Ni kweli amesema ni tshs 2000 kwa change rate hiyo ya 104 huo mtungi utakuwa cuban peso kama 19 plus hongera zao sisi bei ya nishati haikamatiki yawe mafuta uwe umeme iwe gesi ni balaa
Hata kama wangeshiriki si rahisi kushinda kwa sheria za tume huru ya uchaguzi ya mwaka 2024.Ukiwa wakala katika kituo cha kura huruhusiwi hata kuwa na simu ya kumjulisha mgombea wako kiasi alichopata.Nakala ya matokeo utapewa iwapo tu kutakuwa na nakala za kutosha.Inachekesha sana
Kinachokosekana ni utashi wa kufanya hivyo kutoka kwa watawala wakiamua hata leo wanaweza wakabadili vipengele vinavyolalamikiwa kwenye sheria ya uchaguzi ila hawataki wanaona watahatarisha vyeo vyao
Sioni namna yoyote ya kuzuia vuguvugu la madai sheria bora za uchaguzi kwa muda mfupi ambao chadema wamefanya operation yao ya madai ya sheria zisizopendelea chama kimojawapo watu wengi wameanza kuelewa na kuushangaa uhuni wa kuteua wasimamizi unaofanywa na mshindani mmojawapo ambao umefanyika...
Itakuwa ni kosa kubwa sana iwapo chadema itaamua kushiriki uchaguzi huu kwani hawawezi ambulia chochote zaidi ya kuja kutambishiwa na masisiyemu kwamba tumeshinda kwa kishindo.Waacheni na uchaguzi wao na tuvyama rafiki twa ccm mtakuwa mmefikisha ujumbe kwamba kuna uonevu chaguzi za Tanzania
Raia watakaojitokeza kulinda kura zao huoni watakuwa kwenye hatari ya kudhuriwa na vyombo vya dola pamoja na green guard kama tulivyowahi shuhudia chaguzi za huko nyuma !
Ni heri tuendelee kuchangia chama kwa njia ya tone tone kuliko kushiriki kwenye uchaguzi ambao umesheheni hatari luluki za kuuliwa kwa wagombea na wafuasi wa chadema na kutoheshimiwa kwa matokeo kwenye sanduku la kura.Ili mpinzani atangazwe lazima watu wapigwe risasi watu wafungwe au kuwe na...
Kwa miaka mingi chadema wamenangwa na masisiyemu kwamba hawawezi kuacha kushiriki uchaguzi mkuu kwa mazingira yoyote kwa kuhofia kukosa ruzuku mwaka huu wamewaproove wrong
Madai ya mabadiliko ya sheria za uchaguzi yametolewa kwa miaka mingi lakini ccm imeyadharau au kufanya marekebisho ya kimagumashi mfano sheria ya sasa kuna kipengele kinasema watu wanaoshughulikia uchaguzi hairuhusiwi kuwashtaki ikiwa kuna kosa watalifanya wakati wa mchakato wa uchaguzi.Hapo...
Hivi hiyo kura ya hapana wakala wake atakuwa nani ?Acheni ghiliba kwa kuweka sheria zinazolenga kukinufaisha chama cha mapinduzi huku vingine vikiwekewa mazingira magumu ya kushinda
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.