Tatizo ni kwamba kitakachorekodiwa na kurushwa huenda ni kile kitakachokuwa na maslahi kwa serikali na chama chake. Sitegemei kwamba michango ya wabunge wa upinzani itarushwa sawa na ya wabunge wa CCM. Bunge letu haliko huru, bado linafanya sana kazi ya kuitetea serikali hata ambapo sipo...
Matatizo mengine watanzania tunajiletea wenyewe halafu baadaye tunaanza kulalamika. Sisi wenyewe ndo tunaanza kupandikiza mawazo ya udini na ukanda ndani yetu kwa kauli zetu baadaye tunakuwa wa kwanza kulalamika na kuwasema wapinzani ni wadini na wakanda. Mi nadhani kiongozi mzuri atateua kwa...
Pole nyingi sana kwa Nape. Mungu amjalie apone maumivu aliyoyapata aendelee na shughuli zake za kila siku, lakini pia atambue kwamba Mungu ndiye anapanga maisha ya kila mmoja, kuanza kwake na kuisha kwake.
Labda kwa sababu ya umri. Siyo jambo la kawaida mwenyekiti wa chama unaacha kumuunga mkono mgombea wako halafu unampigia debe wa chama tawala, maana ya kuwa mpinzani ni nini kama unamuunga mkono mgombea wa chama tawala? Kama siyo umri basi atangaze tu kuwa mwanachama wa CCM.
Tuweke tofauti za vyama na kimitazamo pembeni katika masuala yanayohusu vifo. Ujue unaposema maneno ya kejeli, au yanayoonyesha wewe kutoumizwa au kufurahia kifo chake kwa vile tu alikuwa na mtazamo tofauti wa kisiasa, ujue kuna wengine waliobaki wanaumia zaidi. Kwa kauli kama hii uliyoitoa...
Tunaomba data mkuu, kama ulivyosema magufuli kafika 79% ya majimbo yote, tuambie pia, mpaka sasa kawafikia wananchi wangapi katika majimbo mangapi? Vinginevyo nitaichukulia hii kama propaganda kama propaganda nyingine zilizopita bila tija yoyote.
Ni hoja dhaifu sana kuongelea afya ya mtu badala ya kuongelea udhaifu wake kiuongozi na kimaendeleo. Hata hivyo nadhani katiba yetu inazuia mtu mwenye ugonjwa wa akili kugombea, lakini magonjwa mengine haijazuia. Kiukweli, naona CCM haina jipya lolote katika kampeni hizi, badala yake sasa...
Edit post yako mkuu:
Mwaka huu wapinzani mwaka huu, Mana, mgufuli, ilee------ndo nini?
Au ndo unazidi kuaminisha watu kwamba CCM haitoi kipaumbele katika elimu ili iendelee kutawala?
Mkuu umezisoma ilani za vyama vyote? Au ni mahaba ya kisiasa tu yanakuendesha? Hebu tupe tofauti ya ilani za vyama hivi (CCM V/s Chadema/ Ukawa) ndipo tujue kama ni ilani mbovu ama la! Vinginevyo tutajua umeongea tu na hujui chochote kuhusu ilani za uchagzi za vyama hivi. Au unashabikia chama...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.