Niliappeal lakini sijapata tena, naona mwaka huu imeshaniwia vigumu sana kusoma. Ngoja nisubiri intake ya March 2026 panapo majaaliwa nijaribu tena. Asanteni kwa ushirikiano ndugu.
Nilithibitisha vyuo vinne vyote nilivyochaguliwa, tena nilituma HESLB kuwa nitaenda kozi mojawapo ya chuo kimoja. Kwa sababu sikuwa na uhakika nilithibitisha vyote nilivyokuwa nimechaguliwa kujiunga navyo, je ndiyo sababu sijapewa mkopo nilitakiwa nithibitishe chuo kimoja tuu au ?
:D:D:D:D Umaskini wangu ni changamoto ndugu, ndio maana ninahaha. Shule ninaitaka sana ila Hela ya kulipia ni nyingi kweli SINA !!!!! Bila mkopo wa hawa ndugu wa HESLB sitafanikiwa kusoma.
Ahaaaah, sawa nitaendelea kusubiri nione. Vyuo nilishaconfirm VYOTE vinne nilivyochaguliwa mda mrefu kabla hata ya kutuma maombi ya kukopeshwa na wakuu HESLB.
Ni hicho cha binafsi chenye kozi ya diploma in Optometry.
Ahaaah sawa ngoja nisubiri, kwani wanatoa lini ?
Kitufe cha Appeal loan kikibonyezwa hakifunguki
Hapo kwenye SIPA mpaka nibonyeze sana vile vitufe vya kwenye akaunti, haifunguki moja kwa moja.
Ahaaah, asante kwa ushauri mzuri ndugu...
Sijapewa mkopo kwa sababu nina multiple selections labda mtu akiripoti chuo ndiyo anapewa mkopo ? Maana kuna msichana alihitimu kidato cha nne 2022 school candidate amepata na alichagua kozi moja tuu, akapata nafasi, Nipo njia panda ninaombeni Msaada wa ushauri au maelezo tafadhali 🙏.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.