Shida ya nchi hii ni kutokuwa na utamaduni wa kufuata Sheria. Hao maafisa usafirisha mitandao wanapokamatwa kwa wrong parking wanakuwa wamepark sehemu zilizoruhisiwa? Mara nyingi ni hapana. Hapo wanakuwa wametenda kosa. Lakini pia swali lingine ninalojiuliza jiji limetenga parking kwa ajili yao...
Shida kubwa hapa ni kutoaminiana na papara. Kama watu wakitulia wakaacha papara na wakawa na nia na upendo wa kweli, uchaguzi huu utakuwa wa amani na hicho ndi ho tunachotaka. Naamini nafasi Bado ipo ya kurekebisha mambo.
Sasa hivi nchi nyingi maskini hasa za kiafrika ziko katika kulia na kulalamikia hatua ya Marekani kuondoa ruzuku na misaada mbalimbali inayogharamiwa na tax payers wa Marekani.
Ninajiuliza hivi kwa nini tunakaa kulialia badala ya kutafuta njia ya kuweza kujiendesha na kujisaidia bila kutegemea...
Kwa demokrasia ya kiafrika kama kwenye kampeni na harakati ulikuwa katika upande ulioshindwa, ni ngumu kuendana na upande uliokuwa unaupinga ingawa ulishinda. Busara ndogo tu ni kuamua kujitoa. Pia busara kubwa zaidi ni kuzika tofauti za kampeni baada ya uchaguzi ili mambo yaende sawa
Bahati mbaya sana kwa watu waliokuwa na matumaini na kuiamini CDM. Hapo nyuma watu waliikubali na ilileta matumaini kwa watanzania wapenda mageuzi. Lakini leo hii uchaguzi wa sasa umeiacha CDM katika sintofahamu. Wanachama na wapenzi wa chama hiki wamebaki kwenye dilema wakiangalia jahazi...
Imekuwa ni nafasi nzuri ya kuwafahamu wanasiasa uchwara wanaoropoka bila kujua wayasemayo. Najiuliza Wenje at his rank anawezaje kuzungumza akiwa hana concrete evidence? What if FAM akibwaga manyanga na kumsuport Lisu Wenje atakuwa upande upi? Amejikaanga kwa mafuta yake mwenyewe!
Nadhani siku zilizobaki kabla ya uchaguzi zinatosha kubadili mambo ndani ya Chadema. Busara ikitumika na FAM akakubali yaishe akajitoa na kumuunga mkono Lissu siyo tu kwamba itaondoa mgogoro bali itaifanya Chadema kuwa imara kuliko siku zote, FAM atakuwa shujaa wa demokrasia na ataenziwa daima
Kwa kweli kwa mfumo uliopo ni ngumu kwa watu wengi kuwa muitikio mzuri wa kupiga kura.
Uchaguzi unashindikana kuwa wa haki kwa sababu hakuna neutrality kuanzia kwenye campaigns, uandikishaji wa wapiga kura, usimamizi, kuhesabu na pia utangazaji wa matokeo. Kwa mfumo huu ulivyo there is no way...
Shida yetu watanzania tunapienda kwenye chaguzi za wabunge tunatanguliza vyama kwanza. Unajikuta kama una support chama fulani basi utampigia kura mgombea wa chama chako bila kujali uwezo wake na kupelekea kuwa na wabunge wasio na uwezo wa kuchambua na kujenga hoja!
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.