Hivi kwanini Nyerere aliidhinisha kunyongwa Mwamwindi?

Sesten Zakazaka

JF-Expert Member
Sep 10, 2017
10,561
19,056
Tunaambiwa katika kipindi chake chote cha cha miaka 23 kama Rais wa Tanzania Mwalimu Nyerere alisaini hati chache sana za kunyongwa watu waliopatikana na makosa mahakamani na kupewa adhabu ya kifo. Miongoni mwa hati za kunyongwa alizowahi kuziidhinisha ni ile ya aliyekua mkulima mkubwa wa enzi hizo mkoani Iringa Bwana Saidi Mwamwindi aliyeshtakiwa kwa kosa la kumuua aliyekua Mkuu wa Mkoa wa Iringa wakati huo Dr Kleruu

Kama umewahi kupitia hati za mashtaka, mwenendo wa kesi na maelezo ya hukumu ya watu waliopatikana na makosa ya kuua kwa kukusudia utagundua kwamba wengi wao walitekeleza mauaji hayo kwa ukatili sana wengine ukijiuliza hawa kweli walikua ni binaadamu wenye roho!? Pengine haitakupata huruma kwa hukumu inayopitishwa juu yao

Said Mwamwindi ni kweli aliua, na wala hakuisumbua mahakama kwani alikiri hivyo mwenyewe na akahukumiwa kunyongwa hadi kufa. Ila kuna simulizi nyiingi sana zinanazohusiana na mauaji aliyofanya na hata baadhi ya watu wanahalalisha kitendo alichofanya na kukiita cha kishujaa!

Wengi ya wanaomuana kua ni shujaa wanasema RC Kleruu alikuachanzo cha mauaji yake mwenyewe. Alikua kweli anamnyanya sana huyu Bwana Mwamwindi. Kwanza alikua anatoka kimapenzi na mkewe halafu alikua anamfatafata sana na kumtolea lugha za kashfa(abusive languages). Kibinadamu hiyo ni dharau na ni adhabu kubwa sana kumpa mwanaume mwenzio hasa kama umemzidi kwa cheo au hata pesa

Kwa intelijensia aliyokua nayo Mwalimu Nyerere lazima atakua alijua chanzo halisi cha Mkulima Mwamwindi kumpiga risasi RC Kleruu., na ingawa mazingira yaliyomfanya atende kosa lile yalikua hayampi nafuu yoyote kisheria linapokuja suala la adhabu kwa maoni yangu hati ya kunyongwa Said Mwamwindi haikupaswa kusainiwa harakaharaka hasa ikiwa inajulikana (angalau kwa uwazi) kua Nyerere hakupenda adhabu ya kifo

Nawauliza wakongwe waliopo JF wenye kujua vizuri historia ya tukio hili na yaliyotokana na jambo hilo, haraka ya Nyerere kusaini hati ya kunyongwa hadi kufa Said Mwamwindi ilitokana na;

1. Hasira za Nyerere kuuliwa RC wake?

2. Mauwaji aliyofanya Mwamwindi yalikua ni ya kikatili kuliko wauwaji wengine walioua kwa kukusudia?

3. Chuki za Nyerere kwa aliowaita Makabaila(wamiliki wa mashamba makubwa) ambapo Mwa
mwindi anaangukia hapo?

4. Double standards wanazokua nazo wanasiasa wengi hasa wa kiafrika katika kuwatendea
watu wao?


Naomba kuelimishwa wakuu
 
Si aliua na mahakama ikamkuta na hatia na hukumu ni kunyongwa mpaka kufa sioni hoja kubwa saana ya kwanini ilisainiwa. Kama hakukuwa na rufani. Nyerere alifanya kile kinachotakiwa kufanywa heko Nyerere.
Sibishi kwamba alipatikana na hatia kama alivyokiri mwenyewe na hukumu aliyopata ni stahili yake. Hoja ni kwamba kwanini Nerere asi sign za wengine waliouwa kwa ukatili mkubwa na akaidhinisha Mwamwindi anyongwe haraka?
 
Huyu jamaa kwangu bado ni shujaa sana lakini najiuliza hao wanaotaka kumpa Mwalimu utakatifu wanatumia vigezo gani ilhali mtu alikua ana sign hati za vifo?
Kuna suala jingine, kuna kitu kinaitwa extra judicial killings, viongozi wengi wa Kiafrika inawezekana wakawa hawaonekani kwamba wana idhinisha hati za hukumu za vifo kwa waliohukumiwa adhabu hiyo lakini wameua sana katika mauaji yasio ya kisheria, kimyakimya
 
Mie bubafsi siioni hoja ya kutuletea humu jf tujadili kwa sababu za msingi zifuatazo;
1. Anaposema nyerere alisaini hukumu ya kifo cha mwamwindi haraka.
- mtoa maada anaposema haraka, ana taarifa Ni siku ngapi Nyerere alisaini toka pale alipohukumiwa. Na anafikiri ingesainiwa siku ngapi baada ya hukumu kutolewa?
- je mtoa maada anajua kipindi ambacho Ni lazima Raisi awe amesaini hukumu ya kifo baada ya hukumu kutoka mahakamani?
- je mtoa maada ana taarifa za wengine ambao raisi aliwahisha au kuchelewesha kusaini hati zao za hukumu za kifo.
Swali kwa mtoa maada!
- Nyerere alisaini hukumu ya mwamwindi ya kifo baada ya siku ngapi tangu kuhukumiwa ili ilinganishwe kama iliwahishwa au kucheleweshwa!
- Mwamwindi alinyingwa siku ngapi baada ya Nyerere kusaini hati yake ya hukumu ili tujilidhishe kuwa aliwahisha!
Mwisho; Nahisi Mtoa maada hana ushahidi na uthibitisho kwa aliyoyaandika!
Raisi na Idara zilizokuwa chini yake zina utaratibu wake wa kufanya kazi.
ASISIKIE STORI ZA VIJIWENI AMBAZO MARA NYINGINE HAZINA UKWELI.
 
Mi nadhani nyerere hizo zingine labda halikua hazipi sign yake sababu sometime ilikua inakua ni mauwaji ya watu ambao hawafahamiki wala alie ua sio mtu anae fahamika,,,,hivo walikua hawatengenezi attention yoyote kwa taifa ambayo ingeweza kuwa positive au negative,,,,hivo mauaji ya aina hiyo wengi wao walifungwa kifungo cha maisha..

Lakn tukio hili la kuuwawa kwa mkuu wa mkoa bwana Kleruu tena kuuawa na tajiri mkubwa,,wote wanafahamika sana nchi nzima...hivo hilo jambo hilo lilitengeneza attention kubwa sana ndani na nje ya nchi huki kila mtu akisubiri kuona ni hukumu gani itafikiwa,,,

Lakn pia alie uliwa ni kiongozi mkubwa,,,,,nyerere angeteneza kitu kibaya sana kwa viongozi kutokuheshimiwa na kutokuogopwa japo hata kidogk kama angetoa hukumu nyepesi kwa huyu alie muua kiongozi.

Yote tisa kumi.......yawezekana pia ni mahakama yenyewe ndio ulio fikia huo kuafaka wa jamaa kunyongwa bila nyerere kuchangia lolote kimawazo juu ya hukumu hiyo
 
Kuna mengine utokea sababu ya fundisho kwa wengine.Kipindi cha ujamaa kulikua na chuki kati ya viongozi na wananchi wenye uwezo.Kitendo cha kuuliwa RC kingeachwa bila onyo kali kingeweza kua mwanzo wa mauaji mfululizo ya viongozi.Pale ni kwamba Serikali ilionyesha mamlaka yake .
Hii hoja inauzito flani hivi, hasa tukimpa mwalimu kitu kinaitwa benefit of doubt
 
Yote tisa kumi.......yawezekana pia ni mahakama yenyewe ndio ulio fikia huo kuafaka wa jamaa kunyongwa bila nyerere kuchangia lolote kimawazo juu ya hukumu hiyo
Ni mahakama ndio iliyofikia uamuzi huo baada ya Mwamwindi mwenyewe kukiri kosa la kuua kwa kukusudia na hapakua na chaguo jingine ila kumpa adhabu hiyo. Lakini kama ilivyo sheria, utekelezwaji wa hukumu hiyo hufanyika baada ya kuidhinishwa na Rais wa nchi kwa ku sign hati ya kunyongwa, kitu ambacho Mwalimu Nyerere inasemekana ilikua ni nadra sana kukifanya
 
Back
Top Bottom