Nadhani wamepewa heshima tu, hasa namna ya kuwabeba ili kuboresha record zao. Kwa sasa rekodo zao zitasomeka wameshiriki makombe ya dunia sita mfululizo!! Hiyo rdkodi kuivunja siyo mchezo!!
Je kwenye soka umri ni namba tu kama ilivyo kwenye mahusiano? Je Ronaldo(41) na Messi(39) bado wana cha kuonesha na kuwakosha mashabiki kiukweli kabisa au watabebwa na majina tu bila kuonesha soka safi la ushindani? Je wamewazibia tu vijana wengine ambao walipaswa kupewa nafasi kuliko vijeba...
Gepu limepungua sana baina ya mataifa yalitokuwa yanatawala soka na mataifa mengine chipukizi katika kusakata kandanda.
Tutarajie matokeo yasiyotarajiwa maana kuna vigogo wataadhirika kwa kichapo kutoka nchi zisizokuwa na historia kubwa ya soka. Kuna nchi toka Afrika na Asia zitashangaza...
Huu ndiyo wakati muafaka wa Ureno kubeba kombe la dunia. Ina vipaji lukuki na bado wanaye veteran CR7 wa kuwahamasisha ndani ya uwanja! Bila shaka haya yatakuwa mashindano ya mwisho CR7 kushiriki kombe la dunia kama mchezaji! Mashindano yajayo atakuwa na miaka 45!! Nadhani baada ya Euro 2028...
Wadau walionya mapema watoto hawa wasiahidiwe!! Unaona sasa, athari zinajitokeza mapema kuelekea fainali za kombe la dunia 2026.
Wadau jipangeni kuwaandaa watoto hawa kisaikologia ili kupunguza athari!!
Zama za CR7 hazijaisha ila zinaelekea kuishia!! Ndio maana watu na akili zao bado wanamlipa mamillioni ya dola! Bado ni mfungaji bora kwa timu yake na bado mchango wake kwa timu ya Taifa unahitajika sana! Ukimchukulia poa anakuliza fasta!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.