Shida ninauoiona ni watanzania kuongea sana lakini ukifika wakati wa uchaguzi hauwaoni wakipiga kura. Hii ni changamoto. Tubadilike. Maneno hayawezi kubadili chochote
Alikuwa anaruka ruka, hoja zenye utata na zilizotengenezwa kwa maslahi yao mapana huwa hawazigusi hata kidogo. Utasikia tumepokea maoni yako tunayafanyia kazi
Jambo hili litavaliwa njuga na kutafutiwa ufumbuzi ambao bila shaka itakuwa wastaafu kukatwa kwenye pensheni yao. Lakini wastaafu wakubwa wa taifa hili kulipwa mishara na wenza wao sio ishu. Mungu atusaidie sisi watanzania na lichama letu tawala lisilo na huruma
Labda waamuke siku hiyo wakiwa wamechanganyikiwa na hawajielewi. Lakini wakiwa na akili timamu hawawezi kudiriki hata kuwaza hivyo. Ni sawa na kujitia kisu kooni
Mfumo wa Elimu unaweka mazingira butu kwa vijana kujihusisha na siasa au uongozi wa nchi yao. Elimu ya uraia sio muhimu katika shule na vyuo. Hivyo tusitarajie kuona mwamko mkubwa katika siasa kutoka kwa vijana. Mungu atusaidie
Hawa jamaa bila kuiba kura hawatoboi , na hawajawahi kutoboa. Wenyewe wanajua kabisa bila kuiba hawawezi kushinda. Tuna safari ndefu sana ili kufikia kwenye lengo la haki
Kwa vyovyote vile, kuwepo kwa upinzani nchini ni muhimu sana kwa mustakabali wa taifa. Kuna namna ambayo sisi kama taifa tukiondoa itikadi zetu tunaona tofauti kati ya wakati upinzani ulipokuwa na nguvu (2015 -2020) na hali ilivyo sasa. Ule uwezo wa kuisimamia serikali imedorora sana. Hivyo wale...
Nenda kwa mchungaji alieokoka akuombee. Unasumbuliwa na jini wa kike kama wewe ni mwanaume, au jini wa kiume kama wewe ni mwanamke. Majini hao wanatabia ya kushirikiana na watu wakiwa ndoto ni. Damu ya Yesu na maombi inamaliza hilo tatizo
Hii nchi kila kitu ni siasa, kama wanasiasa walisema upungufu wa umeme utaisha mara baada ya kuwasha kinu namba 9, na kimeshawashwa na bado mgao upo, lazima tuanze kuamini kuwa yamkini tumepigwa. Kauli ya awali ilikuwa ya kisiasa na matokeo yake yatakuwa ya KISIASA. MUNGU Isaidie nchi yangu Tanzania
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.