Recent content by Parabolic

  1. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Katambi ana mamlaka gani kusamehe wasanii? Waliotenda makosa hayo na kufungwa jela watasamehewa na nani?

    Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, amekutana na wasanii na watengeneza maudhui 21 aliowaita katika kikao maalumu, akisema wamepewa msamaha wa makosa yao ya awali ya jinai yaliyohusishwa na matumizi ya mitandao ya kijamii. Soma pia: Wasanii walioitwa na Katambi leo wamesamehewa...
  2. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Mwenyekiti wa CCM Shinyanga ataja sababu ya Dk Nchimbi kufukuzwa CCM

    Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Shinyanga, Mabala Mlolwa amesema kitendo cha aliyekuwa Makamu wa Rais Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi kuwataka Watanzania kupambana kupata Katiba Mpya hakikuwa sahihi, kwani tayari ilani ya uchaguzi ya chama hicho ilishaahidi kushughulikia suala hilo...
  3. Parabolic

    JamiiForums Tanzania CHADEMA Mara wamkana kiongozi aliyehamasisha maridhiano

    Chama cha Demokrasia Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Mara kimemkataa Katibu wa mkoa huo Donald Felix Mwembe aliyesema kuwa chama hicho kikiongozwa na Makamu Mwenyekiti wake John Heche kinatakiwa kuzungumza na watawala ili kufikiwa kwa muafaka wa kesi ya uhaini inayomkabili Tundu Lissu. Soma pia...
  4. Parabolic

    JamiiForums Tanzania HOJA Kwamba Rais Samia hataki 'Jeshi' lake lichafuke? Kuna uwajibikaji tena hapo?

    Akizungumza baada ya kuwaapisha wakuu wa mikoa na makatibu tawala aliowateua na kuwabadilishia vituo vya kazi Septemba 2, 2026, katika Ikulu Ndogo ya Tunguu, Zanzibar, Rais Samia Suluhu Hassan, alitaja moja ya sababu ya kuwateua kuwa ni kuwalinda na kuwapusha changamoto zilizokuwa...
  5. Parabolic

    JamiiForums Tanzania PostGE2025 Meya wa Dar Awaita Wananchi Kutoa Ushahidi Wa Ghasia Za Oktoba 29

    Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Nurdin Bilal Juma, maarufu Shetta amewataka Wananchi wa Jiji la Dar es Salaam kujitokeza kwa wingi kutoa ushahidi wao kwenye tume ya Uchunguzi wa Jinai kufuatia ghasia za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025. Soma pia: Tume ya Jaji Lila...
  6. Parabolic

    JamiiForums Tanzania PostGE2025 Jaji Lila Awaita Wananchi Wa Ilala Kutoa Ushahidi Kwa Tume Ya Uchunguzi Wa Ghasia Za Uchaguzi Mkuu Oktoba 29

    Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi wa ghasia za Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 Jaji Shaban Lila amewataka Wananchi wa Wilaya ya Ilala kujitokeza kwa wingi kutoa ushahidi wa matukio ya ghasia hizo, kuanzia Jumatatu August 31 hadi Septemba 4, 2026 katika viwanja vya Karimjee Posta. Soma pia: Tume...
  7. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Ulimwengu: Kwa miaka 10 iliyopita, hakuna uchaguzi bora uliofanyika kama wa CHADEMA

    Mwanahabari mkongwe nchini, Jenerali Ulimwengu amesema Tanzania inapaswa kujipa muda katika kujenga mifumo bora ya kidemokrasia, akitolea mfano uchaguzi wa ndani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa mapema Januari 2025, kama miongoni mwa chaguzi za mfano zilizofanyika kwa uwazi...
  8. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Mwabukusi: Kama tunataka kupona kitaifa tutibu kwanza majeraha

    Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Wakilj Boniface Mwabukusi, amesema Tanzania inahitaji umakini, kusikilizana na kukubali makosa ili kujenga maridhiano na kuanza mchakato wa uponyaji wa taifa. Mwabukusi amesema hayo Agosti 28, 2026, katika Jukwaa la Demokrasia, akisisitiza kuwa...
  9. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Heche: Pressure iongezeke kuwafanya viongozi walio madarakani kufanya mabadiliko

    Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), John Heche amesema kuna haja ya kuongeza msukumo kutoka kwa wananchi ili kuwafanya viongozi waliopo madarakani kutambua umuhimu wa kufanya mabadiliko ya Katiba. Heche amesema chimbuko la baadhi ya matatizo yanayotokea nchini...
  10. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Profesa Tibaijuka ataka maboresho ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano kuimarisha mifumo ya uchaguzi

    Profesa Anna Tibaijuka amesema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 inahitaji kufanyiwa maboresho katika maeneo mbalimbali ili kuimarisha mfumo wa kisiasa na uchaguzi nchini. Profesa Tibaijuka ameyasema hayo leo Ijumaa, Agosti 28, 2026, wakati akizungumza katika Jukwaa la...
  11. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Bakari Kazungu asimulia kutekwa, kuteswa na kuachana na siasa: “Nilijua naenda kufa”

    Agosti 4, 2026, kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bakari Kazungu, alitekwa na watu wasiojulikana jijini Tanga na baadaye kupatikana akiwa amepigwa na kuteswa vibaya. Kabla ya tukio hilo, Kazungu alikuwa akitumia mitandao ya kijamii kukosoa baadhi ya mwenendo ndani ya chama chake na kueleza...
  12. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Joseph Mwasote: Kutekwa, kuteswa na kumpoteza mwana katika uchaguzi wa 2025

    Kwa takriban miaka 20, Joseph Mwasote amekuwa sehemu ya safari ya kisiasa ya CHADEMA, akipanda kutoka uongozi wa Kata ya Tunduma hadi kuwa mwenyekiti wa Mkoa wa Mbeya na baadaye kugombea ubunge wa Mbeya Vijijini mwaka 2020. Lakini uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, kwa maelezo yake, uligeuza maisha...
  13. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Masauni Ashiriki Kikao Kujadili Afya Ya Udongo Na Matumizi Sahihi Ya Mbolea

    Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni (katikati) akizungumza wakati wa kikao kilichokutanisha viongozi kutoka matifa mbalimbali katika Ubalozi wa Uingereza nchini Mongolia. Kulia ni Mwakilishi Maalumu wa Uingereza nchini Mongolia Bi...
  14. Parabolic

    JamiiForums Tanzania Othman: Zanzibar haitonyooka bila Baraza madhubuti la Wawakilishi

    Mwenyekiti wa Chama cha ACT Wazalendo Taifa, Othman Masoud Othman, amesema Zanzibar haitofikia maendeleo ya kweli pasi na kuwepo Baraza makini la Wawakilishi, linalosimamia maslahi ya Umma na matakwa ya Wananchi. Amesema Zanzibar katu haitonyooka hadi kuwepo na Baraza madhubuti la Wawakilishi...
  15. Parabolic

    JamiiForums Tanzania NEC ya CCM kukutana kwa dharura

    Kikao cha dharura cha Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM kinatarajiwa kufanyika baada ya makatibu wa chama kuanza kukutana Kikaangoni, Zanzibar, ikiwa ni siku 28 tangu kikao cha awali cha NEC kilichofanyika mjini Unguja. Kikao hicho kilichoitishwa kufuatia kujiuzulu kwa Makamu wa Rais Dk...
Back
Top Bottom