DOKEZO Wizara ya Afya, Je, kuna mlipuko wa ugonjwa wa macho?

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Ozone_

Member
Dec 30, 2023
88
106
Habari za muda tena, heri ya siku ya mapinduzi.

Moja kwa moja kwenye mada, jana nikiwa katika harakati za kutafuta mkate wa siku muda wa saa 4 asubuhi nilianza kuhisi maumivu jicho la kulia kadri muda ukivyozidi kwenda hali ilizidi kuwa mbaya nikaona hata isiwe shida acha nijipumzishe na kazi nielekee home kwa ajili ya matibabu.

Sasa nikiwa narudi home kutoka Makumbusho nikaona sio mbaya nipite Zahanati japo kupata dawa. Muda huo nipo maeneo ya UDSM hapo, nikashuka kwenye gari na kuingia Zahanati ya chuo. Nikiwa katika benchi la kusubiri matibabu nikaona kama watu wawili wakiwa wamevimba macho mmoja alivimba yote, hata haikunishtua.

Ikafika zamu yangu nikaingia kwa Daktari nilipofika tu baada ya kumkabidhi fomu ya NHIF akaanza kuandika dawa then akaniuliza kuna kingine tofauti na macho ikabidi nijibu hapana. Akasema nenda Duka la Daw kachukue dawa.

Nimefika Duka la Dawa nikapewa dawa kilichonishangaza zaidi nikaona ile meza ya pale dirishani kumejaa dawa za macho tu. Akili ikanambia acha kufatilia mambo yasiokuhusu. Nikachukua zangu dawa chaap nikaelekea home kupumzika.

Nimefika home mida ya saa 12 jioni mara kidogo namuona jamaa yangu nae amerudi analalamika jicho linauma nikwambia hata mimi linazingua sema nenda hospital ukapate dawa.

Jamaa akanambia shida ni nini mbona familia ya Mzee fulani watu zaidi ya watatu nao wanashida hiyo hiyo.

Sasa ombi langu kwa Wizara kama kuna shida tupeane taarifa tusisubiri ugonjwa uenee sehemu kubwa pia Wanajamii waelekezwe namna ya kujikinga na maambukizi hayo.

Naomba kuwasilisha
 
Mm mwenyew tangu jana macho yanawasha na yote nimekundu yameanza kuvimba kama Kuna ka mlipuko hvi tupewe taarifa, nmetumia dawa Lakin bado sijapata nafuu yan machoz yanamwagika tu nanimekundu yanawasha
 
Mm mwenyew tangu jana macho yanawasha na yote nimekundu yameanza kuvimba kama Kuna ka mlipuko hvi tupewe taarifa, nmetumia dawa Lakin bado sijapata nafuu yan machoz yanamwagika tu nanimekundu yanawasha
Unapatikan maeneo gani mkuu
 
Unapatikan maeneo gani mkuu
Asante kwa taarifa unacho kisema ni kweli. Na sasa sio muwasho ule wa kawaida ni kana kwamba umeingiliwa na mdudu wale wa barabarani. Imenitokea sijatumia dawa hiyo ilikuwa jana mida ya saa mbili usiku. Leo asubuhi nimetumia kujifuta na kitambaa safi chenye maji ya vuguvugu sijasumbuliwa mpaka sasa hivi.(sipo dar.)
 
Haabri za mda tena, heri ya siku ya mapinduzi.

Moja kwa moja kwenye mada, jana nikiwa katika harakati za kutafta mkate wa siku mida ya saa 4 asubuhi nianza kuhisi maumivu jicho la kulia kadri mda ukivyozidi kwenda hali ilizidi kuwa mbaya nikaona taha isiwe shida acha nijipumzishe na kazi nielekee home kwa ajili ya matibabu.

Sasa nikiwa narudi home kutoka makumbusho nikaona sio mbaya nipite zahanati japo kupata dawa. Mda huo nipo maeneo ya udsm hapo, nikashuka kwenye gari na kuingia zahanati ya chuo. Nikiwa katika benchi la kusubiri matibabu nikaona kama watu wawili wakiwa wamevimba macho mmoja alivimba yote, hata haikunishtua. Ikafika zamu yangu nikaingia kwa daktari nilipofika tu baada ya kumkabidhi fomu ya nhif akaanza kuandika dawa then akaniuliza kuna kingine tofauti na macho ikabidi nijibu hapana. Aksema nenda famasi kachukue dawa.

Nimefika famasi nikapewa dawa kilichonishangaza zaidi nikaona ile meza ya pale dirishani kumejaa dawa za macho tu. Akili ikanambia acha kufatilia mambo yasiokuhusu. Nikachukua zangu dawa chaap nikaelekea home kupumzika.

Nimefika home mida ya saa 12 jioni mara kidogo namuona jamaa yqngu nae amerudi analalamika jicho linauma nikwambia hata mimi linazingua sema nenda hospital ukapate dawa. Jamaa akanambia shida ni nini mbona familia ya mtee fulani watu zaidi ya watatu nao wanashida hiyo hiyo.


Sasa ombi langu kwa wizara kama kuna shida tupeane taarifa tusisubiri ugonjwa uenee sehem kubwa pia wanajamii waelekezwe namna ya kujikinga na maambukizi hayo.


Naomba kuwasilisha
Duuuh kuna na watoto wa rafiki zangu wawili nao wanaumwa macho yaani red eyes
 
Asante kwa taarifa unacho kisema ni kweli. Na sasa sio muwasho ule wa kawaida ni kana kwamba umeingiliwa na mdudu wale wa barabarani. Imenitokea sijatumia dawa hiyo ilikuwa jana mida ya saa mbili usiku. Leo asubuhi nimetumia kujifuta na kitambaa safi chenye maji ya vuguvugu sijasumbuliwa mpaka sasa hivi.(sipo dar.)
Mm pia nilipata shida kama hii nikajua itapotea yenyewe ila usumbufu ukazid aisee...nlienda CCBRT nikapewa eye drops nikawa sawa..ni dec mwanzoni lakn mm
 
Nyie nawe, nendeni mkanawie maji ya baharini itakuwa mnaumwa Nairobi red eyes.Huu ugonjwa huwa unakuja na kuondoka.Si mara ya kwanza. Na mgonjwa anapona vizuri tu,sema ni rahisi sana kuambukizana.
 
Haabri za mda tena, heri ya siku ya mapinduzi.

Moja kwa moja kwenye mada, jana nikiwa katika harakati za kutafta mkate wa siku mida ya saa 4 asubuhi nianza kuhisi maumivu jicho la kulia kadri mda ukivyozidi kwenda hali ilizidi kuwa mbaya nikaona taha isiwe shida acha nijipumzishe na kazi nielekee home kwa ajili ya matibabu.

Sasa nikiwa narudi home kutoka makumbusho nikaona sio mbaya nipite zahanati japo kupata dawa. Mda huo nipo maeneo ya udsm hapo, nikashuka kwenye gari na kuingia zahanati ya chuo. Nikiwa katika benchi la kusubiri matibabu nikaona kama watu wawili wakiwa wamevimba macho mmoja alivimba yote, hata haikunishtua. Ikafika zamu yangu nikaingia kwa daktari nilipofika tu baada ya kumkabidhi fomu ya nhif akaanza kuandika dawa then akaniuliza kuna kingine tofauti na macho ikabidi nijibu hapana. Aksema nenda famasi kachukue dawa.

Nimefika famasi nikapewa dawa kilichonishangaza zaidi nikaona ile meza ya pale dirishani kumejaa dawa za macho tu. Akili ikanambia acha kufatilia mambo yasiokuhusu. Nikachukua zangu dawa chaap nikaelekea home kupumzika.

Nimefika home mida ya saa 12 jioni mara kidogo namuona jamaa yqngu nae amerudi analalamika jicho linauma nikwambia hata mimi linazingua sema nenda hospital ukapate dawa. Jamaa akanambia shida ni nini mbona familia ya mtee fulani watu zaidi ya watatu nao wanashida hiyo hiyo.


Sasa ombi langu kwa wizara kama kuna shida tupeane taarifa tusisubiri ugonjwa uenee sehem kubwa pia wanajamii waelekezwe namna ya kujikinga na maambukizi hayo.


Naomba kuwasilisha
Hii ni kweli ndani ya wiki mbili imeshuhudia watu zaidi ya sita akiumwa macho
 
1. Watu wana tumia sn TV/computers/simu either kucheza games or kuangalia yanayoendelea or movies bilakuyapumzisha macho.
2 kutokana na hali ya hewa ya mvua watu hawanywi maji ya kutosha
3 kula sn vyakula vya kukaanga na hasa chips and kidali
Haya yote kwa asilmia kubwa yanaharibu macho na usipoangalia utaumwa mpk na kichwa kwakua misuli inachoka
 
Back
Top Bottom