Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

ATHARI GANI INAELEKEA KUTOKEA KWA CCM NA KWA NCHI?

Hakika Katika Hili Hakuna Jinsi Na Wala Tusipepese Macho Wala Kutikisa Masikio Kwamba Ni Dhahiri CCM Wasipojipanga Na Kulimaliza Hili Chama Kinaweza Kupoteza Umaarufu, Wabunge Na Kikaathirika Na Kuna Hatari Pia Ya Kutokea MPASUKO Mkubwa Ambao Pia Utahatarisha Hali Ya AMANI Ya Nchi Na Kuelekea Hata Katika Machafuko Na Kuna Kila Dalili Kama Hali Hii Haitotatuliwa Serikali ITATIKISIKA Na Kuwapa Mwanya Jeshi Kuchukua USUKANI Kwa Muda.

Weee nchi hii si ya LOWASA wala MEMBE ni ya WATANZANIA. Lowasa awe gentleman kama Mh. Mwandosya akubali matokeo. Kulikuwa na wagombea 38 waliorudisha fomu na bado 33 hawajalalamika. Lowasa anataka kufanya nini na rushwa yake na Gwajima mzee wa poda na Kingunge.
Nchi hiko imara na Mh. Rais ameonyesha ukomavu wa hali ya juu na kwa tukio hili ameturejesha wengi CCM na tunamuunga mkono. Hatuwezi kuongozwa kwa mafuriko.
Yaone mateso haya tuliyo nayo ya dhuluma na ufisadi. Lazima ifike mwisho na Mungu atatusaidia. AMENI
 
Na ilikua hiviii
 

Attachments

  • 1436610727721.jpg
    1436610727721.jpg
    6.4 KB · Views: 192
Hii observation yenu ni ya kijinga kuliko zote. Kwangu mimi hakuna mtu asiejua siasa kama kikwete. Kwanza katika uongozi wa kikwete ccm ndo imepoteza majimbo mengi kuliko yote, kashfa zilizosababisha aunde upya baraza la mawaziri, ccm ipoteze mvuto mpaka yeye mwenyewe ametamka ccm inaweza kushindwa uchaguzi 2015, sasa kujua kwake siasa kuko wapi. Peleka ujinga huko


Messi na kujua kwake mpira usifikiri ukimweka Wigan basi Wigan itachukua CL..

JK hakuna anayemfikia huko CCM kwa siasa zetu za kibongo.. Na kukataliwa kwa CCM ni kwamba Watanzania tumeamka sasa na hayo si makosa ya JK bali ni Mfumo mzima wa Chama Cha Mapinduzi..

Mpeni JK credit yake, Siasa za Afrika anaziweza sana.. Huyo mgonjwa wenu sasa mkashirikiane kumuuguza Monduli kama mlivyokuwa mnakula pesa yake..
 
Ccm na utawala wao wa kifalme,Na wafalme wasiozaliwa pamoja.
Jakaya anamrisisha Membe ili amlinde na alinde kizazi chake na ukoo wote.
Membe aje kumrisisha January Makamba 2025.Naye amlinde aendelee kulinda na kizazi cha jakaya.
Makamba aje kumrisisha Rizone 2035 ili naye amlinde alinde na kizazi cha membe.
Hii ni hesabu ya haraka haraka inayoonyesha wazi Ccm wameanzisha utawala wa kifalme ndani ya Tanzania.
Tusipo ung'oa huu ufalme utaendelea kupokezana hadi kihama.Wakati ni sasa na kimbilio ni Ukawa tu.
 
Baada ya Jina la aliyekuwa akiaminiwa na watu wengi kuwa atakuja kuwa Kiongozi mzuri ndani ya chama cha mapinduzi CCM, ambayo watu wengi walianza kupoteza uaminifu haswa vijana kukatwa jina, Vijana na wasiovijana zaidi ya 10,000
wajipanga kuhamia UKAWA kutokana na utaratibu mbovu wa wanachama wa chama chicho tawala kuonekana kushindwa kufuata kanuni na taratibu za chama.
CCM go the Hell.......
Kundi hili la vijana walikuwa wameunda TEAM Lowassa, wamedai kuwa walikuwa UKAWA lakini wakahamia CCM baada ya kusikia kwamba Mhe,Lowassa anachukua Fomu.
Pia wamedai kuwa endapo lowasa atafanya maamuzi magumu na kuhamia chama chochote cha siasa,hatuna budi kuongozana naye.
Ili mradi aachane kabisa na SISIEM!!
 
Mchuma Janga hula na wa kwao. Jk kwa nini hakupeleka Jina la Lowassa kwny Kamati kuu? Amewakosea sana Ma Rais wastaafu wamwache wasimsaidie

Kwa janga hili wanalochuma CCM tunaweza kula wote tukiliangalia hili in long run, wanaweza kufanikiwa kumtuliza Lowasa kwa sasa akatulia ila October atakaposhinda Membe ndio mziki part two utakapoanza kwa sababu upinzani hawatakubali na kataa yao yaeza kua na mashiko kwa sababu Membe hana uwezo wa kuwachallenge upinzani watakaokua wamepewa nguvu na team Lowassa, na wakati huo huo CCM washazoea usultani kuachia madaraka hawatakubali ndio tutaona ya kwa jirani walipomtosa Odinga, itakapotokea hali kama hiyo hawa wenzetu wanapanda ndege na familia zao habari tutaipata wananchi wa kawaida.. naunga mkono mkuu getamycine alichosema either wamkate na Membe au wamrudishe Lowassa ili kuua hizi team na kurudisha umoja wa chama.
 
Last edited by a moderator:
JUMA nKAMIA...

Majina matano wote ni wana CCM wazuri na lengo ni chama kushinda...

Waliotoka wametoka kwa sababu zao wanajua wenyewe, chama kimefata utaratibu mzuri...!!

Kuhusu upinzani anasema ni two way traffic...

Kuna Mbunge wa viti maalumu amekasirika sana anasema hata hayo majina waliotanganza hayajui ila watajua kwenye kikao...
 
Tv channels hizo hususan TBC1 mlituahidi tangu jana kuwa mtakuwa live kwenye vikao vya nec na mkutano mkuu cha ajabu tumekaa karibu na tv lakin mpaka sasa hakuna chochote na hamjatuomba msamaha watazamaji wenu kunani? kwa upande wa star kuna mida walitaka kutuunganisha na kikao cha nec lakini nao ikashindikana. tafadhalini tujuzen kimetokea nini maana siamin kama ni hitilafu ya mawasiliano.
 
Zungu anasema hajasikia jina lolote anatajiwa na mwandishi wa habari anasema hiyo si taarifa rasmi ya chama...
 
Kila nikifatilia humu naona jamaa wa Laigwanani wanatokwa povu ckwakumpenda Jamaa ila nivile MKONO uliokuwa unawalisha umekatika
 
Back
Top Bottom