Boda na Bajaji vinaingia mjini kwa sababu hatuna usafiri mwingine wa kueleweka wa umma, vinginevyo wangekuwa wa kufanya delivery na kubeba mizigo tu ila sio abiria.
Tatizo kubwa zaidi sio hata uwepo wake bali utaratibu. Wamachinga wawepo ila wasifanye biashara barabarani sehemu za watu kupita, wasiweke vispika vyao vya kelele na pia wasisumbue wapita njia. Boda ndio wendawazimu kabisa, yani wanapita popote bila utaratibu, wanagonga watu, wanagongwa na...
Ukiwa na akili lazima ujiulize kwa nini watu wanapinga matokeo katika chaguzi zote nchini kwako na kwa nini sehemu nyingine duniani watu hawapingi matokeo.
Watu wenye mawazo kama yako ambao ndio wengi CCM pia huwa mnafikiri uchaguzi ni tukio la siku moja tu la kupiga kura. Huko US hata shughuli...
Namaanisha watu ambao ni kama wanachama base wa CHADEMA. Unaweza kuwa unafikiria kila mtu anayeongea lugha ya CHADEMA kwa sasa ni mwanaCHADEMA jambo ambalo sio sahihi. Kuna watu wengi wanazungumza lugha moja na CHADEMA kwa sasa kwa sababu wamechoshwa na CCM na Samia, siku CCM ikiondoshwa...
Kitu kikubwa kuhusu Nyerere nafikiri ni legacy ya kuunda taifa moja stable kutoka makabila zaidi ya mia pamoja na dini kubwa mbili tofauti na nchi nyingi za Africa, uhuru wetu kama Tanganyika ilikuwa tuupate kirahisi tu. Mataifa kama Angola, Zimbabwe na Africa Kusini uhuru wao ndio ulikuwa mgumu...
Ni propaganda zilizotengenezwa na watawala wengi weusi na wa nchi za Africa na vikundi vya kudai uhuru vya hapa na pale ili ku legitimize powers zao katika nchi wakoloni walizoziachia. Ni kama vile ambavyo huwa unamsikia Nape anasema aliipambania sana CCM mwaka 2015 hadi akatenguka mikono.
Labda huelewei maana ya uchumi jumuishi. Umachinga barabarani, kazi za Bajaji na bodaboda haziwezi kuleta uchumi jumuishi hata ukiziruhusu hadi ndani ya Ikulu. Uchumi jumuishi unaletwa kwa kazi, ajira au biashara za staha "decent jobs".
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.