Mikopo hii, ni tofauti na mikopo mingine kutoka kwenye mabenki ya kibiashara kwani haihitaji Dhamana, kitu ambacho kimekuwa kikiwakwamisha vijana wengi wanaotaka kuanzisha miradi mipya.
Ndugu wanajamvi,
Kwa wale wanaopenda kufuatilia shughuli za Bungeni watakuwa wameshamsikia Mh. Waziri Gaudensia Kabaka akitangaza juu ya jitihada za Serikali kuzalisha ajira laki sita, hususani kupitia miradi ya vijana ambao watapatiwa mikopo ili kukidhi mahitaji ya miradi yao. Jambo hili pia...
Mdau
Hiyo asilimia 17 au 18 uliyoambiwa ni riba kwa kipindi cha mwaka mmoja (miezi kumi na mbili). Kiasi kamili utakacholipa kama riba ya mkopo wako kitategemea muda wa mkataba wako wa mkopo. Ukikokotoa hiyo riba ya 17% ili ujue riba kwa mwezi ni kiasi gani, utapata 1.42%.
Hiyo riba ya 1.42%...
Ni suala jema sana kuhamasisha matumizi ya bidhaa zinazozalishwa na Watanzania ili kuwaunga mkono na kukuza Uchumi wa nchi. Lakini ni suala jema zaidi kuhamasisha ubora wa bidhaa hizo ili ziweze kukidhi mahitaji ya walaji na Soko, kwani kwa kufanya hivyo zitaweza kushindana na bidhaa nyingine...
Tafadhali, tembelea link hii ili ujifunze namna Mdau mwenzio alivyofanikiwa kwa kutumia njia hii ya Crowd Funding
Investor turns to online crowd for expansion funds - Magazines - businessdailyafrica.com
Mdau
Zingatia sana ushauri wa Nyabaheta na Lyamber kwani ni wadau wengi wanafikia malengo yao kwa njia hizo.
Lakini sisi kwa leo tungependa kuzungumzia hii dhana ya CROWD FUNDING. Japo inaonekana kama dhana mpya kwa hapa Tanzania, lakini inafanya kazi.
Je Crowd Funding ni nini? (Tafadhali rejea...
Mdau form hizi hupatikana katika tovuti ya BRELA, www.brela-tz.org
Form yenyewe unayoihitaji wewe ni hii hapa STATEMENT OF PARTICULARS IN THE CASE OF A FIRM
Kila la heri
Mdau
Michango yako inaheshimika sana hapa jamvini.
Sisi kama SEN hatuna ufungamanisho na Pension Scheme yoyote, wala hatuna mamlaka ya kupokea fedha kama akiba kutoka kwa mtu yeyote, (hata kutoka kwa mwanachama wetu).
Tunachokifanya hapa ni kuchokoza mada tu, kwani kwa uzoefu wetu, tumekutana...
Mdau,
Muungwana huwa anahoji pale asipokuwa na uhakika na taarifa ili asije akapotoka au akapotosha watu wengine kwa kutoa hitimisho lisilo sahihi. Sisii kama SEN tunaamin unakidhi vigezo vyote vya uungwana, lakin katika hili tuna haki ya kudhani kuwa umepotoka kidogo.
Ndugu, maudhui ya mjadala...
Uzoefu wetu unaonyesha kuwa wajasiriamali wengi waliokuwa na biashara ndogo ndogo walizokuwa wakiziendesha wenyewe (owner operated business) wanaishi maisha ya kubahatisha sana baada ya kushindwa kujishughulisha na shughuli za uzalishaji mali kutokana na uzee au hali zao za kiafya
Je ni nani...
Wanabodi,
Kwa kuwa wengi wetu tulidhubutu/tumedhubutu kuitathmini dhana hii ya ujasiriamali sambamba na kujitathmini binafsi juu ya njia sahihi zaidi za kufikia mafanikio ya kweli maishani. Tathmini ambayo ilitupelekea/imetupelekea, kudhubutu kufanya maamuzi sahihi ya kujiajiri wenyewe iwe ni...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.