TheChoji
JF-Expert Member
- Apr 14, 2009
- 5,014
- 15,402
Mimi ni mwanaume, nna mke na watoto lakini pia naishi na wadogo zangu wawili wa kike (miaka 18 - 21) na msichana wa kazi. Binafsi najua kupika vizuri na pia napenda kula vyakula vitamu. Mke wangu ni mtu wa kuchelewa kurudi na akirudi yuko hoi.
Kinachonisumbua ni kwamba, hawa ndugu zangu ninaoishi nao ni HAWAJUI KABISA KUPIKA na hawana interest hata ya kujifunza! Yaani mi naenda mjini narudi na sato, au kuku, maini, nyama, nk natia kwenye friji.
Viungo vyote, nazi, kila kitu nahakikisha kipo. Matarajio yangu nikija nikute chakula kizuri ila sasa hayo makorokocho ntakayokuta hata hamu ya kula inaniishia. Chuzi la nyama utalikuta jekunduu limejazwa mimaji na mimafuta, nyanya zinaelea, vitunguu havijaiva, halafu eti wamepika na ugali! Siku zikipikwa mboga za majani utadhani zimekatwakatwa kwa panga.
Yaani vululu vululu. Cha ajabu wao wanaona poa tu. Nimejaribu kuongea nao na mara moja moja hua naingia mwenyewe jikoni nakorofisha misosi ya nguvu. Lengo ni ili na wao watamani kujua kupika lakini naona interest hawana kabisa. Imefika mahali hata kuleta vitu tena naona haina haja bora niwe nakula mitaani.
Nawaza sijui wakija kuolewa itakuaje na kwakweli sijui niwasaidieje.
Kinachonisumbua ni kwamba, hawa ndugu zangu ninaoishi nao ni HAWAJUI KABISA KUPIKA na hawana interest hata ya kujifunza! Yaani mi naenda mjini narudi na sato, au kuku, maini, nyama, nk natia kwenye friji.
Viungo vyote, nazi, kila kitu nahakikisha kipo. Matarajio yangu nikija nikute chakula kizuri ila sasa hayo makorokocho ntakayokuta hata hamu ya kula inaniishia. Chuzi la nyama utalikuta jekunduu limejazwa mimaji na mimafuta, nyanya zinaelea, vitunguu havijaiva, halafu eti wamepika na ugali! Siku zikipikwa mboga za majani utadhani zimekatwakatwa kwa panga.
Yaani vululu vululu. Cha ajabu wao wanaona poa tu. Nimejaribu kuongea nao na mara moja moja hua naingia mwenyewe jikoni nakorofisha misosi ya nguvu. Lengo ni ili na wao watamani kujua kupika lakini naona interest hawana kabisa. Imefika mahali hata kuleta vitu tena naona haina haja bora niwe nakula mitaani.
Nawaza sijui wakija kuolewa itakuaje na kwakweli sijui niwasaidieje.