Pia kulikuwa na : Rombo Investment,Kamwanga Line, Loliondo Bus, Dar Express, Salama Star, Fresh ya Shamba,Osaka,Hood,Njuweni(Ya Mzee Mfinanga wa Kibaha), Imamu Express , Machame, Wakongwe wengine wataongeza.
Wakuu Mrangi na johnthebaptist, mnakumbuka Gari za Kiswele malori na mabasi yote namba zake za usajiri zilikuwa zinaishia na 89? Yaani kama hivi TZ 1089, TZ 2189.
Sijui ndiyo masharti ya Wataalamu!?
Nilipanda kimeo ,kutoka Kisutu kuelekea Arusha , kampuni ya mabasi ya Imamu .
Ile Safari sitahisau, tumeondoka Kisutu saa kumi na moja jioni tumefika Arusha kesho yake saa nne na nusu Asubuhi!.
Sharuks : Abbas Gulamali Mhindi wa Ifakara .
Dar Oyee : Gulam Somji Mhindi wa Mahenge.
Halafu kulikuwa na Ulanga Express , mali ya Ushirika wa vijiji vya Tarafa ya Malinyi.
Walikua Pamoja katika harakati.Wakati Maalim Seif Waziri Kiongozi Zanzibar , Shaaban H Mloo alikuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
Na walitimuliwa wote CCM baada ya ile hali mbaya ya kisiasa kule Zanzibar.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.