Sesten Zakazaka
JF-Expert Member
- Sep 10, 2017
- 10,561
- 19,056
Tunaambiwa katika kipindi chake chote cha cha miaka 23 kama Rais wa Tanzania Mwalimu Nyerere alisaini hati chache sana za kunyongwa watu waliopatikana na makosa mahakamani na kupewa adhabu ya kifo. Miongoni mwa hati za kunyongwa alizowahi kuziidhinisha ni ile ya aliyekua mkulima mkubwa wa enzi hizo mkoani Iringa Bwana Saidi Mwamwindi aliyeshtakiwa kwa kosa la kumuua aliyekua Mkuu wa Mkoa wa Iringa wakati huo Dr Kleruu
Kama umewahi kupitia hati za mashtaka, mwenendo wa kesi na maelezo ya hukumu ya watu waliopatikana na makosa ya kuua kwa kukusudia utagundua kwamba wengi wao walitekeleza mauaji hayo kwa ukatili sana wengine ukijiuliza hawa kweli walikua ni binaadamu wenye roho!? Pengine haitakupata huruma kwa hukumu inayopitishwa juu yao
Said Mwamwindi ni kweli aliua, na wala hakuisumbua mahakama kwani alikiri hivyo mwenyewe na akahukumiwa kunyongwa hadi kufa. Ila kuna simulizi nyiingi sana zinanazohusiana na mauaji aliyofanya na hata baadhi ya watu wanahalalisha kitendo alichofanya na kukiita cha kishujaa!
Wengi ya wanaomuana kua ni shujaa wanasema RC Kleruu alikuachanzo cha mauaji yake mwenyewe. Alikua kweli anamnyanya sana huyu Bwana Mwamwindi. Kwanza alikua anatoka kimapenzi na mkewe halafu alikua anamfatafata sana na kumtolea lugha za kashfa(abusive languages). Kibinadamu hiyo ni dharau na ni adhabu kubwa sana kumpa mwanaume mwenzio hasa kama umemzidi kwa cheo au hata pesa
Kwa intelijensia aliyokua nayo Mwalimu Nyerere lazima atakua alijua chanzo halisi cha Mkulima Mwamwindi kumpiga risasi RC Kleruu., na ingawa mazingira yaliyomfanya atende kosa lile yalikua hayampi nafuu yoyote kisheria linapokuja suala la adhabu kwa maoni yangu hati ya kunyongwa Said Mwamwindi haikupaswa kusainiwa harakaharaka hasa ikiwa inajulikana (angalau kwa uwazi) kua Nyerere hakupenda adhabu ya kifo
Nawauliza wakongwe waliopo JF wenye kujua vizuri historia ya tukio hili na yaliyotokana na jambo hilo, haraka ya Nyerere kusaini hati ya kunyongwa hadi kufa Said Mwamwindi ilitokana na;
1. Hasira za Nyerere kuuliwa RC wake?
2. Mauwaji aliyofanya Mwamwindi yalikua ni ya kikatili kuliko wauwaji wengine walioua kwa kukusudia?
3. Chuki za Nyerere kwa aliowaita Makabaila(wamiliki wa mashamba makubwa) ambapo Mwa
mwindi anaangukia hapo?
4. Double standards wanazokua nazo wanasiasa wengi hasa wa kiafrika katika kuwatendea
watu wao?
Naomba kuelimishwa wakuu
Kama umewahi kupitia hati za mashtaka, mwenendo wa kesi na maelezo ya hukumu ya watu waliopatikana na makosa ya kuua kwa kukusudia utagundua kwamba wengi wao walitekeleza mauaji hayo kwa ukatili sana wengine ukijiuliza hawa kweli walikua ni binaadamu wenye roho!? Pengine haitakupata huruma kwa hukumu inayopitishwa juu yao
Said Mwamwindi ni kweli aliua, na wala hakuisumbua mahakama kwani alikiri hivyo mwenyewe na akahukumiwa kunyongwa hadi kufa. Ila kuna simulizi nyiingi sana zinanazohusiana na mauaji aliyofanya na hata baadhi ya watu wanahalalisha kitendo alichofanya na kukiita cha kishujaa!
Wengi ya wanaomuana kua ni shujaa wanasema RC Kleruu alikuachanzo cha mauaji yake mwenyewe. Alikua kweli anamnyanya sana huyu Bwana Mwamwindi. Kwanza alikua anatoka kimapenzi na mkewe halafu alikua anamfatafata sana na kumtolea lugha za kashfa(abusive languages). Kibinadamu hiyo ni dharau na ni adhabu kubwa sana kumpa mwanaume mwenzio hasa kama umemzidi kwa cheo au hata pesa
Kwa intelijensia aliyokua nayo Mwalimu Nyerere lazima atakua alijua chanzo halisi cha Mkulima Mwamwindi kumpiga risasi RC Kleruu., na ingawa mazingira yaliyomfanya atende kosa lile yalikua hayampi nafuu yoyote kisheria linapokuja suala la adhabu kwa maoni yangu hati ya kunyongwa Said Mwamwindi haikupaswa kusainiwa harakaharaka hasa ikiwa inajulikana (angalau kwa uwazi) kua Nyerere hakupenda adhabu ya kifo
Nawauliza wakongwe waliopo JF wenye kujua vizuri historia ya tukio hili na yaliyotokana na jambo hilo, haraka ya Nyerere kusaini hati ya kunyongwa hadi kufa Said Mwamwindi ilitokana na;
1. Hasira za Nyerere kuuliwa RC wake?
2. Mauwaji aliyofanya Mwamwindi yalikua ni ya kikatili kuliko wauwaji wengine walioua kwa kukusudia?
3. Chuki za Nyerere kwa aliowaita Makabaila(wamiliki wa mashamba makubwa) ambapo Mwa
mwindi anaangukia hapo?
4. Double standards wanazokua nazo wanasiasa wengi hasa wa kiafrika katika kuwatendea
watu wao?
Naomba kuelimishwa wakuu