Rais Jakaya Kikwete amesema anashangazwa na Mwanasheria wa Chadema, Tundu Lissu kumtaka amtaje mhusika wa Richmond wakati mwenye Richmond yupo na anatembea naye mikoani.
Tundu Lissu Kaweka mtego ambao kwa upande wowote utapanic utunaswa.
Nikweli kwamba hichi kipindi sio rahisi kwake hivyo tumuombee Mungu amwongoze ajue watanzania wanahitaji nini, angalie maslahi mapana ya watu walio nyuma yake.
Inashangaza, inamaana kwa kipindi chote hicho walikuwa hawana ushahidi wakumpelaka mahakamani? Maana swali bado litabaki kwamba, kama tuhuma zao ni za kweli kwanini hakupelwekwa mahakamani?
Kwa mujibu wa utawala wa Katiba na Sheria zetu mtu anabaki kuwa "innocent" mpaka mahakama itakapomhukumu kuwa katenda kosa chini ya sheria. Ila nchi hii mtu anatuhumiwa halafu wanaotakiwa kumpeleka mahakamani hawampeleki kuthibitisha tuhuma halafu wanatuaminisha wananchi kuwa tayari katenda kosa...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.