Chris, mimi ni mwana CCM mwenzako, nakuunga mkono kwa ushauri mzuri. Siku zote tuweke maslahi ya Taifa letu mbele na si binafsi wala itikadi zetu hususani katika suala hili muhimu la katiba ya watanzania wote. Kuna baadhi ya watu wanajisahau na kufikiri Tanzania ni ya chama fulani, la hasha ni...
Duuh usomi wa Tanzania unakuwa ni balaa sasa. Je, ni kwasababu mfumo wetu wa elimu ni mbaya kiasi hicho mpaka wanaojiita wasomi kukurupuka hivyo? Kwa msomi aliyebobea hawezi kuja na kichekesho cha namna hii. Msomi anapaswa kufanya utafiti kwanza. Msomi gani anapiga kura ikawa ndiyo jibu lake...
CCM tumekwisha Kama kweli tunaviongizi kama Mwigulu, uzalendo gani ulionao kwa wna Iramba na nchi? Kuwarubuni watu wasiende kutoa maoni ya katiba yao? Jiulize swali rahisi, unafikiri watu walifuata nini kama sio kuangalia wachezaji wa Simba? Hivi ni kweli mtu mwenye kichwa kinachofanya kazi...
Duuuh, kwahiyo suala la kupigwa Ponda lilikuwa na baraka ya nani Kama sio waliokuwa na bunduki? Dhamira hukosesha raha mtendaji wa jambo. Maneno yako yanaonesha dhamira ya kutenda uovu inakusumbua. Pole!
Juliana, mimi ni mwana-ccm ila analysis uliyoifanya ina leta maswali mengi na hatustahiri kujipongeza abadani. Tungeweza kujipongeza kama tusingepoteza kata yoyote kwa wapinzani. Tungeweza kujipongeza kama angalau hata tungeongoza kwenye baadhi ya vituo huko Arusha. Juliana hujatoa takwimu ya...
Pole Kijakazi, Science is a process, Science is a method of thought. In doing a research some one uses scientific methods. So, Dr Mkumbo was doing a scientific analysis. Kwa hiyo kama unafikiri sayansi ni bailojia, kemia you should be out of track in research discipline Kijakazi.
Mwasi, Dkt Mkumbo angekuwa amezungumza tu generally bila kujaribu kufanya analysis ya kisayansi jibu lako lingekuwa sahihi, lakini unapofanya analysis ya kisayansi ambayo inakupelekea kutoa hitimisho, ambalo hilo hitimisho linaweza kuja kutumika na watafiti wengine, kwa hitimisho hili...
Uko sahihi sana 'Tume ya Katiba', huwezi kusema hakuna difference unless umetafuta effect size ambayo itakuonesha magnitude ya ulinganishi wa matokeo hayo. Anaweza kutumia Cohen'd d kutafuta effect size hiyo. Na common interpretation ya effect size ni hii hapa. 0.2 = small, 0.5 - medium na 0.8 =...
Dkt Mkumbo,
Uchambuzi wako ni mzuri na nimeupenda sana hususani kipengele cha kutaka kujua kama kuna 'significantly difference' ya matokeo ya awamu ya kwanza na ya pili. Ingawa katika kutafuta significant difference, kuangalia percentage difference, au means differnce tu na kuja na conclusion...
Naibu waziri wangu, Mulugo, mbona unaendelea kulitia doa taifa letu? Hivi umechanganyikiwa na nini? Umenukuliwa vibaya au ndivyo ulivyosema? Kamwe siwezi kuamini kama matamshi haya yametoka kwa mtu mwenye dhamana ya Elimu katika nchi yangu. Waziri wangu, umejitaabisha hata kidogo tu kusoma...
Kama ayasemayo Tundu Lisu yana ukweli, basi Tanzania demokrasia ni zero.
Kuanzishwa kwa vyama vingi ni kukuza demokrasia nchini, sasa kama kushindana kwa hoja kunashindikana na kuanza siasa taka ni hatari sana. Watawala wetu wawe na huruma kwa watawaliwa jamani. Hivi vyama vyote hata...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.