Jay One
JF-Expert Member
- Nov 12, 2010
- 18,535
- 20,710
Leo mchana, Nape akihojiwa na BBC amesema, Mahakama ya Mafisadi iliyoahidiwa na Magufuli inakuja kweli na watu wajiandae kuburuzwa mahakamani.
Nape amesema mahakama hii itakuwepo na kazi yake ni kushughulikia kesi zinazohusu matumizi mabaya ya madaraka na rushwa.
Amesisitiza kuwa tumekuwa na kesi nyingi zinazochukua muda mrefu sana na ni hasara kwa nchi kwani nyingine hadi unamsimamisha Mkurugenzi.
Ametolea mfano huo wa kusimamisha wakurugenzi kuwa kesi inaweza kuchukua miaka kuisha muda wote huu unamlipa mshahara wale bila kufanya kazi akasema ni bora tukawa na mahakama hiyo ili kufanya kesi hizi ziishe haraka!
"Chukulia kesi kama za EPA, kesi kama za kina Mramba, kuna mkurungenzi kesi ilichukua miaka sita inaendeshwa tu!" alisema Nape.
Nape amesema hivi leo watuhumiwa wa Richmond ndio wengine wanataka kwenda Ikulu. Akaongeza kuwa Mahakama za kawaida zina urasimu mwingi sana na mtu akiwa na madaraka na pesa ndio kabisa!
Amemalizia kwa kusema kuwa Mahakama maalum ya Mafisadi ni muhimu na inakuja!
Nape amesema mahakama hii itakuwepo na kazi yake ni kushughulikia kesi zinazohusu matumizi mabaya ya madaraka na rushwa.
Amesisitiza kuwa tumekuwa na kesi nyingi zinazochukua muda mrefu sana na ni hasara kwa nchi kwani nyingine hadi unamsimamisha Mkurugenzi.
Ametolea mfano huo wa kusimamisha wakurugenzi kuwa kesi inaweza kuchukua miaka kuisha muda wote huu unamlipa mshahara wale bila kufanya kazi akasema ni bora tukawa na mahakama hiyo ili kufanya kesi hizi ziishe haraka!
"Chukulia kesi kama za EPA, kesi kama za kina Mramba, kuna mkurungenzi kesi ilichukua miaka sita inaendeshwa tu!" alisema Nape.
Nape amesema hivi leo watuhumiwa wa Richmond ndio wengine wanataka kwenda Ikulu. Akaongeza kuwa Mahakama za kawaida zina urasimu mwingi sana na mtu akiwa na madaraka na pesa ndio kabisa!
Amemalizia kwa kusema kuwa Mahakama maalum ya Mafisadi ni muhimu na inakuja!