acha uongo mkuu, kweli kuna graduate gani wa BE, CM, LMV, ARCHTECTURE, INTERIOR DESIGN, EE, GM ambae bado anakula ugali wa mama home!makampuni kibao yapo, serikalini nako uhitaji si haba
Ardhi hakuna shule ngumu kama jamaa alivotisha but kuna school kama tatu ni za motoooo hiyo ya BE ani SCEM na SURP(mipango miji) hizi zinaunafuu but kwingine kuna balaa
Hati miliki ya kimila inatolewa kwa ardhi za vijiji na hati miliki kuu hutolewa kwa maeneo ya mijini!!! Na hizi zinasimamiwa na sheria mbili tofauti!hati miliki za kimila zinatolewa na halmashauri za vijiji wakati za general land zinatolewa na kamishna wa ardhi!!
Hati miliki ni Certificate of right of occupancy hii ni legal instrument na proof ya umiliki wako wa intrest fulani katika ardhi!!wakati haki miliki ama Right of Occupancy ni umiliki (ownership na possesion) juu ya ardhi ambayo kwayo hati hutolewa. Ahsante
Kwa sheria ya zanzibar,Mtanganyika hana haki ya kumiliki ardhi kule. 2 issue ya building permit sio kazi ya watu wa ardhi pekee. Wasimamizi ni wahandisi na watu wa mipango miji,mtaalam wa ardhi anahusika kukagua umiliki tu
eneo linatakiwa liwe limepimwa na ramani yake ipate kibali cha Mkurugenzi wa Upimaji na Ramani! baada ya hapo Afisa ardhi atahitajika kufanya ukaguzi ili kujilizisha,then utatakiwa kulipia gharama zifuatazo fee for certificate 1600000,deed plan fee 6000,survey fee kama bado,land rent,stamp duty...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.