Zitto na ushahidi wake Bungeni (Mawaziri kushawishiwa kutoa maamuzi)

MAGAMBA MATATU

JF-Expert Member
Jul 2, 2011
646
1,174
HATMA ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA) aliyelituhumu Baraza la Mawaziri kushawishiwa kubadili msimamo wa kubariki azimio la kuongeza muda wa uhai kwa Shirika Hodhi la Mali za Mashirika ya Umma (CHC) kwa miaka mitatu kinyume cha mapendekezo ya Bunge itajulikana leo.

Hatua hiyo inatokana na Spika wa Bunge, Anne Makinda, kumwagiza Zitto kuwasilisha utetezi wake hadi kufikia leo baada ya agizo lake la mara ya kwanza alilolitoa Juni 23 kumtaka mbunge huyo kuwasilisha utetezi huo hadi kufikia Juni 29 kugonga mwamba.

Hata hivyo, ulishindwa kutolewa uamuzi siku hiyo (Juni 29) baada ya siku ya kwanza ambayo Zitto alitakiwa kuthibitisha kauli yake kuwasilisha barua kwa Spika akiomba amsaidie kupata nyaraka kutoka Baraza la Mawaziri na Wizara ya Fedha zinazohusu mjadala wa CHC ambazo zitamsaidia katika utetezi wake, jambo ambalo Spika alisema alishindwa kumsaidia kwa kile alichoeleza kuwa nyaraka za Baraza la Mawaziri ni siri.

Baada ya tamko hilo la Spika bungeni kumtaka Zitto kuwasilisha utetezi wake, mbunge huyo alimzunguka na kuamua kuwasilisha utetezi wake na vielelezo Alasiri ya siku hiyo (Juni 29).

JE ATANUSURIKA NA HUO USHAHIDI WAKE LEO BUNGENI ATAKAPOKUWA ANAUSOMA MBELE YA BUNGE?
 
Kama ni kweli aliwasilisha ushahidi huo (kwa maana ya nyaraka za baraza la Mawaziri), na hata kama ushahidi wake utashindwa kuthibitisha wazi wazi tuhuma/shutuma alizotoa, jambo moja litabaki kwenye historia ya Nchi yetu kwamba "hakujapata kutokea Serikali ya kijiweni kama hii".

Nyaraka za Baraza la Mawaziri ni Siri na Mhe. Zitto anaelewa hilo, kwa kuziweka hadharani atasaidia kuanzisha mjadala kuhusu uadilifu wa baadhi ya Mawaziri na Maafisa wanaohusika na Baraza la Mawaziri, mwisho wa Siku (bila hata kujali kama tuhuma/shutuma za Mhe. Zitto zimethibitishwa au la) tutawaomba JK na Baraza lake wajiuzulu kupisha Uchaguzi Mpya.
 
Zitto ni jembe lenye makali, sina wasiwasi na ushaidi wake. Namwonea huruma spika!
 
hivi LEMA si aliwasilisha ushahidi wa uongo unaomhusu PM? mbona huyu mama kaukalia? au unamnogea?
 
Ushahidi upo. Hata mimi ninao. Tatizo litakuwa ni ushabiki wa Spika Makinda.
 
Kwleli ubongo wako na akili zinazotoka ndani ya wanachama wa ccm defects tupu. Hivi Zitto analozungumzia huoni ni kwa manufaa ya kwako na familia yako? You guys need to be thrown in a den of fire
 
Hii kitu itaishia hivi hivi tu kimya kimya, kwani Lema, Kafulila na Mwesiga si waliombwa walete ushahidi na walishapeleka lakini hatusikii chochote? Hii tabia ya kukalia vitu muhimu (kuanzia kwa Amiri Jeshi Mkuu, Waziri Mkuu, Spika mpaka viongozi wa ngazi za chini) inakipotezea chama mwelekeo kwa spidi kubwa.
 
Hata PM alitaka utajiwe kama kweli kuna mawaziri wanaishi hotelini wakati nyumba zao zilishajengwa alipotajiwa Shamsi Vuai Nahodha yeye alijbu nimekusikia ... kwisha. Hivyo hizi thibitisho wanazoomba nikuua mjadala unaondelea watu wa-"concentrate" kama uthibitisho upo au la na hoja inakua teyari imepotezewa kiaina ...
 
cdm wasikubali ushahidi wa Zito utolewe kabla ya ule wa Lema. kwa nini ule ushahidi wa Lema spika ameukalia, atoe kwanza wa halafu ndo ufuate wa Zito
 
  • Thanks
Reactions: SG8
hivi LEMA si aliwasilisha ushahidi wa uongo unaomhusu PM? mbona huyu mama kaukalia? au unamnogea?
ndugu unataka ushaidi wa lema usomwe bungeni huku pinda akiwepo?unajua madhara yake?moja,bunge halitakuwa na imani na serikali tena kwani jamaa amethibitisha kuwa pinda ni muongo.pili pinda itambidi ajiuzuru sababu kalidanganya bunge na taifa zima. Tatu pinda atazaraulika mbele ya jamii na kuonekana mtu asiye makini.utetezi wa lema ulikuwa unanguvu sana na wauhakika.
 
Ni njia iliyobuniwa na ccm kujaribu kukandamiza demokrasia bungeni,wanataka siku mtu akishindwa kuthibitisha tu wambane na aonekane ni mzushi but kwa cdm hawawezi.
 
Ni njia iliyobuniwa na ccm kujaribu kukandamiza demokrasia bungeni,wanataka siku mtu akishindwa kuthibitisha tu wambane na aonekane ni mzushi but kwa cdm hawawezi.

Mbona Godbless Lema hajapewa nafasi kudhibitisha uongo wa Pinda..
 
mambo ni yale yale tulitegemea SPIKA angemuhitaji ZITTO kuthibitisha kauli yake lakini naona muda wa maswali umepita na ZITTO hajaitwa kuthibitisha,
 
Back
Top Bottom