Kudai Tume Huru ya Uchaguzi ni lazima iwe ndio ajenda kuu ya upinzani/washindani kwani 2020 haipo mbali vinginevyo aliyepo Magogoni ataendelea kututawala hadi 2025 (Tanzania twafa)
Uonevu katika kesi ya Lema ni wa kutisha. Kumnyima mtu dhamana kwa kesi ambayo inadhaminika ni ukiukaji wa hali ya juu wa haki za binadamu. Huyo Mkuu wa Mkoa wa Arusha na Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Serikali ni lazima wawajibike hata na huyo anayewatuma wafanye uovu huo. Ni lazima wawajibike na...
Uwezo wake ni kawaida ila wale wenye uwezo mdogo wa kisheria wana muona ni kipanga. Alitumiwa sana na Asha Rose Migiro wakati wa Bunge la Katiba kuandika Rasimu Chakachuzi ya Chenge ambayo mwisho wa siku haikupita. Yeye ni mtu wa kutumiwa kutekeleza matakwa ya wakubwa. Hivyo kuweni macho naye.
Gubu ndilo linalokusumbua. Kiongozi kujua matatizo ya wananchi na kupanda daladala nao ni kosa tangu lini? Inaelekea matusi ya Jangwani yamekuharibu. CCM poleni sana na mtalia kila kitendo wafanyacho Ukawa.
Nimepita pale Jangwani wingi wa watu waliohudhuria ni mdogo sana haufikii hata 10% ya watu waliomlaki Lowasa Mbeya au Zanzibar. Hii inamaanisha mvuto wa CCM umekwisha na kama ni nguo ina viraka vinavyoonyesha maungo yote. Na kama ni mpauko basi imepauka kiwango cha kutia kinyaa. Pole sana...
Ninasisisitiza CCM wameandaa wizi mkubwa wa kura. Dar es Salaam kura zitabatilishwa kama mwaka 1995. Tume ya Uchaguzi itatangaza matokeo kama alivyofanya Kivuitu na huo ndio ushindi wa kisayansi alioahidi Magufuli. Ni vema UKAWA na wote wanaoitakia mema nchi hii kupambana na njama hizo ovu za...
Imeamuriwa kuwa Jeshi na Polisi watumiwe kuiba kura ikiwa ni pamoja ya kujaza kura katika masanduku ya kura bandia ambayo ndiyo yatachukuliwa kwenda kuhesabiwa kana kwamba yametoka katika vituo vya kura. Ili kutekeleza mpango huu haramu, unaoendana na majigambo ya Kikwete eti "maarifa tunayo na...
Kikwete kasema "maarifa wanayo" na lazima watashinda. Huu ni moja ya uthibitisho wa "maarifa" waliyonayo. Nenda Lipumba kamsaidie Kikwete kutekeleza wizi wa kura.
Anachomaanisha Kikwete ni kuwa CCM itaiba kura kwa namna yoyote ile ikiwa ni pamoja na kuitumia Tume ya Uchaguzi kumtangaza Magufuli kuwa ni mshindi kama ilivyofanywa na ile ya Kenya ilimpotangaza Kibaki kuwa ni mshindi mwaka 2007/2008. Ni lazima UKAWA kuwa makini na njama zote za wizi wa kura...
Imekula vipi kwa Tibaijuka wakati kawagaragaza wale mahasidi waliotumwa kugombea kutekeleza mradi wa wale waliokwapua pesa za Escrow na kugawiana kwenye lumbesa kutoka benki ya Stanbic?
Sina lengo zaidi ya kutetea ukweli akifanya vibaya nitamsema ila katu kamwe sitakubali uongo unageuzwa kuwa ukweli na ukweli unageuzwa kuwa uongo. Kikwete ndiye aliyetoa amri fedha za escrow zitolewe "kama alivyoshauri Mwanasheria Mkuu". Leo hii anakuwa na ujasiri wa kuwaambia Watanzania eti...
Kazi nzuri sana Mama Tibaijuka licha ya usaliti uliofanyiwa na wale wanokuogopa kwa uwezo wako na ambao wamewekeza kukuchafua wewe tumikia wapiga kura (wachaguzi) wako na mwisho wa siku ukweli utajulikana.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.