Zitto Kabwe kugombea urais kwa tiketi ya CHADEMA endapo....

Umesomeka vizuri. Kwa mtazamo wangu ambao pengine ni finyu sana, nikisoma maoni ya wengi humu wanaopingana na Zitto's bid ni kwamba wanahofia chama chao kisisimamishe mgombea ambae ataenda kuwa Rais kivuli wa CCM. Binafsi sina ushahidi wowote kwamba Zitto anatumika na CCM lakini kama anataka kufanikisha azama yake ya kuwa Rais wa taifa letu, ni muhimu sana akaanza kazi sasahivi ya kuwaondoa mashaka watanzania juu ya hisia hizi ambazo inawezekana kabisa ni hisia potofu.

Mchambuzi,
Zitto mwenyewe ndiyo amechangia hizo hisia. Mwaka 2007 wakati wa issue ya Buzwagi, ZZK alikuwa shujaa wa vijana wengi wa kitanzania, lakini matendo yake ya karibuni yamemfanya kuwa mwanasiasa questionable.
 
Sijui na Dr. Slaa, Mnyika, Lissu, Lema, Mdee nao watangaze nia zao kama ''presidential hopefuls''?? Watu wapo buzy kuimalisha chama na mtu mwingine mmoja yupo busy akitangaza nia yake ya kugombea uraisi - bungeni, kwenye matamasha, na sasa waandishi wa habari.

Well, we all know that wale wooooooooooooote wanaoutamani uraisi, huwa hawaupati (Le big show senior, Mrema Lyatonga, Msuya etc etc). Dr. Slaa mwaka 2010 ''aliombwa'' akagombee na wala hakuanza kujipitisha pitisha akitangaza kwamba ana nia, uezo na uadilifu. Kwa nini mtu asikae kimya tuuu mpaka muda muafaka ukifika?
 
Pasco, watu wengi watakubaliana na wewe kwamba ZZK ni presidential material, LAKINI kwa jinsi anavyocheza karata zake sasa hivi ndani ya chama chake, come 2015 sidhani kama atachomoa. Amefanya kosa kubwa sana kuanza kukanyaga 'vidole' na 'vichwa' vya watu atakaotaka wamfikishe hapo atakapo kwenda, matokeo yake watamwacha aporomoke yeye mwenyewe.
Laiti ZZK angenipa nafasi ya kumshauri, ushauri wangu ungekuwa kumtaka aachane na 2015 bid, badala yake ajenge upya base na image yake ndani ya chama kwanza. 2020 onwards would work better for him.
UMK @ Nkotokwiana.
 
Kugombea sawa na Je hii mikashifa iliyomkumba Lowasa zitto ataipanguaje maana watu wanasema kachukua uchache kumlinda Mhando wa Tanesco,
 
Nilimwona wakati anagombea ubuge akisema atarudi akigombea uraisi na si ubunge tena. Kwa hiyo tangu 2010 alikuwa ameshaamua hivyo,bila hata chama chake kumpa ridhaa.
C4M iwe macho kwani dhahiri ana niya mbaya na chama..Wakati wowote anaweza kukivuruga kabla ya 2015
Nduma kuwili huyo,na inaweza kwa amepewa kazi hiyo na mafisadi.
 
Hapo kwenye mstari ni breaking News....Mkuu FJM jamaa anacheza kote kote ili kuhakikisha asikose kuambulia mafuta uzuri mnamo mwaka 2015.

Wanabodi,


Kwa vile mimi sina chama, sio mwanachama, mshabiki, wala mkereketwa wa chama chochote, kwa Chadema nitaiunga mkono bid ya ZZK!. Kwa CCM bado namshabikia sana EL asimamishwe, na kama ni kweli afya yake ni mgogoro kuhimili mikiki mikiki ya 2015, then namshabikia Membe!. .
 
Last edited by a moderator:
Update 1.

Sifa za kiongozi kwa mujibu wa mmoja wa Ma Great Thikers wakuu na wa ukweli humu JF.

ZZK ana
1.Charisma(haiba)
2. Popularity(umaarufu)
3. intellectual (weledi)
4. 'Political strategy' mkakati wa kisiasa
5. Timing
Mkuu Pasco, nadhani hukunielewa katika uzi uliotangulia. Sikusema hizo ni sifa za kiongozi. Nilichosema ni kuwa baadhi ya mambo yanayomtengeneza (au kumpa makali) mtu katika nafasi za uongozi machache ni hayo.

Hakuna anayeweza kutengeneza haiba yake kwasababu hicho ni kitu mtu anazaliwa nacho kama ilivyo gundu na hivyo haiwezi kuwa sifa ya uongozi.

Ima ukitaka kuzisoma sifa za kiongozi kwa kadri yangu nilivyoziandika basi nenda katika thread ya Mzee Mwanakijiji inayozungumzia ujana vs uzee.

Nimeona ni vema niweke kumbu kumbu vema kama nakuu yangu inavyojieleza. Si vema ukabadili maneno ya mtu kwasababu inaweza kuleta usumbufu usiokusudiwa.

Na mwisho, hakuna shida kama viongozi wote unaodhani wanaweza kutuongoza wanakidhi vigezo vya uongozi .
Muda muafaka ukifika tutawajadili kwa undani na kuangalia kila kitu kwa kina bila haya wala soni, bila kumuonea mtu au kumsamehe. JF inakumbu kumbu za kutosha tu.
Tumuombe mola atupe uzima, pengine wengine mbio zao zitaishia hapa JF! trust me!
 
Tatizo la ZZK ni kujiona yupo juu ya chama, thats why mara nyingi anaenda kinyume na misimamo ya wabunge wengine wa CDM ambayo wengi wetu tunaona ni constructive as well as kutoshiriki M4C....Ni vigumu sana kupewa ridhaa na chama kugombea uraisi wakati haushiriki ktk kukijenga.

Its not too late though, so anaweza badilika na akapewa ridhaa.
 
Mi sina shida na mtu anayeonyesha nia ya kutaka kugombea urais 3years before election day kwasababu watu wamemchoka huyu rais aliyepo madarakani
 
Zito Zuberi Kabwe umesema wewe, hayo ni mambo yako kichwani kwako usitake watu wafuate ununda wa kichwani kwako. CCM bana, kwahiyo ndivyo alivyoku2ma huyo Zana Za Kilimo
 
Mwambie huyo zito hajui ya kesho. Ni Mungu pekee ajuaye mwaka kesho kutakuwaje na mwaka 2015 utakuwaje. Anataka kujiharibia bure hata urais wa mwaka 2025 ambapo angetulia na kujiandaa taratibu angepata. anayekimbilia ikulu mwogopeni kama ukoma by Mwl Nyerere.
 
Back
Top Bottom