlipia anyways deni hilo,

Mkuu wangu hakuna gazeti lolote wala serikali ambayo imewahi kutuambia Mzindakaya alipataje ule mkopo wa BOT, huu ninaouweka hapa ndio ukweli wake na unamhusu Balali period! Je alifanya madudu mangapi huko BOT?

Kwa hiyo mkuu huwezi kutaka wananchi wakaandamane DC nyumbani kwa Balali, halafu hapa unakuja kumtetea kuwa hakuiba hela za taifa letu, sasa mbona unajichanganya mkuu?

2.
Nahisi kuna usaliti aliofanyiwa, na inawezekana siku zote ambazo tulikosa habari zake kuna watu walizizuia kwa makusudi.

Jamani sisi ni watu wazima hapa JF, zimetolewa habari za wizi wa watu wa karibu na rais wetu kama Lowassa, na Karamagi sasa zitakuwa za Balali? Eti kuna watu wamezizuia kwa makusudi? Yaaani hao watu wana nguvu mpaka ya kumzuzia Balali asiongee akiwa nje ya nchi? Usaliti? Alifanyiwa au alijifanyia mwenyewe?

Mkuu ninaamini kuwa una uwezo wa kufikiri zaidi ya hizi hoja finyu za kujaribu kumsafisha Balali, kiongozi yoyote msafi hawezi kuishia kwenye haya mazingara ya Balali, the matter of fact toka tupate uhuru hizi habari zake za sasa ni the best comedy ever, na ni lazima iende kitabu cha record za dunia za historia!
 
Mkuu mambo haya hapa

Ballali debate continues to dominate Bunge

THISDAY REPORTER
Dodoma

THE alleged involvement of Bank of Tanzania (BoT) Governor Dr Daudi Ballali in suspect multi-million dollar expenditures at the central bank yesterday continued to dominate parliamentary debate here, with lawmakers seemingly split in their opinions.

In an unexpected move, Chrisant Mzindakaya (Kwela - CCM), who declared himself an expert on BoT external commercial debt account affairs, stood up to defend Dr Ballali over the matter of some 200bn/- or so disappearing without explanation from the account.

The veteran MP offered to set the record straight by asserting that the amount of money said to have mysteriously vanished from the account ''was actually $131m (approx. 160bn/-), and not $200m (250bn/-) as suggested by opposition legislators.''

''I can say I am speaking with authority because I have already done a detailed research on this matter and have all the relevant information,'' Mzindakaya told parliamentarians here as debate on the 2007/08 government budget proposals entered a third day.

He said he had been briefed about the issue by two people, one a Tanzanian national and the other a Zimbabwean based in South Africa. But he did not name them in parliament.

Expressing support for the current move to conduct an official government audit of BoT, he said ''once this audit is completed, we will know the full truth about this matter.''

He added: ''According to my own research, the Bank of Tanzania is one of the top ten central banks in Africa.''

On the BoT Twin Towers construction project costs which have also raised many questions and much controversy, Mzindakaya asserted that there were no irregularities here either.

''People might now say that the new BoT headquarters building was too costly. But ten years from now, we will all be happy with the wise decision to build it,'' he said.

According to available records, Mzindakaya is the owner of Sumbawanga Agricultural and Animal Food Industries Limited (SAAFI), a new, ultra-modern meat processing company that is understood to have been set up through a long-term loan of 9.7bn/- from Standard Chartered Bank.

It is also understood that the credit line that SAAFI received from Standard Chartered Bank was expressly guaranteed by the BoT.

Contributing to the same debate yesterday, Ms Halima Mdee (Special Seats - CHADEMA) called on MPs across both sides of the political divide to set ideological differences aside for the sake of national interests.

She urged the government to thoroughly investigate the myriad of allegations raised against BoT, saying: ''It may be that these reports are either true or false�but they are very sensitive matters involving us as a country.''

Ms Mdee added that ''instead of trying to neutralise these issues and dismiss these reports as mere lies, we should back the government's stated intention to investigate.''

Opposition legislators have demanded an official statement from Finance Minister Ms Zakia Meghji regarding the alleged gross mismanagement of funds at the BoT. One of them, Dr Wilbrod Slaa (Karatu � CHADEMA) made a direct reference to allegations ostensibly aimed at Dr Ballali in person.

The MPs also slammed the controversial BoT Twin Towers project in Dar es Salaam, noting that the structure is said to have cost four times more than the cost of erecting a similar building in some of the world's most expensive cities like London, New York and Tokyo.
 
Wakuu linki hiyo ya dataz za balali..Lakini hakuna rekodi ya kifo!
Which ni jambo la kushangaza sana kwa hapa US!


Sign In to Intelius | Manage Account
Help: (88 445-2727 | View My Reports

Return to Home






clear-pix.gif
Get More Information on Daudi Ballali in Bethesda, MD
background checkphone searchCriminal CheckDaudi Ballali is 65 years old.Previous Locations for Daudi Ballali:1 in Philadelphia, PA
1 in Rockville, MD
1 in Silver Spring, MD
1 in Washington, DC
1 in Potomac, MD
1 more location in 1 other city...
Relatives of Daudi Ballali:Elizabeth Ballali
Rachel Ballali
Albina Ballali
progress.gif
 
Wakuu kuna huyu Daudi Kinyaga nina wasiwasi!
Nimeanzisha thread ya jina hilo na ninaomba mchango!
 
Mkuu ES

Aliyeanzisha hii thread ni mimi, wala si Kuhani Mkuu kama ulivyorejea wakati wa kuchangia. Hata hivyo mchango uliotoa unawaongezea members hapa nami nikiwepo ufahamu zaidi kuhusu hili tukio la Balali. Mimi nimeweka hiyo caption niliyonakili kutoka katika hiyo ripoti niliyoambatisha, nikielezea tu mshangao wangu kuhusu mtu aliyefanya kazi IMF kwa miaka 21 na mwenye makazi ya kudumu Marekani, nyumba nzuri na kipato kizuri, lakini anajiingiza katika dubious deals ambazo anafahamu wazi kuna siku zitasanuka! Kwa hakika sikutegemea hayo kwa mtu mwenye upeo huo wa elimu, kipato na uhakika wa maisha. Kwa hisia zangu nikadhani (speculate) kuwa kuna zaidi ya choyo binafsi, ingawa hii haitetei uhalifu wowote alioufanya, lakini nahisi kuna wenzie ambao walihitaji huo ufisadi kuliko yeye alivyouhitaji, na sasa wamemzidi, wamepata pa kufunikia yote yaliyotokea! Namaanisha pengine yeye hakuzihitaji pesa hizo, ila waliozihitaji ndio waliomsaliti, bila kujali ni makubaliano gani aliyofanya nao (ambayo yanaashiria ni makubaliano haramu, yangekuwa halali zisingekuwepo juhudi zote hizi za kufichaficha!) Yaani mambo yamefichwafichwa hadi yakaonekana kama ya kichawi!
 
Hajasalitiwa huyu!!! Kajisaliti mwenyewe. Yeye alidhani kusaidia watu kuiibia nchi atasalimika? Kama angetaka uhai wake basi angegoma kuwapa CCM hela. Sasa aliowapa WAMEMTANGULIZA!!!! licha ya kwamba na wao watafuata
 
Wanaosalitiwa wanakuwa hivyo? Ballali kajisaliti mwenyewe. Mshahara wa dola 25,000 kwa mwezi bado akaamua kujihusisha na ujambazi dhidi ya nchi na wananchi wake waliompa nafasi ya juu namna hiyo? Chunguza rais Bush anapata pesa ngapi? Au waziri mkuu wa UK anapata ngapi? Wote wanapata pesa kidogo kuliko alizokuwa anapata Ballali
hasa ukiondoa taxes.

Yeye angeweza siku yoyote kukataa kujihusisha na ujambazi na kurudi USA ambako angepokewa kama shujaa na kupewa nafasi zingine kwenye IMF au Worl Bank.

Ballali ni mwendelezo tu wa maprofesa na madaktari wetu ambao wamejaa unafiki na ujinga, elimu zao hazijawasaidia kabisa, badala ya kutumia elimu zao kulijenga taifa, wanatumia elimu hizo kulibomoa.

Ballali ataishia kuwa mjinga katika Watanzania wajinga, msomi mroho aliyezidiwa na tamaa, akaishia kuanguka na kufa kama kibaka.

Akina Chenge na mafisadi wengine sasa wanamcheka.
 
Jamani mimi naamini kabisa kuwa Bwana Balali hakufa kifo cha kawaida nafikiri serikali inatakiwa kuja clean mbele ya wananchi wake na kuwaeleza inachofahamu kuusiana na balali bila kuficha ukweli wowote.

Balali aliondolewa nchini kwa siri na wala hakuondoka mwenyewe bali aliondolewa kuficha kashifa iliyokuwa inainyemelea serikali ya CCM, wizi! wizi wa mamilioni ya watanzania na kupelekwa marekani ambako inasadkikiwa alikuwa anumwa, hili Dr. anaushaidi na alilitaja pale mwembe yanga kabla hata wananchi hatujajua kuwa kuna upotevu mkubwa wa pesa za serikali.

Hii habari ya kupewa sumu katika hafla moja huko dodoma haijawahi kukanushwa na serikali, na huyu mtu leo amekufa kifo cha kutatanisha Je serikali inausika vipi na kifo cha mtuhumiwa mkuu wa wizi ambao CCM inausishwa?

Kwanini serikali ilikataa kuwaeleza wananchi balali amelazwa hospitali gani ili watanzania walioko marekani waweze kuumuona na kuongea nae, serikali inaficha nini katika hili, kwanini haikuruhusu watu wajue amelazwa wapi?

Kifo kimechukua siku 4 kutangazwa nayo baada ya kuona watu wamenusa na kupata ukweli wakawa hawana jinsi zaidi ya kukubali ukweli, je serikali ilikuwa inaficha nini, kwanini haikutaka watanzania wasijue kuwa balali amekufa?

Je Balali alitaka kusema ndo maana walimuondoa Tanzania kwa siri na kumpeleka marekani na wakampa sumu ili afe na siri moyoni? Je serikali ilihusika vipi kuakikisha balali aongei na watanzania kwa gharama yeyote hile? Je katika hili serikali inaficha nini?

Je kama serikali inaficha kitu, inamaana inashirikiana na mafisadi katika kuiujumu nchi yetu?
 
Sikubaliani na hoja ya kuwa Balali alisalitiwa
Baada ya kupata memo toka kwa Mkapa na walafi wengineo ili washinde uchaguzi kwa kishindo ili pia watupe kishindo cha unmaskini, alikuwa na hiari ya kujiuzulu na kurudi Maryland akiwa mtu safi..kukubali kwake kutumiwa na mafisadi ili washinde uchaguzi ndio kosa ambalo hatajisafisha nalo hata akiwa kaburini..huihtaji kufanya makosa mengi ili kuonekana mchafu na ukachafuka. Ukikosa penalti moja, unakosa ubingwa na hutaitwa shujaa hata kama ulicheza dakika 90 kwa uangalifu..Akiwa msomi na mwenye sifa kemkem za utendaji, alipaswa ajue kuwa hizi memo ni penalty shoot out..I have to play mine well..basii..yeye kwetu anazikwa kama FISADI
 
Sikubaliani na hoja ya kuwa Balali alisalitiwa

Balali hajasalitiwa ila kasaliti elimu na wadhifa wake. tatizo alilokumbana nalo Balali si lake pekee bali ni kwa wengi wa viongozi wetu wateule. Hushindwa kuchagua kati ya kufanya kazi yake kitaalamu au kumfurahisha yule aliyemchagua iwe katika ngazi yeyote. Hii ndio dilemma kubwa kwani sijui huchangiwa na hofu gani, kwani ingelikuwa ni pesa/mshahara Gavana wa benki kuu usingetegemea ashindwe kusema hapana pale ambapo ndilo jibu mwafaka, na kukubali hata kuachia ngazi ili kulinda heshima ya cheo chake na yeye mwenyewe. Je ni tamaa ya kujilimbikizia mali? maana ni wachache ambao huridhika. Money begets more money and if uncontrolled greed. Jana nilikuwa nikisikilizamahojiano ya miljdair mmoja uingereza na BBC kuhusu kutafuta njenje. Alikiri kuwa huo ni kama ugonjwa kwanianaamini pesa alizonazo na anazoendelea kuzitafuta yeye binafsi hazihitaji. Pengine lingelikuwa swali zuri kama mhojaji angelimuuliza za nini basi.
Mtizamo wangu ni kuwa kusalitiwa kwa viongozi wetu hakuko bali wao husaliti hata ile trust kidogo ambayo umma huwapa. Je rais mstaafu mkapa alihitaji kufanya hayo aliyoyafanya pamaoja na marupurupu yote ambayo rais mstaafu anatakiwa kupewa? Je ni wasiwasi wasi wa maisha ya baadaye?
 
Last edited:
nasikia alianza kuumwa baada ya kuitwa dodoma last year...mmmh a case of polonium perhaps (source - radio mbao)
 
nasikia alianza kuumwa baada ya kuitwa dodoma last year...mmmh a case of polonium perhaps (source - radio mbao)



Jamaa ni mgonjwa siku nyingi tu na ameunga kwenye msururu uliomtangulia, na nyuma yake kuna msururu utakaomfuata pia.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom