🤣🤣 Unaota vipi unafukua fukua mkuu 🤣
Ila swala la mwili kuvimba au kuwasha baada ya kula vyakula ni kawaida Kwa watu wengi, mwingine akila nyama ya mbuzi anavimba, kwahiyo shida siyo nguruwe.
Mimi Kuna kipindi nilivimba Sana baada ya kula mayai nikayachukia Sana
Mimi pia nimekulia kwenye familia za madhehebu tofauti,
Kipindi Fulani nilikuwa Kwa wasabato, pale kitimoto Ilivyokuwa inazungumzwa mpaka unaogopa.
Sifa zote mbaya anapewa nguruwe, mpaka nikawa naogopa Sana.
Nikiona au kusikia mtu Fulani anakula kitimoto basi roho inakereka Sana nahisi...
Kule nilienda nikiwa mdogo wa miaka 12 hivi tu mkuu,
nilikaa kama mwaka mmoja hivi.
Isitoshe kule tulienda watoto kama 6 hivi tukitokea mwanza, Kuna mwenzetu yeye alikuwa mkubwa kwetu kama 15 years hivi ndiyo alisema twende geita. Kabla yake tulikuwa mwanza tunaokota vyumba chakavu, Kwa ufupi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.