Una mpango gani na uzao wako wa nje ndoa?

Una mpango gani na uzao wako wa nje ndoa?

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
40,460
Reaction score
62,846
Kila mchepuko umetokea kutamani kuzaa na mimi

Hii imepelekea kukaribia kuwa na watoto 20, wengine wanahudumiwa na mama zao na mimi pia kuwapa ushirikiano kwa vitu vidogo vidogo ili maisha yaweze kusogea.

Sijajua, kwa nini wote wamekuwa na mwitikio huo, au labda watakuwa wamependa mbegu, kwa sababu ata kwenye mifugo na huko mashambani huwa tunachangua mbegu nzuri na kuziotesha ili zitupatie mazao yaliyo bora.

Hivi sasa, wapo wengine wawili ambapo tunategemea hapo mwakani kwenye mwezi wa kwanza na wa pili watuletee wapiga kura wawili.

Sijajua ni kwa nini wanapenda uzao wangu.

Na wazazi wenzangu wote ni pisi kali, waswahili wanaita visu.

Natamani katika uzee wangu, niishi na hao wote niliowaleta duniani; yaani nitengeneze ‘Empire’.

Hapa natafuta kijiji chenye hali ya hewa nzuri, nichukue kama ekari 10, nipige uzio na humo ndani tuburudike na uzao wangu kwa kufuga na kulima vibustani vya hapa na pale.

Muhimu tu,nizeeke vizuri na vijana wangu.

Je, wewe una mpango gani na uzao wako wa nje ya ndoa?​
 
Hii imepelekea kukaribia kuwa na watoto 20,
Wazee wa zaman walikuwa na Rasilimali nying na ndio maana wameoa wake weng na kupata watoto wengi.

ulitakiwa uwe na hizo ekar 10 kwanza na sehem nzur kama unavyotamani alaf ndio uzae hao watoto.
Otherwise umeongeza idad ya single mothers na watoto wanaokosa malezi na huduma wanazostahili.
 
Hakunaga kitu inaitwa "Kizazi cha Nje".

Mwanaume ukipata mtoto mahali popote, nenda kamlipie ili umkomboe aje kwenye himaya yako.

Haya mambo ya kuiga uzungu mwingi ni upuuzi unaofanya watoto wanakosa malezi ya familia za baba zao.
 
Wazee wa zaman walikuwa na Rasilimali nying na ndio maana wameoa wake weng na kupata watoto wengi.

ulitakiwa uwe na hizo ekar 10 kwanza na sehem nzur kama unavyotamani alaf ndio uzae hao watoto.
Otherwise umeongeza idad ya single mothers na watoto wanaokosa malezi na huduma wanazostahili.
Uko sahihi, kuna baadhi ya vijiji ekari moja unapata kwa elfu70 tu, ingawa mazingira ya hivyo vijiji hayajanishawishi.
 
Hakunaga kitu inaitwa "Kizazi cha Nje".

Mwanaume ukipata mtoto mahali popote, nenda kamlipie ili umkomboe aje kwenye himaya yako.

Haya mambo ya kuiga uzungu mwingi ni upuuzi unaofanya watoto wanakosa malezi ya familia za baba zao.
Unaweza ukaleta watoto na wasikuhurumie huko uzeeni; muhimu ni kila kitu kufanya kwa kiasi.
 
Unaweza ukaleta watoto na wasikuhurumie huko uzeeni; muhimu ni kila kitu kufanya kwa kiasi.
Sasa mkuu mzazi unatafuta huruma ya nn kwa watoto?

Wewe walee ktk malezi bora waje wawe watu bora maishani mwao.

Mengine muachie Mungu.

Na utake usitake watoto wote hawatakaa wafanane, kuna watakaofanikiwa na kuna ambao hawatafanikiwa.
 
Sasa mkuu mzazi unatafuta huruma ya nn kwa watoto?

Wewe walee ktk malezi bora waje wawe watu bora maishani mwao.

Mengine muachie Mungu.

Na utake usitake watoto wote hawatakaa wafanane, kuna watakaofanikiwa na kuna ambao hawatafanikiwa.
Uzee unaitaji faraja kutoka kwa uzao wako, kama uzao wako hautakufariji ata kwa maneno mazuri, utahisi dunia ni jehanamu
 
Uzee unaitaji faraja kutoka kwa uzao wako, kama uzao wako hautakufariji ata kwa maneno mazuri, utahisi dunia ni jehanamu
Kwenye haya maisha ya sasa tena ya nyakati hizi, jifunze kuwa your own source of happiness.

Hawa Gen Alpha hawatakuwa kama sisi Millenials ambao tunawahudumia wazazi wetu.

Kufika 2050 jua kutakuwa na centre za kulele wazee na vikongwe kama huko Ulaya na Marekani.

Vijana watakuwa busy kukimbizana na maisha.
 
Kwenye haya maisha ya sasa tena ya nyakati hizi, jifunze kuwa your own source of happiness.

Hawa Gen Alpha hawatakuwa kama sisi Millenials ambao tunawahudumia wazazi wetu.

Kufika 2050 jua kutakuwa na centre za kulele wazee na vikongwe kama huko Ulaya na Marekani.

Vijana watakuwa busy kukimbizana na maisha.
Ndio maana nataka niwatafutie pori, watakao oa au kuolewa wakae ndani ya hiyo pori (empire). Muhimu nikigeuka kulia na kushoto,nione uzao wangu.
 
Back
Top Bottom