J
Jamani nashukuru kwa michango yenu.Lakini hili ni tatizo limenisumbua muda mrefu na msichukulie kiwepesi.Nitaridhika roho yangu iwapo nitajibiwa kwa dalili aitha za biblia au quran.Mimi sijisemeshi mwenyewe bali sauti hii huniteka nyara na kuongea.Yaani ina ni override.
Wakati ikiongea hunitumia mimi mwenyewe kwa hivyo huwa kama ni mimi.Naweza fikiria jambo akalijibu aitha ndani kwa ndani au kwa mdomo wangu mwenyewe.Ajabu siwezi kujadiliana naye.kamwe hanijibu,lakini anajibu wazo langu.
Wala si ugonjwa.mimi ni mzima na mtu hawezi kujua yanayo nifanyikia mpaka nimweleze.Huyu anaeongea huchukua kama nafasi ya Mungu.Huniambia maneno ya kuniliwaza na kunipa matumaini.Naogopa asije kuwa ibilisi anipoteze.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.