Women...........!

Miaka mingi iliyopita iliukuwa ni miaka yenye ufahari juu ya mwanamke,mwanamke alikuwa mwanamke kwelikweli,ni kweli alikuwa MSAIDIZI WA MWANAUME,kwa hali hiyo tulijivunia sana hawa wakina dada zetu na mama zetu.Waliwapikia waume zao,waliwafulia na mengineyo mengi.Lakini siku hizi mambo yamebadilika;wanawake wanataka haki,wanataka kuwa sawa na wanaume,hawapiki tena na wala hawawafulii tena waume zao,wanachotaka waoni HAKI SAWA,eti mwanamke akipika mchana basi mwanaume apike usiku,kulea watoto eti pia iwe zamu.MIAKA HIYO WAKINA DADA WALIPIKA KAMA MAMA ZAO LAKINI SIKU HIZI WANAKUNYWA KAMA BABA ZAO,DUUUUUUU.Je usaw huu unaopiganiwa na wanawake ni sawa?nini faida zake na hasara zake?

my dear instead of kulalama na kuanza kwenda history za kale tugange yajayo, mi kijana wangu namfundisha kupika na kazi na kumwambia ukweli dunia imebadilika kuliko kumdanganya ajione kidume kumbe wanawake wenyewe siku hizi ndio hao kama wanaume tu. tuwaambie vijana wetu ukweli kuwa dunia imebadilika na itaendelea na kuzidi kubadilika mambo ya karne zilizopita hayapo tena, we hata angalia familia za sasa zinavyolea watoto wao utachoka binti anakua msichana hata chai hajui kupika loohh!!!!!
 
Miaka mingi iliyopita iliukuwa ni miaka yenye ufahari juu ya mwanamke,mwanamke alikuwa mwanamke kwelikweli,ni kweli alikuwa MSAIDIZI WA MWANAUME,kwa hali hiyo tulijivunia sana hawa wakina dada zetu na mama zetu.Waliwapikia waume zao,waliwafulia na mengineyo mengi.Lakini siku hizi mambo yamebadilika;wanawake wanataka haki,wanataka kuwa sawa na wanaume,hawapiki tena na wala hawawafulii tena waume zao,wanachotaka waoni HAKI SAWA,eti mwanamke akipika mchana basi mwanaume apike usiku,kulea watoto eti pia iwe zamu.MIAKA HIYO WAKINA DADA WALIPIKA KAMA MAMA ZAO LAKINI SIKU HIZI WANAKUNYWA KAMA BABA ZAO,DUUUUUUU.Je usaw huu unaopiganiwa na wanawake ni sawa?nini faida zake na hasara zake?

habari ndio hiyo. ukitaka kufanyiwa kazi zote lete matumizi by 100% kama uwezi na wewe kubali kuwajibika.
 
nashukuru kwa kuedit,ila mbona mnaipa kipaumbele sana gari?ukimnunulia gari si kama zawadi as vile unaweza mnunulia boxer,so majukumu ya mwanaume yatabakia kuwa majukumu ya mwanaume n mwanamke atabakia na majukumu yake.

Asante. Mimi sijaipa kipaumbele gari, labda kama kuna wengine wamefanya hivyo. Hapo nilikuwa naweka msisitizo suala la mwanamume kupenda kulelewa. Nimekuelewa.
 
my dear instead of kulalama na kuanza kwenda history za kale tugange yajayo, mi kijana wangu namfundisha kupika na kazi na kumwambia ukweli dunia imebadilika kuliko kumdanganya ajione kidume kumbe wanawake wenyewe siku hizi ndio hao kama wanaume tu. tuwaambie vijana wetu ukweli kuwa dunia imebadilika na itaendelea na kuzidi kubadilika mambo ya karne zilizopita hayapo tena, we hata angalia familia za sasa zinavyolea watoto wao utachoka binti anakua msichana hata chai hajui kupika loohh!!!!!

kumfundisha kazi si vibaya kwasababu si kwamba akianza kujitegemea ataoa moja kwa moja,wanawake wamebadilika kutokana na mambo mbalimbali ikiwamo harakati mbalimbali za kutafuta usawa na mwanaume,haya ndio yanayopelekea wao kutaka kila kitu wawe sawa na mwanaume.
 
unaweza kuniambia mwanamke anabagulia katika lipi?unazumngumziaje hizi harakati zenu za kutaka hadi baba ampeleke mtoto kliniki?
FYI this is a male poster. kama mke wangu kachoka au kazidiwa kazi sioni shida kumpeleka blaine junior clinic. Sikujieleza vizuri mwanzoni, nilitaka kusema wanawake hawaheshimiki sehemu nyingi hasa vijijini, ona jinsi wasichana wanavyoozwa wakiwa wadogo, vipigo nk. wanawake wanataka hali hii iishe, mimi siongeleii zamu za kupika/kufua/kuosha vyombo nk
 
Siku hizi wanawake wote kama wajawazito na vitambi vinachomoka kabinti kadogo kana kitambi cha viazi
 
FYI this is a male poster. kama mke wangu kachoka au kazidiwa kazi sioni shida kumpeleka blaine junior clinic. Sikujieleza vizuri mwanzoni, nilitaka kusema wanawake hawaheshimiki sehemu nyingi hasa vijijini, ona jinsi wasichana wanavyoozwa wakiwa wadogo, vipigo nk. wanawake wanataka hali hii iishe, mimi siongeleii zamu za kupika/kufua/kuosha vyombo nk

kaka kupigwa na kunyanyaswa ni tofauti na utekelezaji wa majukumu ya mwanamke,ninachochesema hapa ni pale mwanamke anapodai afanyiwe kazi na mwananume ambazo alipaswa kufanya yeye mwenyewe,kumpiga mwanamke sio ishu.
 
We una bahati mbaya.. Wapo bado japo ni 2% lakini watalipa bills na bado watakutunza na kukushuhulikia vizuri.. Tatizo wanawake saivi wamesoma na wana kazi so hawaelezwi wala kuambiwa hasa hawa wa mjini
 
kama ambavyo imeandikwa mwanamke ni msidizi wa mwanaume,so ni jukumu lako wewe kuhakikisha mumeo anakula vizuri na anakuwa msafi,lakini pia kumsaidia kwenye bills kama unauwezo.
kama unaona ni halali mimi kusaidia kulipa bills kama nina uwezo unashangaa nini wewe kunisaidia kuosha vyombo kama upo home? mbona wakaka mnajipenda sana?
mimi sisemei ile dada ameshinda nyumbani na bado analazimisha mumewe kuja kumsaidia kufua au kupika, lakini kama wote tumetoka kazini na wote tumechoka kuna shida gani wewe ukasonga ugali na mimi nikapika mboga tukala tukapumzika?
 
Kwangu mwanaume yeyote anayeshindwa kuya handle majukumu yake ipasavyo na kuja kuishia kulalama hapa ni wazi ana matatizo.
Kila kitu kimeundwa/umbwa so kama ukiwa mwanaume kweli usitegemee out of the blue mwanamke afanye vile utakavyo. Ndoa na familia pamoja na muundo wake hujengwa. Mwanaume ukiwa kichwa cha familia na kutimiza majukumu yako sidhani kama mkeo atapata nafasi ya kukupanda kichwani. Nadhani hapa unazungumzia zaidi ya kuosha vyombo, unazungumzia zaidi mamlaka ya mwanaume kutotambulika. Usipojenga heshima kwa mkeo atakuheshimu kweli?
Mimi napenda Mume wangu awe na mamlaka na mwenye kuwajibika...mamlaka hayo kwa maana ya kumanage wajibu wake vyema sio mamlaka ya ku abuse
 
kaka kupigwa na kunyanyaswa ni tofauti na utekelezaji wa majukumu ya mwanamke,ninachochesema hapa ni pale mwanamke anapodai afanyiwe kazi na mwananume ambazo alipaswa kufanya yeye mwenyewe,kumpiga mwanamke sio ishu.
kama mkeo anakusaidia majukumu yako kwa nini wewe usimsaidie yake?? mke karudi saa 12 unataka aanze kupepeta mchele wakati wewe umetulia kwenye TV, wachache wataokubali hicho unachotaka. mke akiomba umsaidie kitu reasonable fanya hivyo.
 
kama mkeo anakusaidia majukumu yako kwa nini wewe usimsaidie yake?? mke karudi saa 12 unataka aanze kupepeta mchele wakati wewe umetulia kwenye TV, wachache wataokubali hicho unachotaka. mke akiomba umsaidie kitu reasonable fanya hivyo.

hayo niyafanye mwenyewe nikiongozwa na busara zangu lakini sio yeye afanye hiyo kama ndio wajibu wangu,abadani haitawezekana.
 
Kwangu mwanaume yeyote anayeshindwa kuya handle majukumu yake ipasavyo na kuja kuishia kulalama hapa ni wazi ana matatizo.
Kila kitu kimeundwa/umbwa so kama ukiwa mwanaume kweli usitegemee out of the blue mwanamke afanye vile utakavyo. Ndoa na familia pamoja na muundo wake hujengwa. Mwanaume ukiwa kichwa cha familia na kutimiza majukumu yako sidhani kama mkeo atapata nafasi ya kukupanda kichwani. Nadhani hapa unazungumzia zaidi ya kuosha vyombo, unazungumzia zaidi mamlaka ya mwanaume kutotambulika. Usipojenga heshima kwa mkeo atakuheshimu kweli?
Mimi napenda Mume wangu awe na mamlaka na mwenye kuwajibika...mamlaka hayo kwa maana ya kumanage wajibu wake vyema sio mamlaka ya ku abuse

sijasema mwanaume kutotimiza wajibu wake kwa familia,nasema mwanamke atimize wajibu wake na mwanaume atimize wajibu wake,sio kunilazimisha nikufanyie majukumu yako kwa sababu ya kudai haki/usawa.
 
Miaka mingi iliyopita iliukuwa ni miaka yenye ufahari juu ya mwanamke,mwanamke alikuwa mwanamke kwelikweli,ni kweli alikuwa MSAIDIZI WA MWANAUME,kwa hali hiyo tulijivunia sana hawa wakina dada zetu na mama zetu.

mke alikua msaidizi, msaidizi sio hausigeli aka beki tatu... usaidizi upo kwenye naniliu banaaa

Waliwapikia waume zao,waliwafulia na mengineyo mengi.Lakini siku hizi mambo yamebadilika;wanawake wanataka haki,wanataka kuwa sawa na wanaume,hawapiki tena na wala hawawafulii tena waume zao,

unaoa ili upate mpishi na dobi?
kupika na kufua n.k mwanamke anafanya kwa mapenzi, mapenzi aliyonayo juu ya mumewe, kupika kufua kuosha vyombo sio jukumu la mwanamke pekee...ukiona ndoa imara ujue wanandoa wameoana kwa sababu wanapendana na wanashirikiana na si kuoana ili kufuliana na kupikiana.........


wanachotaka waoni HAKI SAWA,eti mwanamke akipika mchana basi mwanaume apike usiku,kulea watoto eti pia iwe zamu.MIAKA HIYO WAKINA DADA WALIPIKA KAMA MAMA ZAO LAKINI SIKU HIZI WANAKUNYWA KAMA BABA ZAO,DUUUUUUU.Je usaw huu unaopiganiwa na wanawake ni sawa?nini faida zake na hasara zake?

ruksa kwa wanaume kunywa ila mwanamke hairuhusiwi?
kuna ubaya gani mume ukaamua kumkarangizia mkeo?
huoni inakuwa romantic?
ndoa ni vile mnavyoijenga, je unamwonaje mwenzi wako? mke/ubavu au dobi/mpishi?
au ndo aina ya mwanaume hata mtoto akilia unamuita mkeo aje ambembeleze?
hiyo nyumba mke anatoa maoni yake au akitoa maoni ndo inakuwa anataka haki?
afterall haki kumbe inatafutwa kwa kupangiana zamu za kupika?
 
kama ambavyo imeandikwa mwanamke ni msidizi wa mwanaume,so ni jukumu lako wewe kuhakikisha mumeo anakula vizuri na anakuwa msafi,lakini pia kumsaidia kwenye bills kama unauwezo.

Usaidizi si manake, unitumikishe. Ni kukusaidia tu. Sasa nyie mmegeuza kuwa ni wajibu wa ke.
 
Wakati Adamu na Hawa wanatimuliwa Edeni Mungu alimwambia Eva utazaa kwa Uchungu na Adamu utakula kwa jasho. Kwa maana hii ke kazi yake ni kuzaa tu na me kufanya kazi zote. Mmepotosha maana ya Mungu na kuleta ubinafsi wenu, maudhi yenu, masimango yenu ndo yametufanya tujitetee.
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Back
Top Bottom