Women...........!

wanamme wenyewe wakwapi???

Hawa tunaogombea nao mabwana???

Una utani
 
Mwanamke hana manufaa zaidi ya usaidizi ee?

Sasa mbona hayo majukumu mengine unataka ayafanye yeye yote na sio kama msaidizi?
 
sijasema mwanaume kutotimiza wajibu wake kwa familia,nasema mwanamke atimize wajibu wake na mwanaume atimize wajibu wake,sio kunilazimisha nikufanyie majukumu yako kwa sababu ya kudai haki/usawa.

Ndio maana nikakueleza nidhamu hujengwa, mwanamke akikupelekapeleka it means wewe ni dhaifu you can't handle your affairs period!
 
mke alikua msaidizi, msaidizi sio hausigeli aka beki tatu... usaidizi upo kwenye naniliu banaaa



unaoa ili upate mpishi na dobi?
kupika na kufua n.k mwanamke anafanya kwa mapenzi, mapenzi aliyonayo juu ya mumewe, kupika kufua kuosha vyombo sio jukumu la mwanamke pekee...ukiona ndoa imara ujue wanandoa wameoana kwa sababu wanapendana na wanashirikiana na si kuoana ili kufuliana na kupikiana.........




ruksa kwa wanaume kunywa ila mwanamke hairuhusiwi?
kuna ubaya gani mume ukaamua kumkarangizia mkeo?
huoni inakuwa romantic?
ndoa ni vile mnavyoijenga, je unamwonaje mwenzi wako? mke/ubavu au dobi/mpishi?
au ndo aina ya mwanaume hata mtoto akilia unamuita mkeo aje ambembeleze?
hiyo nyumba mke anatoa maoni yake au akitoa maoni ndo inakuwa anataka haki?
afterall haki kumbe inatafutwa kwa kupangiana zamu za kupika?

kunanihiiii sio usaidizi,hiyo ni haki ya wanandoa.
 
huko sasa itakuwa ni ile ishu ya kuwatunza ma mariooo,hapa nazungumzia for a responsible women and men,kumnunulia mmeo gari ni kama zawadi tuu strong lady na hivyo haikuondeshei wewe majukumu yako ya msingi kwa mwanaume.

majukumu ya familia ni kusaidiana jamani, hebu fikiria wote mnafanya kazi,mnarudi home late mkifika mwanaume unakaa tu kwenye kochi umeshikilia rimoti, mwanamke aandae chakuka,ule aoshe vyombo na bado utahitaji na kile chakula cha ndoa, hee ist possible? majukumu ya familia ni ya wote jamani tusifanye ndoa iwe burden kwa upande wa mwanamke tu.
 
Kuna jamaa yangu amekamuliwa mahari milioni moja na laki mbili za Tshs. Unadhani hii kitu haina bearing na namna hawa waoanaji watakuwa wakihusiana???
 
Kwangu mwanaume yeyote anayeshindwa kuya handle majukumu yake ipasavyo na kuja kuishia kulalama hapa ni wazi ana matatizo.
Kila kitu kimeundwa/umbwa so kama ukiwa mwanaume kweli usitegemee out of the blue mwanamke afanye vile utakavyo. Ndoa na familia pamoja na muundo wake hujengwa. Mwanaume ukiwa kichwa cha familia na kutimiza majukumu yako sidhani kama mkeo atapata nafasi ya kukupanda kichwani. Nadhani hapa unazungumzia zaidi ya kuosha vyombo, unazungumzia zaidi mamlaka ya mwanaume kutotambulika. Usipojenga heshima kwa mkeo atakuheshimu kweli?
Mimi napenda Mume wangu awe na mamlaka na mwenye kuwajibika...mamlaka hayo kwa maana ya kumanage wajibu wake vyema sio mamlaka ya ku abuse

Si tu kwamba ana matatizo bali si mwanaume kabisa, avalishwe baibui na kanga.
 
yan hiyo new edition ni poa ile mbaya,wakitaka tufanye hayo warudi kwenye majukumu yao
 
kama ambavyo imeandikwa mwanamke ni msidizi wa mwanaume,so ni jukumu lako wewe kuhakikisha mumeo anakula vizuri na anakuwa msafi,lakini pia kumsaidia kwenye bills kama unauwezo.

hapo kwenye red: siku zote mkuu ndio kila kitu na msaidizi anakuwa msaidizi tu, kwa hio kila mtu afanye jukumu lake, lini uliona Kikwete anamwachia Bilali kuapisha viongozi? Au naibu waziri anawajibika kwa kazi ya waziri?
 
Miaka mingi iliyopita iliukuwa ni miaka yenye ufahari juu ya mwanamke,mwanamke alikuwa mwanamke kwelikweli,ni kweli alikuwa MSAIDIZI WA MWANAUME,kwa hali hiyo tulijivunia sana hawa wakina dada zetu na mama zetu.Waliwapikia waume zao,waliwafulia na mengineyo mengi.Lakini siku hizi mambo yamebadilika;wanawake wanataka haki,wanataka kuwa sawa na wanaume,hawapiki tena na wala hawawafulii tena waume zao,wanachotaka waoni HAKI SAWA,eti mwanamke akipika mchana basi mwanaume apike usiku,kulea watoto eti pia iwe zamu.MIAKA HIYO WAKINA DADA WALIPIKA KAMA MAMA ZAO LAKINI SIKU HIZI WANAKUNYWA KAMA BABA ZAO,DUUUUUUU.Je usaw huu unaopiganiwa na wanawake ni sawa?nini faida zake na hasara zake?

Mara nyingi issue hizi huwakuta wale wanaokataa kutafutiwa wenza wao (wake zao) na wazazi wao
 
mhhhhh.....kwahiyo baba akiwa njiani anrudi kutoka kazini anafikiria kuwa akifika nyumbani anazamu ya kupika,kuosha vyombo na kufua,kwangu mimi nasema moja ya vitu vinavyoleta matatizo katika ni mwanamke kufanya kazi hali inayopelekea kutotumiza wajibu wake kwa mwanaume.

ukiona mpaka inafikia hatua ya mkeo kukupangia zamu ya kufanya shughuli za nyumbani ujue kabisa wewe sio mwanaume imara tena ni DHAIFU haswa! Mimi ninachozungumzia ni wanandoa kusaidiana kwa mapenzi yao bila kupangiana, mfn. mume akijisikia kupika weekend hakuna ubaya ni mahaba hayo..
Hiyo ya kutaka wanawake wasifanye kazi ni mtazamo duni sana cause wapo wanaofanya kazi na wanatimiza majukumu yao vizuri, elimu imemkomboa mwanamke kutoka kwenye unyanyasaji uliokua unafanywa zamani, kwa dunia ya sasa huwezi kuzuia m/mke asifanye kazi cha msingi kama unataka kuoa ambae hafanyi kazi(tegemezi) tafuta wamejaa tele!
 
Siku mtakapoacha kudai 50/50 sharing of bills na ndio sio siku tutafikiria kuwapikia 3 x a day na kuwafulia.

Asante MadameX, ujue ni hulka ya mwanadamu kuyaona mapungufu ya mwenzie bila kutafakari anachangiaje ktk madhaifu hayo?
 
Last edited by a moderator:
majukumu ya familia ni kusaidiana jamani, hebu fikiria wote mnafanya kazi,mnarudi home late mkifika mwanaume unakaa tu kwenye kochi umeshikilia rimoti, mwanamke aandae chakuka,ule aoshe vyombo na bado utahitaji na kile chakula cha ndoa, hee ist possible? majukumu ya familia ni ya wote jamani tusifanye ndoa iwe burden kwa upande wa mwanamke tu.

kwani wakati nakuoa nilikwambia nakuoa kwa ajili ya chakula cha usiku tuu,hujui kuwa wengine wanaoa ili wafuliwe,wapikiwe sasa ukianza kumwambia ayafanye hayo utakuwa unamkosea.
 
Tatizo hapo ndugu zangu ni kuwa kuna dadas wamelelewa na upande mmoja tu wa mzazi,hapa niseme mama,na kama hajawahi kumuona mama yake akiwajibika kwa baba yake hatakuwa na cha kujifunza na hivyo ni vigumu kuwa mkamilifu katika ndoa,pamoja na kuwa si wote,hivyo pia kwa sisi wanaume kama baba hakuwa familly man ni ngumu pia kwa baadhi yetu kuwajibika ipasavyo kwa familia zetu,labda kama umekwenda shule na umetembea kidogo.Kingine ni utandawazi mambo ya haki sawa,kama ni kazi tunafanya wote na tukirudi home wote tumechoka hivyo ngoma droo.Hii pia inachangia sana kwa divorce nyingi asubuhi ndoa mchana wameachana.TAFAKARI CHUKUA HATUA.
 
majukumu ya familia ni kusaidiana jamani, hebu fikiria wote mnafanya kazi,mnarudi home late mkifika mwanaume unakaa tu kwenye kochi umeshikilia rimoti, mwanamke aandae chakuka,ule aoshe vyombo na bado utahitaji na kile chakula cha ndoa, hee ist possible? majukumu ya familia ni ya wote jamani tusifanye ndoa iwe burden kwa upande wa mwanamke tu.

Pokea like zangu ma dia
 
Back
Top Bottom