Zitto na ushahidi wake Bungeni (Mawaziri kushawishiwa kutoa maamuzi)

Kama Spika Makinda hatamruhusu Zitto kusoma ushahidi wake leo kwenye Bunge la Dodoma, basi Zitto asome ushahidi huo kwenye bunge la juu yaani huku mtaani kwa wananchi. Wananchi ndio wenye mamlaka na kama Makinda ameshindwa kazi aliyotumwa Zitto anatakiwa atutaarifu sisi wananchi maana ndio tuna mamlaka ya mwisho na sio Makinda. Hivyo Zitto tunategemea kutupa ushahidi kupitia njia mbalimbali, radio, tv, magezeti, JF, etc. Ni haki yetu sisi wananchi kujua nyinyi wawakilishi mnatuwakilishaje hivyo leta taarifa hapa.
 
nadhani kweli waulete humujamvini great thinkers waudadavue. aanze na Lema, Zitto na mch. Msigwa. spika ashajidhihirisha ni kimeo hawezi kuongoza bunge bila kuweka mbele maslahi ya ccm
 
naomba Waziri Mkuu kivuli adai matokeo ya ushahidi wa Lema, Zitto, Msigwa na Lissu. Huu mtindo wa kukalia majibu/matokeo ya tume za uchunguzi sasa unahamia bungeni...lazima ukomeshwe mara 1
 
Hivi wananchi wanawezaje kumuondoa Spika kama wanaona hafai? Wanasheria mnaweza kusaidi hili.

Nasema haya kwa sababu ili wananchi wawe na imani na bunge ni lazima wawe na imani kuwa wawakilishi wao wanapata nafasi ya kuwawakilisha kama sheria inavyosema. Spika Makinda badala ya kuongoza vikao vya wawakilishi wa wananchi kwenye chombo cha kutunga sheria na kuhoji serikali yeye amegeuka kuwa msemaji wa serikali, muamuzi wa nini na kwa style gani majibu yatolewe! Pamoja na kelele za muda juu ya utendaji wake mbovu Spiake Makinda ama kwa kutojua kazi na mipaka ya bunge kama mhimili wa doa au kwa makusudi ameamua kuligeuza bunge kuwa taasisi ya serikali. Imani juu ya bunge kama sehemu ya kutafuta majibu ya matatizo ya wananchi imepotea. Sasa kuna umuhimu gani kuendelea kutumia kodi zetu kumlipa huyu mama?. Wanasheria saidieni - Makinda hafai, miezi sita tu tayari amechafua kwa kiasi cha ajabu, je hadi 2015 nchi hii itakuwaje kama bunge litaendeshwa hivi? Serikali itawajibika kwa wananchi kweli?
Labda swala liko mahakamani kama la Godbless Lema...hahaha
 
dakika 2 zilizopita, bunge limeahirishwa hakuna ushahidi wa Zitto wala nini. Related story ni kwamba m'bunge mwingine wa upinzani (Ms. Sakaya, CUF) ametakiwa kuleta uthibitisho wa madai yake kwamba kutokana na ukosefu wa utawala bora kuna baadhi ya watendaji wakubwa wa serikali mfano DCs wanafanya wanachojisikia. Ni mwendo wa kupigwa mikwara kwa wabunge wa upinzani.
 
Kikao cha bunge jioni hiii kinaendelea lakini ille issue ya muheshimiwa Zito Kabwe kuwasilisha ule ushahidi wake leo Tarehe 4/07/2011 Spika Anne Makinda ameutupa kapuni! Kweli tunaye spika komandoo mwanamke.
jamani mh spika ,unavyoendesha bunge sio sawa na nina wasiwasi unawaonea wabunge wa upinzani, hii ni mara ya pili ushahidi wa mh lema dhidi ya waziri mkuu kulidanganya bunge uliukataa, ushahidi wa zitto dhidi ya baraza ka mawaziri kurubuniwa umekataa
 
nisicho elewa ni kama kuna kanuni inayozuia mbunge yale anayo changia bungeni kuyaweka hadharani ! make kama hicho kifungu hakipo
kwa nini mh Zitto nakala hajatutupia hapa jamvini ?
 
Hi imedhiririsha MAWAZIRI ni kweli walichukua RUSHWA,hii serikali ya CCM imeshindikana kabisa ni serikali ya kilaghai sasa hivi mtasikia mgawo wa umeme masaa 24.
 
Kikao cha bunge jioni hiii kinaendelea lakini ille issue ya muheshimiwa Zito Kabwe kuwasilisha ule ushahidi wake leo Tarehe 4/07/2011 Spika Anne Makinda ameutupa kapuni! Kweli tunaye spika komandoo mwanamke.

Hajautupa kapuni bana......Zitto hakuwepo bungeni leo,alikuwa jimboni kwake Kigoma ambako Rais JK alikuwa akizindua barabara so ilikuwa vigumu kwa spika kusoma utetezi/ushahidi wa Zitto ilhali yeye hayupo bungeni......

Cha msingi ni kusubiri Zitto arudi bungeni Dodoma hapo ndio zitajulikana mbivu na mbichi.....

Bala.
 
Arusha umeme a.k.a mgawo wa giza ni masaa 18 na mara nyingi unarudi saa 6 usiku na kukatika saa 12 asb.Umeme umegeuka mlinzi wa usiku!!

Hi imedhiririsha MAWAZIRI ni kweli walichukua RUSHWA,hii serikali ya CCM imeshindikana kabisa ni serikali ya kilaghai sasa hivi mtasikia mgawo wa umeme masaa 24.
 
Sasa Zitto na Lema waombe kutendewa haki .Waambie hatima ya kuombwa ushahidi na tujue nini kinaendelea baada ya ushahidi kuwa ni ukweli .Wasikubali wabanane naye .
 
kikao cha bunge jioni hiii kinaendelea lakini ille issue ya muheshimiwa zito kabwe kuwasilisha ule ushahidi wake leo tarehe 4/07/2011 spika anne makinda ameutupa kapuni! Kweli tunaye spika komandoo mwanamke.

hivi huyu mama yangu mbona anatuaibisha sana sisi wanachama ,, mbona hana msimamo??/ au tayari zitto alizipata
nyaraka alizobaniwa,, kama ndio hivi nitahama hii camp ya hawa jamaa wa kijani,
 
iLA IMESEMEKANA KUWA KIKWETE ALIKUWA KIGOMA NDO MAANA KUWA ANA MAKIND HAJARUHUSU HUO USHAHIDI KUSOMWA, KIUKWELI
LEO SIJAANGALIA BUNGE ILA KAMA KUNA MTU ALIANGALIA BUNGE LEO ATUHABALISHE ILI TUJUE KAMA KWELI ZITTO HAKUWA BUNGENI!!!
 
Vipi bado hajasoma ushahidi wake tu jamani??? mwenye kusikiliza huko naomba atujuze

mkuu nimeangalia bunge asubuhi kama nusu saa hivi ila ni bajeti ya ofisi ya rais menejimenti ya utumishi ndiyo iliyosomwa leo na nhawa ghasia cha
ajabu zaidi hakusema kama watumishi wa umma kama wataongezewa mishahara, huuu ni uhuni mtupu na hii serikali ya
KIKWETE.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom