Ninavyisema miezi mitano ni kama mfano tu. Ila jamaa anaweza kununa hata mwaka na zaidi. Ndo maana nikalileta huku. Na anafanya chini juu nisipate hata jinsi ya kuchepuka kwa sababu anajua ukame nnaopata
Ndg yangu kununa kwake kama nilivosema mwanzo yeye ni jambo la kawaida. Na kama kuomba msamaha nimeomba saaaaana kamaa unavyoona ni ndani ya miaka 13 maisha yamekuwa ni hayo. Ndo maana niko kwenu kujaribu kutafuta jinsi ambayo pengine sikuwahi kuitafuta
Na nikijaribu kujishusha ananinanga wee mpaka naumia. Siku zote ananifanya nionekane tatizo liko kwangu. Najishusha ili maisha yasonge lakini analazimisha mgogoro unakuwepo. Miaka 13 sasa ya ndoa , mwendo ndo huo. Nisaidie nifanye nini maana tumezaa watoto watatu.
Mimi ni mgeni jamvini lakini ni muuini mzuri mzuri wa jf. Nawataka mnisaidie katika hili. Inawezekana mume akamnunia mkewe kwa miezi mitano na zaidi? Wanalala kitanda kimoja na kuishi nyumba moja bila mgegedo? Nisaidieni jamani.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.