Recent content by milimo

  1. M

    Kwa mwendo huu tutampata kiongozi wa nchi anayejali maendeleo endelevu?.

    Mtazamo wa jamii husika ndio hujenga mifumo ya jamii hiyo. Nimefuatilia kwa karibu kupitia vyombo vya habari na kwa macho yangu mwenyewe kuhusu mwenendo wa kampeni za uraisi hasa kwa vyama viwili vyenye ushindani mkubwa (ccm & chadema/ukawa). Badala ya kushindana kwa hoja wanashindana kwa kuwa...
  2. M

    Nimebaki kushangaa tu

    1. Nashangaa na kutaka kujua ni nani aliyewafanya baadhi ya wana ccm kuwa na maneno ya kihuni? Kwa mfano; nimejaribu kutafakari kuhusu maneno ya "Musukuma" (Mwenyekiti wa ccm mkao wa Geita) nashindwa kuelewa kama kweli huyo ni kiongozi mkubwa wa chama na mgombea ubunge! Nimejaribu kuuliza...
  3. M

    Kiongozi makini hawezi kuja na propaganda za ufisadi

    Ninavyo amini hakuna mtu mmoja pekee ambaye anaweza akawa na ufisadi unaoweza kusababisha kusinyaa kwa uchumi wa nchi na pia kudumaza huduma za jamii. Pia hakuna mtu mmoja pekee ambaye anaweza kutokomeza ufisadi. Wale wanaokuja na gia za kutokomeza ufisadi kwenye utendaji wa umma watuambie wazi...
  4. M

    Somo tutakalojifunza toka UKAWA ni umuhimu wa KUJITOA (SACRIFCES) kwa ajili ya Nchi

    1. UKAWA sio chama ila ni mwamvuli wa kushirikiana kwa ajili ya ushindi na unambatana na kujitoa kwa kila chama 2. Kwa utitiri wa vyama vilivyopo sio rahisi kushirikisha kila chama kwa sababu itakua ngumu kukaa mezani pamoja, pia vyama vingine inawezekana ni matawi ya chama kimoja. 3. Ukitaka...
  5. M

    Somo tutakalojifunza toka UKAWA ni umuhimu wa KUJITOA (SACRIFCES) kwa ajili ya Nchi

    Natumaini kama nilivyo mimi, watanzania wengi wako makini (anxious) kujua hatma ya UKAWA. Nikiwasikiliza watu wengi wanavyongolea UKAWA kama vile ni jambo dogo na la kawaida, lakini kwa watu wenye kutazama kwa upana hata kama hawasemi lakini wanajua kuwa iwapo UKAWA watafanikiwa kufika mwisho...
  6. M

    Natangaza nia ila sifanani na mwingine yeyote .

    Natangaza nia si muda mrefu ujao. Kuna wengine wanasema wanafanana na Baba wa Taifa Marehemu Mwalimu Nyerere, wengine wanajifananisha na Marehemu Sokoine nk. Mimi natangaza kugombea lakini sifanani na yeyoye yule. Mwenyezi Mungu ameniumba kama nilivyo, nina mazuri na udhaifu kama binadamu...
  7. M

    Ni tabia chafu kwa viongozi wa chama kuingilia watendeja wa serikali.

    Tunavyoelekea kwenye uchaguzi mkuu na wakati baadhi ya vyama wameanza mchakato wa kuwapata watakao peperusha bendera na kunadi sera za vyama vyao ili wapate kuongoza serikali baada ya uchaguzi, nichukue nafasi hii kivisihi vyama kuchagua mtu/watu ambao wanajua hawatawangusha. Wakifanya makosa ya...
  8. M

    Makongoro Nyerere achukua fomu Dodoma, Asema akiwa Rais atapambana na Ufisadi na Rushwa

    Nimemsikia Mh. Makongoro Nyerere alivyokua anatangaza nia ya kutaka kurudi tena Ikulu. Nasema kurudi tena kwa sababu mara ya kwanza alikuwepo Ikulu kama mtoto wa Rais (tunajua mtoto wa Raisi anakua na heshima inayokaribiana kwa karibu sana na Raisi mwenyewe). Bahati mbaya kwa nchi zetu ambazo...
  9. M

    Kwa kutojua au makusudi, nadhani tunatumia vibaya maana ya neno siasa

    Nikiri kuwa mimi si mjuuzi wa kudadavua maana ya neno siasa kwa sababu siasa niliyosoma ni ile ya shule ya msingi na sekondari tu. Lakini bado ni wazi kwamba neno siasa linatumika sivyo ndivyo. Mtu akiongea vitu ambavyo vinaonekana ni poroja yaani visivyo na faida au uhalisia, mara utasikia...
  10. M

    Malengo,mikakati na mgawanyo utekelezaji

    Nionavyo moja kati ya mambo yanayotufanya tusipige hatua inayostahili kimaendeleo ni viongozi wetu wa juu kabisa kuchanganya kati ya Malengo na Mikakati ya kufikia malengo hivyo kuhangaika na mikakati bila kuwa na malengo kisha kupelekea kushindwa kujipima au kujitathimini wanapomaliza muda wao...
  11. M

    Tukubaliane bila aibu kwamba mchakato wa katiba mpya usimamishwe mara moja.

    Acha hasira mtanzania mwenzangu badala yake jenga hoja watu watakuelewa vizuri. Nina imani kuna siku utaelewa tunamaanisha nini baada ya upende mwingine kuwa madarakani. Wengine hutushabikii vyama ila tunataka yeyote atakaye kuwa madaraka utende sawa sawa.
  12. M

    Tukubaliane bila aibu kwamba mchakato wa katiba mpya usimamishwe mara moja.

    Ninamwomba sana Mwenyezi Mungu asikie kilio cha watu wengi wanaojali maslahi pana ya wananchi wengi kuhusu kusimamisha mchakato wa kuelekea kwenye upigaji kura za Ndiyo au Hapana kwa katiba inayopendezwa. Karibu watu wote wenye nia njema na nchi hii walipiga kelele, wanapiga kelele na bado...
  13. M

    Red brigade, katiba inayopendezwa na tume ya uchaguzi

    Red Brigade; Licha ya propaganda za chama tawala kupiga vita kikundi cha vijana wazalendo wa Chadema wakati wao wanayo Green Guard, vijana hawa ni muhimu sana sio tu kwa wapenda mabadiliko bali pia kwa Jeshi la polisi. Ni Muhimu kwa wapenda mabadiliko kwa sababu inawapa moyo wa kujiandisha...
  14. M

    Yaliyojiri katika Maadhimisho ya miaka 38 ya CCM Songea Mkoani Mkoani Ruvuma

    Hayo maandalizi ni baadhi ya fedha kidogo za escrow, nyingine kidogo watawagawia wagombea kuhonga kanga, vitenge, kofia (ili kuwanyamazisha) lakini nyingi wajanja wamegawana na zimekwenda USWIS. Na hao watoto ni wanachama wa CCM? Je wanajua maana ya vyama kama sio kuwatumikisha na kuwafundisha...
Back
Top Bottom