passion_amo1
JF-Expert Member
- Dec 3, 2023
- 1,578
- 3,148
Wakuu habari za uzima?
Leo nataka niongee na baadhi ya wanaume wenzangu wanaongelea sana maovu ya wanawake na kuyaacha ya kwao kana kwamba sisi wanaume hatukosei kwenye jamii wakati maovu yote yanayofanywa na wanawake ni sawa tu na maovu yote yanayofanywa na wanaume.
Wapo wengine watasema ati wanaongelea maovu ya wanawake kwa sababu wanawake ndiyo wanapata madhara zaidi kuliko wanaume, wao linapokuja suala la mahusiano hawana cha kupoteza kabisa ila niwaambie tu kuwa hiyo siyo sababu ya wanaume kufanya maovu wanavyojisikia ati ili kuwakomoa wanawake. sasa mbona magonjwa ya zinaa hayaangalii jinsia na yanaua kwa mtindo ule ule?.
Kama hatuna cha kupoteza kwenye mapenzi Kwanini sisi ndio tunaongoza kushinda kwenye mitandao kulalamika kuwaongelea wanawake? Ati tunafanya kwa lengo la kuwasaidia hao wanawake wenye hayo maovu, Kwanini muishie kuongea kwa mdomo si kufanya vitendo?
Unakuta mwanaume anasema “kuna demu nimemtongoza Jana akakubali, muda ule ule na mzigo akanipa siku ile ile” Halafu anamalizia kwa kusema “daah wanawake wa siku hizi wanajirahisisha sana acheni umalaya la sivyo wanawume tutaendelea kuchapa na kusepa”sasa mwanaume kama huyu ni mnafki yaani anajifanya kusikitishwa na wimbi la la wadada kujirahisisha wakati huo huo yeye ndio kinara wa kutongoza kama kweli ana nia na hapendi wanawake kujirahisisha Kwanini asiache kutongoza na kuwaomba mzigo?
Kama baadhi ya wanaume wana nia ya kuwasaidia wanawake na mmeona maneno hayasaidii Kwanini msifanye vitendo kwa kuacha kuyafanya mambo yanayowafanya wanawake wajirahisishe??
Halafu wanaume wengi utasikia “Kwanini mwanamke ukitongozwa ukubali” badala ya kuuliza “ Kwanini mwanaume anatongoza pasipo kuwa na nia ya dhati?
Yaani tunalazimisha ionekane kama mwanaume kutongoza si kosa ila mwanamke kukubali ni kosa. Wakati kinachoanza ni kutongoza Halafu kinafata kukubali au kukataa,
Mwanaume anayetongoza na mwanamke anayekubali wote wana makosa.
Kama kila jinsia imeshindwa kubadilika kwa nafasi yake na kusubiria Ati jinsia nyingine ianze kubadilika hapo tutakuwa tunasubiri meli kwenye uwanja wa ndege
Ninyi endeleeni kupiga na kusepa tuone mwisho wake, kama sio kuongeza vibarua viwandani, magenge ya uhalifu, na mambo ambayo kwa kizazi kwa taifa lijalo hayana ustawi .
FROM: instagram.
Leo nataka niongee na baadhi ya wanaume wenzangu wanaongelea sana maovu ya wanawake na kuyaacha ya kwao kana kwamba sisi wanaume hatukosei kwenye jamii wakati maovu yote yanayofanywa na wanawake ni sawa tu na maovu yote yanayofanywa na wanaume.
- Wanawake wanaochepuka wanaenda sambamba na wanaume wanaochepuka.
- Wanawake wanaozalishwa bila ndoa/nje ya ndoa wanaenda sambamba na wanaume wanaozalisha bila/nje ya ndoa.
- Wanawake wasagaji wanaendana na wanaume wasagaji
- Wanawake wanaopenda kutembea na waume za watu wanaendana na wanaume wanaopenda tembea na wake za watu.
- Wanawake wanopenda kutembea na mijibaba wanaendana na wanaume wanaopenda kutembea na mijimama.
- Wanawake waliopo kwenye mahusiano sababu ya pesa wanaendana na wanaume waliopo kwenye mahusiano sababu ya ya mbunye.
- Wanawake wanaopenda kuhudumiwa kwenye mahusiano wanaendana na wanaume vinga’sti wanaopenda kulelewa.
- Wanawake wanaowaacha wanaume waliowasomesha wanaendana na wanaume wanaowaaacha wanawake walioanza nao kwenye umaskini.
- Wanawake wasio watu kwa waume zao wanaendana na wanaume wasio na upendo kwa wake zao.
Wapo wengine watasema ati wanaongelea maovu ya wanawake kwa sababu wanawake ndiyo wanapata madhara zaidi kuliko wanaume, wao linapokuja suala la mahusiano hawana cha kupoteza kabisa ila niwaambie tu kuwa hiyo siyo sababu ya wanaume kufanya maovu wanavyojisikia ati ili kuwakomoa wanawake. sasa mbona magonjwa ya zinaa hayaangalii jinsia na yanaua kwa mtindo ule ule?.
Kama hatuna cha kupoteza kwenye mapenzi Kwanini sisi ndio tunaongoza kushinda kwenye mitandao kulalamika kuwaongelea wanawake? Ati tunafanya kwa lengo la kuwasaidia hao wanawake wenye hayo maovu, Kwanini muishie kuongea kwa mdomo si kufanya vitendo?
Unakuta mwanaume anasema “kuna demu nimemtongoza Jana akakubali, muda ule ule na mzigo akanipa siku ile ile” Halafu anamalizia kwa kusema “daah wanawake wa siku hizi wanajirahisisha sana acheni umalaya la sivyo wanawume tutaendelea kuchapa na kusepa”sasa mwanaume kama huyu ni mnafki yaani anajifanya kusikitishwa na wimbi la la wadada kujirahisisha wakati huo huo yeye ndio kinara wa kutongoza kama kweli ana nia na hapendi wanawake kujirahisisha Kwanini asiache kutongoza na kuwaomba mzigo?
Kama baadhi ya wanaume wana nia ya kuwasaidia wanawake na mmeona maneno hayasaidii Kwanini msifanye vitendo kwa kuacha kuyafanya mambo yanayowafanya wanawake wajirahisishe??
Halafu wanaume wengi utasikia “Kwanini mwanamke ukitongozwa ukubali” badala ya kuuliza “ Kwanini mwanaume anatongoza pasipo kuwa na nia ya dhati?
Yaani tunalazimisha ionekane kama mwanaume kutongoza si kosa ila mwanamke kukubali ni kosa. Wakati kinachoanza ni kutongoza Halafu kinafata kukubali au kukataa,
Mwanaume anayetongoza na mwanamke anayekubali wote wana makosa.
Kama kila jinsia imeshindwa kubadilika kwa nafasi yake na kusubiria Ati jinsia nyingine ianze kubadilika hapo tutakuwa tunasubiri meli kwenye uwanja wa ndege
Ninyi endeleeni kupiga na kusepa tuone mwisho wake, kama sio kuongeza vibarua viwandani, magenge ya uhalifu, na mambo ambayo kwa kizazi kwa taifa lijalo hayana ustawi .
FROM: instagram.