Ulisemalo ni sahihi kabisa kwamba dawa ya matatitzo ya nchi yetu, wakati huu, ni wananchi sote kuamka na kuwa na ujasiri wa kudai haki ya kuwa na katiba sahihi ambayo, kwanza, itatambua Serikali tatu za Mungano (Serikali ya Muunga o, Serikali ya Tanganyika, na Serikali Zanzibar). Lakini wzkati...
Ni shuhuda au ni kibaraka? Madawa hayo kwa nini hayakuweza kutolewa huko Ngorongoro mpaka yasubiri watu walazimishwe kuhamia Msowera? Huo siyo msaada bali ni hongo kufunika ukatili wa serikali hii inayojiita ya 'awamu ya sita' inaofanyia wananchi wa Ngorongoro. Hivi leo wakisema watu wahamishwe...
MADAI YA KATIBA MPYA YANATOKANA NA UKWELI KWAMBA KATIBA ILIYOPO IMEKIUKWA NA WAKATI KWA SABABU INAZUNGUMZIA MUUNGANO, WAKATI MUUNGANO ULIVUNJIKA ZANZIBAR ILIPOAMUA JUWA NA SERIKALI YAKE NJE YA MUUNGANO. KATIBA MPYA NI LAZIMA ILI KUIPA TANGANYIKA SERIKALI YAKE PIA AU KUVUNJA SERIKALI YA ZANZIBAR...
KAULI ZA NAPE ZINATOKANA NA ANDIKO LIPI LA CHAMA CHA MAPINDUZI? ANDIKO MOJA LA CHAMA LINASEMA "NITASEMA KWELI DAIMA, FITINA KWANGU MWIKO". JE, KAULI YA NAPE KWAMBA CHAMA KINA WENYEWE NI YA KWELI? JE, KAULI YA NAPE KWAMBA MWENYEKITI ALIYEFARIKI ALIKUWA GODFADHA KWA BAADHI YA WANACHAMA NI YA...
Ni sahihi kabisa starehe nyingi zinasemekana kuwa ni dhambi. Hiyo inatokana na ukweli kwamba starehe nyingi huwaelekeza wanaostarege kutenda dhambi. Sasa, kabla hatujaangalia ni kwa vipi starehe inaongoza watu kutenda dhambi, tujiulize, dhambi ni nini? Dhambi ni uasi wa sheria ya Mungu. Starehe...
It can be true that generally the tests are working well, but how far sure is the learned CDC Director that the tests in Tanzania, in particular, are working well? Scientist never give blind responses. What scientific steps has the honourable Director taken to disapprove the Tanzania...
Nimeanza kufuatilia Mada kuhusu vicoba hivi karibuni. Nimebaini mijadala kuhusu mada hii kuhusu uanzishaji na uendeshaji wa vicoba imeishia 2017. Naweza kupata mdau wa kunisaidia kupata literature kuhusu kuanzisha na kuendesha kikundi cha vicoba? Nikipata contact ya mtaalam anayeweza kunisaidia...
Siamini kama kweli barua ya Msajili wa Vyama vya Kijamii ni 'fake'. Kama ingekuwa batili isingekuwa imenukuu vifungu vya SHERIA husika, wala isingesainiwa na Afisa mhusika wa Kitengo husika. Bora Waziri aeleze kama zipo sababu zingine zilizompelekea kusimamisha zoezi hilo.
Nakubali kulikuwa na makosa mengi ya uchapaji (typing errors), lakini hilo halifanyi nisielewe ninachokizungumzia.
Kwa ufupi nilichokimaanisha ni kwamba viongozi wetu wa kiroho (hasa wa Makanisa ya Kiprotestanti) wana wajibu wa kutoa ufafanuzi wa kina kwetu sisi waumini wao kuhusu Mkataba wa...
Kiongozi wetu wa KKKT wananishangaza sana; maana badala ya kushughulikia changamoto za kiimani zilizo katika Kanisa wanaloliongoza wanadandia hoja za utawala wa ulimwengu huu. Yesu katika Kitabu cha Injili ya Yohana 15:19 aliwaonya wanafunzi wake (na wale wote wanaodai kuwa ni wafuasi wake (kama...
Kwani hao wapinzani wangeshiriki majadiliano ya Bunge bila kuonekana au kusikika katika vyombo vya habari wangenyang'anywa ubunge? Au kwa maneno mengine, hao wapinzani waliomba Ubunge kuwakilisha wananchi kuonyesha sura katika luninga, ama kuwasilisha hoja za kutetea maslahi ya maendeleo ya Taifa?
Kama upinzani walijuwa kuwa CCM wakibaki peke yao watawapandishia kodi "wananchi", kwa nini walisusa vikao pasipo kufukuzwa!? Iliwapasa waelewe kwamba mtu hawezi kumuua nyoka aliye ndani ya nyumba kwa kusimama nje ya nyumba hiyo. Wala haiwezekani mtu akashinda hoja ya kujadiliana kwa kuziba...
Hongera Mheshimiwa Rais, Dr. Shein, kwa uamuzi wa kuwateua wapinzani kuingia katika Baraza la Wawakilishi. Sasa ninashauri busara itumike kuteuwa mmoja wao ashike nafasi ya Makamu wa Kwanza wa Rais. Hatua hiyo itasaidia kuzima uongo na ghiliba za Seif. Wengi tunafahamu kwa uongo na unafiki wake...
Chanzo kikuu cha mzozo katika siasa za Tanzania Visiwani ni Seif. Huyu ndiye anayewadanganya na kuwatumia Wananchi, hasa wa Pemba, kutimiza malengo ya maslahi yake binafsi na wale wanaomtuma na kumfadhiri. Ķutokuteuwa Makamu wa Kwanza wa Rais (kutoka upinzani) ni kumpa nafasi Seif kuendelea...
Ni kweli katika uchaguzi wa marudio uliyofanyika tarehe 20 Machi 2016 hakuna Chama cha upinzani kilichokidhi vigezo vya kuingia katika ushirikiano na CCM kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa kikatiba. Lakini kwa sababu ya utete wa hali ya kisiasa ilivyo hapo Visiwani; mimi nadhani ingekuwa jambo...
Hongera sana, Rais JPM. Hii ni uthibitisho kwamba nchi yetu ni tajiri, ila tatizo ni mipango ya matumizi pamoja na ubinafsi wa kifisadi. Kwa mwendo huu, hao mabeberu wa kikoloni, Wamarekani na MCC yao, hawawezi kututisha. Rais wetu kaza uzi nasi wananchi tunaotaka uhuru wa kweli tuko nyuma yako...
Mimi nadhani watu wengine vichwa vyao vimejazwa maji badala ya akili. Hivi kweli mtu kutamka ati Rais alipwe mshahara wa laki nane una akili timamu!? Hivi wewe ungekuwa ndiyo Rais ungethubutu hata kuwazia tu kujilipa shs milioni tano, achia mbali kuota kupunguza hiyo milioni tisa!!! Sasa hayo...
Hayo ni maoni yako. Kumbuka bandari zetu hazihudumii Watanzania peke yao bali na mataifa mengine pia. Ufisadi ukitokomezwa bandarini mataifa yanayohitaji huduma ya bandari yatahamasika kuongeza ujazo (volume) wa kupitisha mizigo zaidi katika bandari yetu na hivyo mapato yataongezeka zaidi. Vile...
Ndugu Lambard hayo mawazo uliyonayo ya kudhani nchi hii itaendelea kwa kutegemea kutembeza bakuli la kuomba misaada ni ndoto za mchana (jinamizi). Ili tuweze kuendelea Watanzania wote kwa pamoja tunatakiwa tujitoe kwa moyo mmoja, bila unafiki, kuunga mkono juhudi za Rais JPM za kupambana na...
Kwa wale wote wanaopenda kuona nchi inaendeshwa kwa uhuru wa kweli, hatua hii ya MCC si ya kushangaza. Hiyo ndiyo hali halisi ya uhuru wa bendera, wakubwa (wakoloni mabeberu) kuamrisha (dictate) matakwa yao kwa viongozi vibaraka. Kutokana na hili imetupasa Watanzania wote tusimame imara kumuunga...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.