Recent content by Parabolic

  1. Parabolic

    Bei ya Mafuta Imepandaje wakati Serikali ilisema kuna akiba hadi Julai 2026

    Waati Serikali ya Tanzania ikitaja vita vinavyoendelea kati ya Marekani na Israel dhidi ya Iran kuwa ndiyo chanzo cha ongezeko la bei za mafuta kuanzia Aprili 1, 2026, utata umegubika suala hilo kutokana na kauli za viongozi wa Serikali waliowahakikishia Watanzania kuwa kuna mafuta ya kutosha...
  2. Parabolic

    CHADEMA Yapinga Uteuzi wa Jakaya Kikwete ndani ya AU, Yataka Mapitio ya Haraka

    Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeiandikia Umoja wa Afrika (AU) kikitoa wito wa kufanyika kwa mapitio ya haraka kuhusu uteuzi wa Jakaya Kikwete kama Mwakilishi wa Ngazi ya Juu wa Mwenyekiti wa Tume ya Umoja huo kwa Ukanda wa Pembe ya Afrika na Bahari Nyekundu. Machi 25, 2026...
  3. Parabolic

    Mtandao wa Pan-African Solidarity wahoji Hali ya Haki za Binadamu Tanzania na Uganda, Wataka Wafungwa wa Kisiasa Waachiliwe

    Mtandao wa wanaharakati wa demokrasia barani Afrika, Pan African Solidarity Network, umetoa tamko kali ukieleza wasiwasi mkubwa kuhusu kuzorota kwa hali ya haki za binadamu katika nchi za Afrika Mashariki, hususan Tanzania na Uganda, huku ukitaka hatua za haraka kuchukuliwa kulinda demokrasia na...
  4. Parabolic

    Heche: Bwege alikuwa mpigania haki

    Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche amesema Mbunge wa zamani wa Kilwa Kusini, Suleiman Said Bungara maarufu Bwege, alikuwa mwanasiasa anayepigania haki za watu wake na Taifa kwa ujumla. Ameyasema hayo leo Machi 31 katika mazishi ya Bwege wilayani Kilwa Mkoa wa Lindi. Bwege alifariki Machi...
  5. Parabolic

    Tafakuri kuhusu matokeo ya Tume za Rais zilizochunguza mgogoro wa ardhi, uhamaji katika Eneo la Hifadhi Ngorongoro

    Machi 12, 2026 Rais Samia Suluhu, alipokea taarifa ya Tume za Rais alizoziunda kutathmini masuala ya mgogoro wa ardhi na utekelezaji wa zoezi la uhamaji wa hiari wa wakazi kutoka eneo la Hifadhi ya Ngorongoro, Ikulu Chamwino, Dodoma. Soma: Rais Samia apokea taarifa ya Tume za Rais kuhusu...
  6. Parabolic

    I&M yapanua uwekezaji sekta ya fedha, ikifungua tawi ijpya Dar

    Benki ya I&M imeendelea kupanua uwekezaji wake katika sekta ya fedha baada ya kufungua rasmi tawi lake la tisa katika eneo la Palm Village, Mikocheni jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kusogeza huduma za kifedha karibu na wananchi na kuchochea ujumuishaji wa kifedha kwa wateja...
  7. Parabolic

    Heche aitembelea familia ya Nyalusi Iringa

    Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche ameitembelea familia ya aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Iringa, Frank Nyalusi aliyefariki Septemba 19, 2025 katika Hospitali ya rufaa ya Iringa alipokuwa akipatiwa matibabu. Soma: Frank Nyalus afariki dunia Heche ambaye hakuhudhiria mazishi...
  8. Parabolic

    Mawakili wa Lissu wamfungulia kesi Kamishna wa Magereza na Mkuu wa Gereza kuu la Ukonga

    Sisi mawakili Maduhu William, Nashon Nkungu na Paul Kisabo tumefungua shauri la Kikatiba ambalo ni Shauri No. 7300dhidi ya Kamishina Jenerali wa Magereza, Mkuu wa Gereza la Ukonga na Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Shauri hili limefunguliwa katika mahakama kuu masijala kuu ya Dodoma. Tumefungua...
  9. Parabolic

    Harbinder Sethi atakaswa na Polisi

    Harbinder Singh Sethi (Singasingal, mwenyekiti mtendaji wa makampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited IPTL) na Pan African Power Limited (PAP), amesafishwa na Jeshi la Polisi kwamba hakabiliwi na makosa yoyote. kwa tuhuma zilizokuwa zikimkabili zikiwamo za mradi tata wa...
  10. Parabolic

    TANZIA Waziri William Lukuvi (na Mbunge wa Isimani) afariki Dunia

    Unaweza kusema ni mbuyu umeanguka katika siasa za Tanzania, kwani William Vangimembe Lukuvi ndiye aliyekuwa mbunge mkongwe kuliko wote katika Bunge la 13 linaloendelea sasa na waziri mwenye uzoefu mkubwa kuliko wengine. Waziri Lukuvi aliyeingia bungeni tangu mwaka 1995 aligombea na kushinda...
  11. Parabolic

    Hoja nne za CHADEMA Mahakama ya Rufani katika mapitio kesi ya mgawanyo wa mali

    Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA, Dk Rugelemeza Nshala amefafanua hoja nne walizowasilisha katika Mahakama ya Rufani katika marejeo ya kesi ya mgawanyo wa mali za chama hicho, leo Machi 24, 2026. Hoja hizo ni pamoja na ukomo wa muda wa mgogoro unaobishaniwa, thamani ya mali zinazotakiwa kugawanywa...
  12. Parabolic

    Wasiwasi watanda, Tume ya Jaji Chande ikikamilisha ripoti yake

    Wakati muda wa Tume ya Kuchunguza Uvunjifu wa Amani kabla na baada ya Oktoba 29, 2025 ikikaribia mwishoni katika uchunguzi na kutoa ripoti yake, Watanzania wana kiu ya kuona ripiti hiyo itakuja na majibu gani. Tume hiyo iliundwa Novemba 20, 2025 na Rais Samia Suluhu Hassan kufuatia kuwepo kwa...
  13. Parabolic

    Profesa Tibaijuka aitabiria ushindi CHADEMA

    Waziri wa zamani na kada wa CCM Profesa Anna Tibaijuka ameitabiria ushindi CHADEMA, akisema katika misukosuko inayopitia ikiwa pamoja na tishio la kufutwa, chama hicho kitashinda. Katika andiko lake lenye kichwa cha habari: "MAWAKILI WA CHADEMA WAKIWASILI DODOMA KUTETEA CHAMA CHAO" aliloliweka...
  14. Parabolic

    Sugu: Nilikuwa team Mbowe, ila Lissu ni mwanangu

    Mwenyekiti wa Kanda ya Nyasa CHADEMA, Joseph Mbilinyi a.k.a Sugu amesema katika uchaguzi mkuu wa chama hicho Januari 2025 alikuwa akimuunga mkono aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, lakini alikuwa na urafiki zaidi na Mwenyekiti wa sasa, Tundu Lissu. Akizungumza katika mahojiano...
  15. Parabolic

    Lissu awasilisha maombi kwa hati ya dharura Mahakama ya Rufani

    Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu amewasilisha maombi mbele ya Mahakama ya Rufaa akiomba kusikilizwa kwa haraka kwa kesi yake ya uhaini. Kesi hiyo iliahirishwa wiki tatu zilizopita baada ya upande Jamhuri kukata rufaa katika Mahakama ya Rufani, ukitaka marejeo ya uamuzi wa Mahakama kuu...
Back
Top Bottom