Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
Fuatilia yanayojiri kwenye Bunge la 12, Mkutano wa 12, Kikao cha 3, leo Agosti 31, 2023.
Ratiba:
WAZIRI GWAJIMA: MILA YA KUWEKEZA MKE AKIWA TUMBONI INACHOCHEA UKATILI WA KIHISIA
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima amesema mila hiyo ina madhara, inachochea ukatili wa kihisia, ndoa za utotoni na inamnyima mhusika haki ya msingi ya kumchagua mwenza wa kuishi naye umri utakapofika.
Ufafanuzi huo umetolewa baada ya hoja ya Mbunge Maryam Azan Mwinyi aliyehoji mpango wa Serikali kutokomeza Mila ya kuwekeza mke akiwa tumboni kwa mama hasa katika maeneo ya Mikoa ya Manyara na Arusha.
Luhaga Mpina: Serikali inasema Uwekezaji umeongezeka, je dola zimeenda wapi?
Mbunge Luhaga Joelson Mpina akichangia hoja Bungeni kuhusu Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Hitifaki ya Biashara ya Huduma ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ya Mwaka 2012.
Amehojia “Rais Jakaya Kikwete alisaini mkataba huo mwaka 2012, leo unarejeshwa kuna marekebisho gani? Dola nazo zimeadimika, Serikali inasema Wataelii wameongezeka na Uwekezaji umeongezeka, Dola zimeenda wapi? Serikali lazima iwajibike kwa kutatua uhaba wa Dola Nchini.
MSITUME NYARAKA ‘WHATSAPP’ Ni marufuku
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete amesema sheria inayosimamia nyaraka za Serikali inaelekeza kuwa mawasiliano ya Serikali yafanyike kwa njia ya barua na si vinginevyo.
Kufuatia kuwepo kwa sheria hiyo, Naibu Waziri Kikwete amewaonya watendaji wa Serikali ambao wanatumia njia ambazo sio rasmi kutuma nyaraka.
“Haitokuwa sawa na ni marufuku ya Serikali kuwasilisha au kutumiiana ‘Documents’ za Serikali kupitia njia ya WhatsApps na njia nyingine zisizo rasmi, isipokuwa kwa maelekezo ambayo yatakuwa yametolewa vinginevyo katika mamlaka,” amesema Naibu Waziri Ridhiwani Kikwete.
Ameyasema hayo Bungeji jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Janejelly Ntate James ambaye amehoji uhalali wa matumizi ya makundi ya WhatsApp kutumiana nyaraka.
Aidha, Naibu Waziri Kikwete amelihakikishia Bunge kuwa Serikali bado inaendelea kutengeneza mifumo mbalimbali ambayo itaileta Serikali yote katika adabu ya utendaji.
Ratiba:
- Dua
- Hati za kuwasilisha Mezani
- Maswali
- Hoja za Serikali
WAZIRI GWAJIMA: MILA YA KUWEKEZA MKE AKIWA TUMBONI INACHOCHEA UKATILI WA KIHISIA
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dorothy Gwajima amesema mila hiyo ina madhara, inachochea ukatili wa kihisia, ndoa za utotoni na inamnyima mhusika haki ya msingi ya kumchagua mwenza wa kuishi naye umri utakapofika.
Ufafanuzi huo umetolewa baada ya hoja ya Mbunge Maryam Azan Mwinyi aliyehoji mpango wa Serikali kutokomeza Mila ya kuwekeza mke akiwa tumboni kwa mama hasa katika maeneo ya Mikoa ya Manyara na Arusha.
Luhaga Mpina: Serikali inasema Uwekezaji umeongezeka, je dola zimeenda wapi?
Mbunge Luhaga Joelson Mpina akichangia hoja Bungeni kuhusu Azimio la Bunge kuhusu mapendekezo ya kuridhia Hitifaki ya Biashara ya Huduma ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) ya Mwaka 2012.
Amehojia “Rais Jakaya Kikwete alisaini mkataba huo mwaka 2012, leo unarejeshwa kuna marekebisho gani? Dola nazo zimeadimika, Serikali inasema Wataelii wameongezeka na Uwekezaji umeongezeka, Dola zimeenda wapi? Serikali lazima iwajibike kwa kutatua uhaba wa Dola Nchini.
MSITUME NYARAKA ‘WHATSAPP’ Ni marufuku
Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Ridhiwani Kikwete amesema sheria inayosimamia nyaraka za Serikali inaelekeza kuwa mawasiliano ya Serikali yafanyike kwa njia ya barua na si vinginevyo.
Kufuatia kuwepo kwa sheria hiyo, Naibu Waziri Kikwete amewaonya watendaji wa Serikali ambao wanatumia njia ambazo sio rasmi kutuma nyaraka.
“Haitokuwa sawa na ni marufuku ya Serikali kuwasilisha au kutumiiana ‘Documents’ za Serikali kupitia njia ya WhatsApps na njia nyingine zisizo rasmi, isipokuwa kwa maelekezo ambayo yatakuwa yametolewa vinginevyo katika mamlaka,” amesema Naibu Waziri Ridhiwani Kikwete.
Ameyasema hayo Bungeji jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Janejelly Ntate James ambaye amehoji uhalali wa matumizi ya makundi ya WhatsApp kutumiana nyaraka.
Aidha, Naibu Waziri Kikwete amelihakikishia Bunge kuwa Serikali bado inaendelea kutengeneza mifumo mbalimbali ambayo itaileta Serikali yote katika adabu ya utendaji.