Recent content by Joo Wane

  1. J

    JamiiForums Tanzania Tetesi: Good News. Yule Shujaa Mwanamke wa Shoka, Shupavu na Shujaa wa Chadema, Kamanda Halima Mdee, Iron Lady is Back Ndani ya Nyumba!.

    Hivi suala hapa ni kutoka nje ya CHADEMA au usaliti kwa CHADEMA. Je Halima na wabunge wenzake wa mchongo waliwahi kuwaambia watanzania au hata wana CHADEMA wenzao walifikafikaje bungeni. Na ile jeuri ya Halima na wenzake kushindana na chama mahakamani ilitokana na nini na ghafla kimebadilika...
  2. J

    JamiiForums Tanzania Peter Msigwa: Nilienda CCM kutokana na Uongozi uliokuwepo CHADEMA ulikuwa unakiuka Misingi ya Demokrasia

    Suala kubwa hapa sio kwenda upande ule bali akiwa kule aliongea nini kibaya kuhusu alikokuwa ametoka. Ila kila siku nasema hao CHADEMA ni kama kenge tu hawasikii mpaka damu ziwatoke masikioni. Wasaliti wanarudi kama nyumbu halafu wanapokelewa kwa mbwembwe na bashabasha. Hao walipaswa waishie...
  3. J

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Tetesi: Tetesi za usajili Ligi Kuu msimu wa 2026/27

    Kwangu mimi huyo Msimu, William Edgar, Idd Nado na yule Rashid Chambo ndio mawinga ninaona wanafaa pale Simba. Wana kasi na nguvu sana aina ya mpira anaopenda Barker. Ila pale kwa Sopu naona ile ni dili ya wajanja pale Simba kwenye kamati ya usajili kama ilivyokuwa kwa Miraji Zambo. Wazee wa...
  4. J

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Tetesi: Tetesi za usajili Ligi Kuu msimu wa 2026/27

    Mkuu wewe umeona mbali. Kikubwa timu ziwe makini maana mawakala wapo kazini.
  5. J

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Simba ijiongeze nje ya uwanja kwa gharama yoyote lasivyo Yanga anaenda kubeba kombe mara ya tano, aibu hii

    Simba kukosa ubingwa ni uzembe wao tu. Ubingwa hautafutwi mwishoni mwa ligi au kutegemea mshindani wako apoteze mechi. Ubingwa unatafutwa mwanzoni mwa ligi wakati timu nyingi za kati na zile za chini zinapokuwa zinasuasua. Simba kabla ligi haijaanza viongozi wake na msemaji wao wana kelele...
  6. J

    JamiiForums Tanzania CHADEMA, chagua Moja kukumbatia wasaliti au Wananchi!

    Hawa CHADEMA naona hapo walipofika wamejisahau kabisa na anguko lao linakuja muda si mrefu na wakija wakishtuka itakuwa too late. Hakuna cha mwenye afadhali hapo Halima Mdee aliifanya nini CHADEMA mahakamni eti alikaa kimya kwa nini hakuutema ubunge feki. Je leo CHADEMA ikichukuwa nchi halafu...
  7. J

    JamiiForums Tanzania Neno langu kwa wasaliti wote wanaorejea CHADEMA: Karibuni nyumbani, ila....

    CHADEMA ni kama kenge tu mpaka damu iwatoke masikioni ndio watasikia. 1. Hivi ni nani asiyejua vituko vya huyo Jose Selasini alivyomfanyia Mbatia kule NCCR na wala sio miaka mingi ni juzi juzi tu. Lile halikuwa shambulio kwa Mbatia au NCCR bali kwa watu wenye akili timamu lile lilikuwa ni...
  8. J

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Tetesi za kuachwa loemba na siasa za Mo

    Ni kweli shida ya baadhi ya wachezaji wakisikia mashabiki wanakaanga chipsi jukwaani mabega yanapanda na kifua kinatanuka lakini kiukweli hakuna mashabiki wa hovyo kama wakibongo leo wanakusifia kesho wanaandama kwa viongozi utimuliwe.
  9. J

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Tetesi za kuachwa loemba na siasa za Mo

    Loemba kuachwa Simba ni yeye mwenyewe na miguu yake ndiyo ataamua na wala sio kiongozi au mtu mwingine yoyote yule. Loemba ni bonge la mchezaji na hilo amelithibitsha yeye mwenyewe na miguu yake mara tu alipofika Simba. Mechi za mwanzo za ligi ya nyumbani na hata za kimataifa kacheza vizuri...
  10. J

    JamiiForums Tanzania KERO KKPESA: Benki Kuu ifuatilie hii kampuni ya Mkopo

    Yaani wewe mleta mada una bahati sana maana hawa jamaa wanakupiga tu mikwara. Nimeshuhudia wafanyakazi wezangu watatu wametukanwa matusi ambayo hayasemeki na yakasambazwa kwenye group la ofisi na bado pia kwenye group zao mbali mbali za whatssap zikiwapo za familia. Aisee ukiwa na shida hata ya...
  11. J

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Simba inajiamulia tu mambo yake! Yaipiga Coastal 2-1 na kuongoza Ligi Kuu, leo Mei 21, 2026

    Hongereni Simba kwa ushindi wa jana. Lakini nawakumbusha tena kuna mambo fulani yanonekana kama madogo madogo hivi yasipokemewa na benchi la ufundi au uongozi mtaendelea hivyo hivyo kutamba mna timu nzuri sana lakini makombe mtakuwa mnayaona yakipita hapo Msimbazi na "parade" yakielekea...
  12. J

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Tetesi: Tetesi za usajili Ligi Kuu msimu wa 2026/27

    Sawa mkuu ila naona kama hao wanaofanya usajili hapo Simba hawataitendea haki Simba. Sopu kwa Simba hii kiwango ilipofika Sopu sio chaguo sahihi ni bora mara mia kama wanahitaji winga basi wamrudishe Karabaka au wamsajili yule William Edgar ambaye anaweza kucheza "almost" nafasi zote za mbele...
  13. J

    JamiiForums Tanzania Roho Mbaya na Wivu wa Majirani: Kisa cha mtoto aliyetambaa hadi ndani ya gari Arusha kitufundishe umuhimu wa CCTV

    Na hii waswahili ndiyo wanaifanya kuwa ni silaha yao kubwa ya maangamizi ya nyuklia ili uwe mpole hata wakikunyanyasa au wakikuletea uswahili wao uwe mpole ukubaliane nao. Kwangu mimi naamini kuzikwa na watu wengi au wachache kote ni kuzikwa tu hakuleti tofauti yoyote. Ni basi tumejijengea tu...
  14. J

    JamiiForums Tanzania Roho Mbaya na Wivu wa Majirani: Kisa cha mtoto aliyetambaa hadi ndani ya gari Arusha kitufundishe umuhimu wa CCTV

    Uswahili ni uswahili tu. Wapo waswahili wenye hela na wasio na hela pia wapo wenye elimu na wasio na elimu. Nilihamia sehemu moja nje ya mji nikiwa mtu wa kwanza kwanza. Wakaja majirani zangu kujenga wakanikuta na ni watu wameenda shule tu vizuri. Nikawapokea nikafurahi kuwa wakimaliza ujenzi...
  15. J

    JamiiForums Kenya, JamiiForums Tanzania Okwi vs Chama: Nani anastahili kuwa mchezaji bora wa muda wote wa Simba SC?

    Aisee kwa mtu aliyewaona wote wakiwa kwenye viwango vyao lazima atapata ugumu wa kujua nani mkali zaidi ya mwingine. Lakini kwa mtizamo wangu mimi narudia tena kwa mtizamo wangu mimi Chama ni zaidi kwa sababu pamoja na kufanya kazi yake uwanjani kwa usahihi sana yeye anakitu cha ziada nacho ni...
Back
Top Bottom