Elections 2010 Waraka wa Waislam Kuhusu Uchaguzi Wakamilika

Watanzania kwa kupenda siasa na kuongea maneno mengi vitendo sifuri ndio wenyewe.

Kwanini hawa watu wa dini hawatoi waraka juu ya kilimo bora na namna ya kumsaidia mwumini aweze kujitegemea? Kwanini hawatoi waraka juu ya elimu bora kwa vijana wetu na namna ya kuzisadia shule za vijana wetu ziweze kuwa nzuri?

Wache wote watoe lakini ni kama tunapoteza muda kujadiliana mambo ambayo yanaeleweka na kilichobaki ni sisi kwenye majumba yetu na kwenye jamii yetu kuyatekeleza.

Hivi kuna mtu ambaye hajui madhara ya ufisadi mpaka ahitaji waraka kuyaelewa? Kwanini basi hatufanyi kitu pamoja na kujua ubaya wake?

Mtu mwenye njaa atachukua pesa kutoka kwa fisadi hata akijua kufanya hivyo ni vibaya.

Juhudi ifanyike kuwafanya watu waweze kujitegemea; hilo ndilo muhimu kuliko mengine yote. Kuna mwana JF aliandika hapa kwamba mwenye njaa hawezi kuwa na mawazo huru. Mimi nakubaliana naye.

Tukiondoa umaskini uliokithiri na tukiwasaidia vijana wetu kupata elimu bora, hao mafisadi hawatakuwa na muda mwingi wa kutunyanyasa.
 
Serikali inawaogopa sana waislamu haina uwezo wa kuwapiga mkwara. Waislamu ndio wana uwezo wa kuipiga mkwara serikali, na serikali mara zote huwa inawabembeleza. It is misleading kusema serikali imewachimba mkwara waislamu, labda ingeanza kuwachimba mkwara wakristo.
 
Kingunge kawajia juu maaskofu wa Kikatoliki kwa waraka wao ambao unaeleza waziwazi sifa za kiongozi bora anayetakiwa kuchaguliwa na wananch bila hata kujali dini wala Kabila,

Kalalamika haya sasa waisalamu nao wamekuja na waraka wao. Let us wait na tuone kilichopo humo.
Taasisi za dini zina wajibu wa kuwaelimisha wafuasi wao kwa kuzingatia sheria na katiba ya nchi na kwa maslahi ya Taifa,
Mana KIna Kingunge na CCM yao walishashindwa masuala ya maslahi ya TAifa. au mnasemaje waungwana???
 
Watanzania kwa kupenda siasa na kuongea maneno mengi vitendo sifuri ndio wenyewe.

Kwanini hawa watu wa dini hawatoi waraka juu ya kilimo bora na namna ya kumsaidia mwumini aweze kujitegemea? Kwanini hawatoi waraka juu ya elimu bora kwa vijana wetu na namna ya kuzisadia shule za vijana wetu ziweze kuwa nzuri?

Wache wote watoe lakini ni kama tunapoteza muda kujadiliana mambo ambayo yanaeleweka na kilichobaki ni sisi kwenye majumba yetu na kwenye jamii yetu kuyatekeleza.

Hivi kuna mtu ambaye hajui madhara ya ufisadi mpaka ahitaji waraka kuyaelewa? Kwanini basi hatufanyi kitu pamoja na kujua ubaya wake?

Mtu mwenye njaa atachukua pesa kutoka kwa fisadi hata akijua kufanya hivyo ni vibaya.

Juhudi ifanyike kuwafanya watu waweze kujitegemea; hilo ndilo muhimu kuliko mengine yote. Kuna mwana JF aliandika hapa kwamba mwenye njaa hawezi kuwa na mawazo huru. Mimi nakubaliana naye.

Tukiondoa umaskini uliokithiri na tukiwasaidia vijana wetu kupata elimu bora, hao mafisadi hawatakuwa na muda mwingi wa kutunyanyasa.

ndugu inaonyesha ni jinsi gani haujausoma huo waraka .. na kama umeusoma basi haujauelewa ... mambo yote hayo yameanishwa .. elimu, uchumi, kilimo etc .. etc

Kwanini unafikiri Kingunge ameshindwa kukosoa contents na kuishia kukosoa mantiki yake - which is also wrong??

tuache ushabiki usiona na manufaa
 
ila kama hawa waislam walikuwa wanaupinga waraka katoliki wao wanasababu gani kutoa nao waraka, kazi sana
 
Kama Waraka utakuwa ni kwa Mustakabali wa Taifa then I real welcome it, tuuchambue ila kama ni COUNTER ROMAN CATHOLIT WARAKA then watakuwa wameshindwa kabla hawajaanza
 
Hidaya Kivatwa na Salim Said
SHURA ya Maimamu wa Tanzania, kesho inatarajia kuzindua rasmi mwongozo kwa Waislamu kuhusu uchaguzi mkuu wa 2010 na moto wa siasa za ukombozi.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 8:00 mchana.

Akizungumza na waandishi wa habari Kinondoni jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa kamati kuu ya siasa ya taasisi hiyo, Sheikh Ponda Issa Ponda, alisema uzinduzi huo utahudhuriwa na zaidi ya masheikh 100 kutoka katika mikoa 22 ya Tanzania Bara.

Alisema mwongozo huo utagusia masuala mbalimbali ya kitaifa yakiwemo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

“Mwongozo unahusisha masuala ya elimu, afya, uchumi, demokrasia, siasa na kilimo. Mambo mengi zaidi tutayaeleza katika uzinduzi ,” alisema Sheikh Ponda.

Alisema kila mkoa utatoa masheikh watano ambao watawawakilisha Waislamu wa mikoa yao na baadaye kuwarejeshea salamu za pamoja za Waislaam kwa serikali ya CCM.

Alisema mWongozo huo utakuwa na salamu na ujumbe maalum kwa serikali kufuatia kitendo chake cha kukaa kimya wakati Kanisa Katoliki, lilipotoa waraka ambao kimsingi unahatarisha amani, usalama na umoja wa kitaifa.

“Ndani ya mwongozo wetu kuna ujumbe maalum kwa serikali ya CCM kwa kule kakaa kimya kwake kimya baada ya Kanisa Katoliki kutoa waraka ambao kimsingi jamii na serikali zinajua kabisa kwamba unahatarisha umoja wa kitaifa,” alisema Sheikh
Ponda.
Alisema huko nyuma, viongozi wa madhehebu ya Kiislamu walijaribu kutoa elimu ya uraia, lakini serikali iliwakamata na kuwawe ndani kwa madai ya uchochezi.

"Je waraka na ilani ya Wakatoliki hazileti uchochezi,” alihoji Ponda.

Alisema mwongozo huo utaweka mwelekeo na msimamo wa pamoja wa Waislamu kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu na uchaguzi mkuu wa urais, ubunge na udiwani utakaofanyika mwakani

SOURCE:http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14158
 
Serikali inawaogopa sana waislamu haina uwezo wa kuwapiga mkwara. Waislamu ndio wana uwezo wa kuipiga mkwara serikali, na serikali mara zote huwa inawabembeleza. It is misleading kusema serikali imewachimba mkwara waislamu, labda ingeanza kuwachimba mkwara wakristo.

Hii ya serikali kuwaogopa waislamu imenimaliza kabisa. Kwa nini serikali iwaogope waislam kama serikali yenyewe ni kama vile inaongozwa na waislam?

1. Rais wa nchi
2. Makamo wa rais
3. Waziri wa fedha
4. Waziri wa ulinzi

nk....

CCM yenyewe imejaa waislam. Sasa kuna haja gani kwa serikali kuwaogopa waislam?
 
Hidaya Kivatwa na Salim Said
SHURA ya Maimamu wa Tanzania, kesho inatarajia kuzindua rasmi mwongozo kwa Waislamu kuhusu uchaguzi mkuu wa 2010 na moto wa siasa za ukombozi.

Uzinduzi huo unatarajiwa kufanyika katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 8:00 mchana.

Akizungumza na waandishi wa habari Kinondoni jijini Dar es Salaam jana, Katibu wa kamati kuu ya siasa ya taasisi hiyo, Sheikh Ponda Issa Ponda, alisema uzinduzi huo utahudhuriwa na zaidi ya masheikh 100 kutoka katika mikoa 22 ya Tanzania Bara.

Alisema mwongozo huo utagusia masuala mbalimbali ya kitaifa yakiwemo ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.

“Mwongozo unahusisha masuala ya elimu, afya, uchumi, demokrasia, siasa na kilimo. Mambo mengi zaidi tutayaeleza katika uzinduzi ,” alisema Sheikh Ponda.

Alisema kila mkoa utatoa masheikh watano ambao watawawakilisha Waislamu wa mikoa yao na baadaye kuwarejeshea salamu za pamoja za Waislaam kwa serikali ya CCM.

Alisema mWongozo huo utakuwa na salamu na ujumbe maalum kwa serikali kufuatia kitendo chake cha kukaa kimya wakati Kanisa Katoliki, lilipotoa waraka ambao kimsingi unahatarisha amani, usalama na umoja wa kitaifa.

“Ndani ya mwongozo wetu kuna ujumbe maalum kwa serikali ya CCM kwa kule kakaa kimya kwake kimya baada ya Kanisa Katoliki kutoa waraka ambao kimsingi jamii na serikali zinajua kabisa kwamba unahatarisha umoja wa kitaifa,” alisema Sheikh
Ponda.


Alisema huko nyuma, viongozi wa madhehebu ya Kiislamu walijaribu kutoa elimu ya uraia, lakini serikali iliwakamata na kuwawe ndani kwa madai ya uchochezi.

"Je waraka na ilani ya Wakatoliki hazileti uchochezi,” alihoji Ponda.

Alisema mwongozo huo utaweka mwelekeo na msimamo wa pamoja wa Waislamu kuelekea katika uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika mwezi Oktoba mwaka huu na uchaguzi mkuu wa urais, ubunge na udiwani utakaofanyika mwakani

SOURCE:http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14158

Kishaanza kujichanganya sasa.

Ohh, mwongozo wa kiraia na kielimu, kabla ya kupiga u-turn na kuanza kuwalamu wakatoliki.

Tafadhali mikanda ya mabomu ya kujilipua muiache nyumbani kwenu na wala msiilete mnazi mmoja maana vijana wa kazi mgulani na mabibo watawashikisha adabu mkileta upuuzi wenu hapa.
 
Kama forumite mwingine alivyodokeza kua huu waraka ukiwa tofauti na wawakatoliki basi kuna potential ya mikwaruzano kwasbabu uchaguzi ukija ni rahisi watu kua associate wanaopigania kura kwa kulinganisha yupi anakubalika zaidikutokana na waraka wa dini yake.

Tayari hapo tunaingiza udini kwenye siasa na uwezekano wa ghasia kubwa sana nafkiri ndio maana serikali inapinga.
Imagine wagombea wawili wanapigania ubunge eneo moja. Huyu anapanda na kusema yeye ndie kiongozi bora hata ukim assess kupitia waraka wa katoliki.
Mwingine aja na kusema yeye ni bora na sifa za waraka wa islam anazo zote. Sasa si ndio udini wenyewe tumeingiza.!!!
 
kesho watakuja walutheri, kisha wasababato, kisha waanglican na walokole n.k


lazima nchi ichukue hatua kinyume chake itakuwa balaa


Ilitakiwa ichukue hatuwa lakini udini wa viongozi umewagubika macho kiasi kwamba sasa wamechelewa kwani kuunyamazia waraka mmoja na kuukaripia mwengine utakuwa na tafsiri nyengine.
Just for curiosity Marmo ana madhehebu gani vile? Na Kingunge na Makwaia kwa upande wao Jee vipi? Naomba msaada hapo.
 
Muslims cautioned over document on elections


I think the government should stay quite in my opinion and not interfere this issue. They did not comment on Catholic's so called "Waraka" they are starting a new saga with muslims. Let us see what will be the next move.

Are you sure, the Government didn't comment? Have you forgotten what Pinda said when asked during Q&A session?
 
Ni waraka wa Kiislamu au wa waislamu?
Uletwe kwanza tuusome. Kama unapinga ufisadi na kukiuka miiko ya uongozi, na kuwataka waislamu wawachague viongozi wasio wezi na mafisadi na uletwe. Tuusome kwanza usipingwe tu bila hata kuuona. Naona Marmo naye ameanza Kingenge approach.


Kwa mujibu wa Kardinali Pengo ule waraka ni wa kimungu na tabia zetu tuna tofauti katika mambo ya kiungu katika dini zetu, sasa kwa hili tutakuwa tayari kukubaliana na huku nikiamini kuwa kigezo kimoja cha waraka wa Waislamu itakuwa kutaka waumini wao wamchague kiongozi atakaekuwa tayari kuleta Mahakama ya Kadhi?
Suala hili tuliliona ni dogo lakini lina upana wake na ndio Kingunge akalitanabahisha,
 
serikali inakimbia kinvuli chake,kweli uchaguzi ujao utakuwa wa ukweli zaidi. kila mtu atoe mwingozo lengo ni moja kupata watu waadilifu katika uongozi wa nchi, na mabudha na wahindu nao tusijeshangaa wametoa wa kwao.!
 
kesho watakuja walutheri, kisha wasababato, kisha waanglican na walokole n.k


lazima nchi ichukue hatua kinyume chake itakuwa balaa

Kama nyaraka zote zitapinga ufisadi na kuasa uadilifu, uwajibikaji, haki sawa kwa wote hakuna ubaya hata kama kila dini na kanisa na vyombo vya habari na vyama vya siasa vyote vitatoa nyaraka hata kama ni zaidi ya 100 kila siku.

Kitakachotakiwa ni moyo na speed ya kusoma tu! Shida itakuja pale ambapo dini au dhehebu moja badala ya kushughulikia hayo niliyoyataja kuanza kuwa'attack' wengine au kusababisha mtafaruku 'without justifiable cause'!

Swali langu ni hili: wakati waraka wa Katoliki ukitoka hao wanaotoa wa kwao walisema ni kuchanganya dini na siasa. Sasa sijui wa kwao watasema nini? Vilevile, kuna Makwaiya aliandaa programmes kadhaa na kujaribu kushawishi viewers kwamba Kanisa Katoliki limeanzisha machafuko ya kidini. Sasa je, ataweka programmes nyingine kusema hayohayo kwa waraka wa kesho au atanyamaza. Na yeye kama mwandisho mkongwe kama hatatoa similar programmes atakuwa anaonyesha bias au la?
 
Hii ya serikali kuwaogopa waislamu imenimaliza kabisa. Kwa nini serikali iwaogope waislam kama serikali yenyewe ni kama vile inaongozwa na waislam?

1. Rais wa nchi
2. Makamo wa rais
3. Waziri wa fedha
4. Waziri wa ulinzi

nk....

CCM yenyewe imejaa waislam. Sasa kuna haja gani kwa serikali kuwaogopa waislam?

Usichokijuwa kuwa kuna tofauti ya uislamu, wako waislamu wa siasa kali , wapo waislamu kanzu , wapo waislamu jina na tabaka nyingi nyingi hivyo huu wingi wao katika nafasi za uongozi hakuna maana yoyote.
 
Kishaanza kujichanganya sasa.

Ohh, mwongozo wa kiraia na kielimu, kabla ya kupiga u-turn na kuanza kuwalamu wakatoliki.

Tafadhali mikanda ya mabomu ya kujilipua muiache nyumbani kwenu na wala msiilete mnazi mmoja maana vijana wa kazi mgulani na mabibo watawashikisha adabu mkileta upuuzi wenu hapa.

Kwa Wakatoliki walisema kutoa waraka ni kuchanganya dini na siasa na je wao watakuwa nao wamechanganya dini na siasa au?
 
Are you sure, the Government didn't comment? Have you forgotten what Pinda said when asked during Q&A session?

Eti kuwa Kanisa lisidharau yanayosemwa (yanayoshauriwa) na watu juu ya waraka huo. Ndugu yangu hizo ndio comments unazoziita kuwa ni tamko la serikali? Nionavyo mimi ni kuwa amekubaliana na waraka na anataka kanisa lisipuuze maoni ya watu, Hilo ni karipio kama la Marmo?
 
Kama nyaraka zote zitapinga ufisadi na kuasa uadilifu, uwajibikaji, haki sawa kwa wote hakuna ubaya hata kama kila dini na kanisa na vyombo vya habari na vyama vya siasa vyote vitatoa nyaraka hata kama ni zaidi ya 100 kila siku.

Kitakachotakiwa ni moyo na speed ya kusoma tu! Shida itakuja pale ambapo dini au dhehebu moja badala ya kushughulikia hayo niliyoyataja kuanza kuwa'attack' wengine au kusababisha mtafaruku 'without justifiable cause'!

Swali langu ni hili: wakati waraka wa Katoliki ukitoka hao wanaotoa wa kwao walisema ni kuchanganya dini na siasa. Sasa sijui wa kwao watasema nini? Vilevile, kuna Makwaiya aliandaa programmes kadhaa na kujaribu kushawishi viewers kwamba Kanisa Katoliki limeanzisha machafuko ya kidini. Sasa je, ataweka programmes nyingine kusema hayohayo kwa waraka wa kesho au atanyamaza. Na yeye kama mwandisho mkongwe kama hatatoa similar programmes atakuwa anaonyesha bias au la?

Nafikiri Makwaia atainuka na kusema kuwa "Hili nililisema kabla". Watakachofanya Waislamu hakitokuwa tofauti na walichofanya wenzao yaani kuchanganya dini na siasa na wala tusijidanganye kuwa Waraka huo utapokelewa kwa tafsri nzuri na Wakatoliki kwa vile hivi sasa tunashuhudia tofauti ya matakwa na mambo yaliyowekwa mbele kati ya Wakirsto na Waislamu.
 
Sitta vipi na huu umeshausoma! vipi unawaambiaje wabunge waislamu unaunga mkono MWONGOZO? kama ulivyounga mkono WARAKA?
kiongozi unatakiwa uwe na subira na usiwe na jazba kuoongoza si mchezo bwana uongozi ni Dhamana Nasikia Na Budhits Nao Jumatatu Wanazinduwa Wao Itakuwa Kama Wanamuziki Na Wacheza Cinema Kila kukicha Wana Launch Kama Tuko Hollywood
 
Back
Top Bottom