Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,842
- 31,075
Kama nilivyoeleza kwenye heading yangu, leo ni siku ya 12 watu waliotaka kupora maisha ya Tundu Lissu hawajafanikiwa kukamatwa....
Hakika huu ni muujiza mkubwa ambao tunatakiwa watanzania wote tuurejeshe utukufu kwa Mungu aliyetuumba ambaye ndiye anayetupangia pia siku zetu za kuishi hapa duniani.
Nirudi kwenye mada yangu ya kuwa leo ni siku ya 12 hakuna dalili yoyote ya kumkamata yule "jambazi" aliyemminia risasi zaidi ya 32 Tundu Lissu mchana kweupe tena ndani ya makazi ya "wakubwa" ambapo pia kuna walinzi getini!
Kama mimi ningekuwa IGP Sirro au kama mimi ningekuwa RPC was Mkoa wa Dodoma au kama mimi ningelikuwa Waziri wa mambo ya ndani Mwigilu Nchemba, ningekuwa nimeshatuma barua yangu ya kujiuzulu......
Kwa kuwa nisingekubali aibu hii iendelee kuniangukia mimi kwa uzembe uliokithiri wa kutowakamata waliohusika na mkasa huo!
Kama ningelikuwa mimi ningepeleka "faster" barua hiyo ya kujiuzulu kwa kuwa najua wajibu Na. 1 wa kazi yangu ni kulinda RAIA na MALI zao.
Yule dereva wa Lissu amewarahisishia ile kazi yenu ya kumtafuta "mbaya" wa Lissu kwa kuwatajia namba ya gari iliyokuwa "ikiwatail" kutoka Dar ambayo ni gari no. T932AKN
Sasa ni kitu gani ambacho nyinyi Polisi wetu mnataka Raia wawafanyie???
Kama mimi ningelikuwa Polisi ningeenda TCRA na kutaka taarifa za mawasiliano za huyo mtu/watu waliokuwa wakiemdesha gari hiyo mamba T932AKN, mchezo ungekuwa umekwisha!
Kutokufanya hivyo maana yake ni kuwa waliofanya ukatili huo mkubwa ni "wao" wenyewe na hivyo kusababisha IGP Sirro, RPC wa Dodoma na Waziri Mwigulu Nchemba wachukue dhamana ya kujiuzulu Mara moja bila kuchelewa.
Imenenwa na wahenga MWISHO WA UBAYA AIBU!
Mungu ibariki Tanzania
Hakika huu ni muujiza mkubwa ambao tunatakiwa watanzania wote tuurejeshe utukufu kwa Mungu aliyetuumba ambaye ndiye anayetupangia pia siku zetu za kuishi hapa duniani.
Nirudi kwenye mada yangu ya kuwa leo ni siku ya 12 hakuna dalili yoyote ya kumkamata yule "jambazi" aliyemminia risasi zaidi ya 32 Tundu Lissu mchana kweupe tena ndani ya makazi ya "wakubwa" ambapo pia kuna walinzi getini!
Kama mimi ningekuwa IGP Sirro au kama mimi ningekuwa RPC was Mkoa wa Dodoma au kama mimi ningelikuwa Waziri wa mambo ya ndani Mwigilu Nchemba, ningekuwa nimeshatuma barua yangu ya kujiuzulu......
Kwa kuwa nisingekubali aibu hii iendelee kuniangukia mimi kwa uzembe uliokithiri wa kutowakamata waliohusika na mkasa huo!
Kama ningelikuwa mimi ningepeleka "faster" barua hiyo ya kujiuzulu kwa kuwa najua wajibu Na. 1 wa kazi yangu ni kulinda RAIA na MALI zao.
Yule dereva wa Lissu amewarahisishia ile kazi yenu ya kumtafuta "mbaya" wa Lissu kwa kuwatajia namba ya gari iliyokuwa "ikiwatail" kutoka Dar ambayo ni gari no. T932AKN
Sasa ni kitu gani ambacho nyinyi Polisi wetu mnataka Raia wawafanyie???
Kama mimi ningelikuwa Polisi ningeenda TCRA na kutaka taarifa za mawasiliano za huyo mtu/watu waliokuwa wakiemdesha gari hiyo mamba T932AKN, mchezo ungekuwa umekwisha!
Kutokufanya hivyo maana yake ni kuwa waliofanya ukatili huo mkubwa ni "wao" wenyewe na hivyo kusababisha IGP Sirro, RPC wa Dodoma na Waziri Mwigulu Nchemba wachukue dhamana ya kujiuzulu Mara moja bila kuchelewa.
Imenenwa na wahenga MWISHO WA UBAYA AIBU!
Mungu ibariki Tanzania