Habari za muda huu wana-JF,
Kwanini watu wengi, tunapoulizwa “Habari?” au “Upo vipi?”, jibu letu mara nyingi huwa ni “salama”, “niko poa” au “nzuri tu” hata pale ambapo kiuhalisia hatuko poa kabisa?
Ujuzi wa thamani hufichwa,
hauko wazi na haupatikani kirahisi. Hakuna mtu anayegawa ujuzi huo hovyo hovyo.
Njia rahisi na yenye ufanisi zaidi ya kupata ujuzi ni kufundishwa na mtu ambaye tayari ana ujuzi huo.
Hii ndiyo njia pekee inayoweza kuhakikisha unauelewa ujuzi huo kwa asilimia mia, kwa...
Ujuzi pia ni uwezo unaokua kupitia mafunzo, mazoezi na uzoefu.
Unaweza kuwa kwenye kazi za ufundi, taaluma mbalimbali, sanaa, biashara au michezo.
Kadiri mtu anavyofanya na kujifunza zaidi, ndivyo ujuzi wake unavyokua.
Wataalamu wengine wanaeleza kuwa kiwango cha juu cha ujuzi hufikiwa pale ambapo mtu anafanya jambo kwa ustadi bila kufikiria sana kila hatua.
Inakuwa kama sehemu ya kawaida ya uwezo wake.
Hapo ndipo mtu anakuwa mtaalamu wa kweli, kwa sababu utekelezaji wake unakuwa wa uhakika na wa kuaminika.
Kwa lugha rahisi,
ujuzi ni uwezo unaojifunzwa wa kufanya jambo na kupata matokeo yaliyokusudiwa kwa uhakika na kwa ufanisi, bila kupoteza muda au nguvu nyingi.
Ujuzi ni nini hasa
Ujuzi ni uwezo wa kufanya jambo fulani na kupata matokeo.
Sio kujua tu, bali kuweza kutekeleza kwa ufasaha, usahihi na ufanisi.
Je wewe unaelewa nini kuhusu ujuzi kwa mtazamo wako? Karibuni tushirikiane mawazo.
Kuangalia tarehe ya kujiunga au idadi ya post hakujibu hoja niliyoweka.
Hoja inajadili uwezo wa kujenga na kujibu hoja kwa mantiki, si historia ya akaunti ya anayechangia.
Kama una pingamizi juu ya wazo lenyewe, weka hoja yako wazi tuijibu kwa hoja.
Uwezo wa kujenga hoja na kujibu hoja kwa kuzingatia misingi ya mantiki, usahihi wa habari, na uwezo wa kuelewa maoni tofauti,
kisha kuyajibu kwa njia yenye nguvu na utulivu, ni moja ya ujuzi wa juu zaidi wa kiakili.
Hauhusiani tu na uelewa wa mambo, bali pia na uwezo wa kuyafanya wengine...
Ni kweli, mazingira yana chelewesha pesa, lakini kama mtu ana ujuzi wa thamani,
mazingira yatamchelewesha tu au kumlazimisha kubadilisha njia.
Lakini tayari anaweza kutengeneza pesa popote atakapo enda
tofauti na mtu ambaye hana ujuzi wowote ataweza kubadilisha mazingira na bado hataona...
Kwa kufanya kazi, unaenda kufanya kazi gani hasa ilhali huna hata ujuzi wa chini kabisa?
Nenda popote pale iwe jeshini,
au hata kwa vijana wengi wanaopendelea kukimbilia nchi za Magharibi
bila ujuzi huwezi kutengeneza pesa, popote pale ulipo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.