Wapanga kumburuza Babu wa loliondo kortini

Imani ni kitu cha kusadikika. Ni kitu kinachoelea akilini tu. Na kitu ambacho hakithibitiki kwa kutumia kanuni za kisayansi au njia na michakato mingine ya kutafutia ukweli. Imani haishikiki, haionekani kwa macho, hainusiki kwa pua, na haisikiki na masikio, na wala haisikiki kwa kuigusa. <br />
<br />
Sasa yeye aliweka wazi tokea mwanzo kuwa pasipo na imani hata ukitumia dawa yake basi haitakuwa na nguvu ya kufanya kazi. Kwa maneno mengine, dawa yake hiyo ni ya kipoza-uongo (placebo-effect). Placebos hutumika hata kwenye hospitali za kawaida zinazotumia zana na mbinu za kisayansi katika kutibia. Madaktari hufikia uamuzi wa kumpa mtu kipoza-uongo pindi wagunduapo kuwa huyo mgonjwa husika anasumbuliwa na maruweruwe (matizo yaliyo imaginary). <br />
<br />
Kila dawa huwa zina masharti yake. Kuna dawa ambazo unatakiwa kuzimeza na chakula na zingine ambazo haijalishi, unaweza kuzimeza na chakula au pasipo na chakula. Na dawa ya babu pia masharti au sharti lake kuu lilikuwa ni imani. Pasipo na imani ni vigumu kwa hiyo dawa yake kufanya kazi. Hili aliliweka wazi kabisa. Serikali nayo ilifanyia uchunguzi hicho "kikombe" chake na kuona hakina madhara yoyote.<br />
<br />
Leo hii mnataka Babu aburuzwe mahakamani kwa misingi ipi? Kwa sababu tu kuna watu wenye magonjwa sugu ambao hawakupona baada ya kupata kikombe? Mbona waliambiwa pamoja na kikombe cha babu wasiache kutumia dawa zao. Kuna aliyedhurika baada ya kupata kikombe? Kuna aliyekufa baada ya kupata kikombe? Je, mnaweza kuthibitisha pasipo wingu la shaka kuwa ni kikombe cha babu ndicho kilichopelekea kudhurika au kupoteza maisha kwa mtu au watu kama wapo iliyowatokea hivyo?<br />
<br />
Kwa kweli hapo hamna kesi kabisa. Lakini kwa vile wana haki ya kwenda mahakamani, acha tu waende. Kwa yote ninayoyajua kuhusu Babu nakuhakikishia kuwa ataibuka kidedea labda kuwepo na mengine ambayo hayajulikani.
<br />
<br />
kweli kabisa.. Anaweza akajitetea hawakupona kwa sababu hawakuwa na imani.
 
Hehehehe! Mbona kuna watu wanatoa sadaka na misaada misikitini au makanisani lakini bado hawana imani? Imani ni mtu mwenyewe na sio gharama!
I don't believe kuwa watu hawakuwa na imani ndo waspone mtu atoke iringa mufindi na alipe nauli ya laki na nusu uniambie hana iman.
 
kila aliyekunywa kikombe na hajapona anatakiwa kunipa mimi sh 1000 kuna kitu mungu alisahau kumpa babu amenipa mimi kwa maelezo zaidi nipm<br />
usidharau,nimeoteshwa.
<br />
<br />
acha upuuzi wako, MUNGU hawezi kusahau, kumbukumbu zake hazielezeki..ungama hata kimoyo moyo
 
Imani ni kitu cha kusadikika. Ni kitu kinachoelea akilini tu. Na kitu ambacho hakithibitiki kwa kutumia kanuni za kisayansi au njia na michakato mingine ya kutafutia ukweli. Imani haishikiki, haionekani kwa macho, hainusiki kwa pua, na haisikiki na masikio, na wala haisikiki kwa kuigusa.

Sasa yeye aliweka wazi tokea mwanzo kuwa pasipo na imani hata ukitumia dawa yake basi haitakuwa na nguvu ya kufanya kazi. Kwa maneno mengine, dawa yake hiyo ni ya kipoza-uongo (placebo-effect). Placebos hutumika hata kwenye hospitali za kawaida zinazotumia zana na mbinu za kisayansi katika kutibia. Madaktari hufikia uamuzi wa kumpa mtu kipoza-uongo pindi wagunduapo kuwa huyo mgonjwa husika anasumbuliwa na maruweruwe (matizo yaliyo imaginary).

Kila dawa huwa zina masharti yake. Kuna dawa ambazo unatakiwa kuzimeza na chakula na zingine ambazo haijalishi, unaweza kuzimeza na chakula au pasipo na chakula. Na dawa ya babu pia masharti au sharti lake kuu lilikuwa ni imani. Pasipo na imani ni vigumu kwa hiyo dawa yake kufanya kazi. Hili aliliweka wazi kabisa. Serikali nayo ilifanyia uchunguzi hicho “kikombe” chake na kuona hakina madhara yoyote.

Leo hii mnataka Babu aburuzwe mahakamani kwa misingi ipi? Kwa sababu tu kuna watu wenye magonjwa sugu ambao hawakupona baada ya kupata kikombe? Mbona waliambiwa pamoja na kikombe cha babu wasiache kutumia dawa zao. Kuna aliyedhurika baada ya kupata kikombe? Kuna aliyekufa baada ya kupata kikombe? Je, mnaweza kuthibitisha pasipo wingu la shaka kuwa ni kikombe cha babu ndicho kilichopelekea kudhurika au kupoteza maisha kwa mtu au watu kama wapo iliyowatokea hivyo?

Kwa kweli hapo hamna kesi kabisa. Lakini kwa vile wana haki ya kwenda mahakamani, acha tu waende. Kwa yote ninayoyajua kuhusu Babu nakuhakikishia kuwa ataibuka kidedea labda kuwepo na mengine ambayo hayajulikani.


Tatizo la Babu ni kujigamba kuwa ana uwezo wa kutibu magonjwa sugu,yaliyoshindikana hospitali wakati dawa yake ni magumashi au placebo kama unavyosema.Wagonjwa waliacha tiba za hospitali,wakakimbia hospitali wakaamini kikombe kitawaponya.Matokeo yake ni maafa.

Babu alikuwa hana uhakika na dawa yake na ndiyo mana alikuwa ana insist watu waendelee na dozi ya hospitali,sasa kukiri dawa yake ni 'kimeo',akaona ataharibu biashara siyo?Wagonjwa hali zimekuwa mbaya zaidi,wameamua kurudia full dozi ya hospitali ili wasogeze siku na wengine wameshapoteza maisha kwa kuacha dozi na mikikimikiki ya kwenda kwa babu,halafu wewe unauliza tatizo liko wapi?
 
Mi nina swali dogo,kwa nini watu wanakufa kwa malaria wakati kuna dawa za kutibu?kwani wote wanaopewa dawa hospitali wanapona?wengine dawa mseto ikikataa wanawekewa drp lakini huwezi sema mseto haitibu,na pia unakuwa umepoteza hela,hivyo ni ujinga kuargue kuwa hawajapona kwa hiyo ni tapeli,basi mahospitali na madokta ni matapeli?
 
Tatizo la Babu ni kujigamba kuwa ana uwezo wa kutibu magonjwa sugu,yaliyoshindikana hospitali wakati dawa yake ni magumashi au placebo kama unavyosema.

Babu alijigamba lini na wewe? Yule mzee hana majigambo kabisa. He has a very unassuming demeanor and he is very soft-spoken. Kusema eti alijigamba ni kumzushia. Babu hata matangazo ya tiba yake hakuwa nayo au more appropriately hana. Ni word of mouth tu ndiyo ilipaisha jina lake.

Wagonjwa waliacha tiba za hospitali,wakakimbia hospitali wakaamini kikombe kitawaponya.Matokeo yake ni maafa.

Serikali iliwasihi wagonjwa wote waliokuwa wanapata kikombe wasiache kutumia dawa zao za hospitali. Sasa kama waliacha watakuwa walifanya hivyo kwa hiari yao wenyewe. You can't hold Babu criminally or civilly liable for that.

Babu alikuwa hana uhakika na dawa yake na ndiyo mana alikuwa ana insist watu waendelee na dozi ya hospitali,sasa kukiri dawa yake ni 'kimeo',akaona ataharibu biashara siyo?Wagonjwa hali zimekuwa mbaya zaidi,wameamua kurudia full dozi ya hospitali ili wasogeze siku na wengine wameshapoteza maisha kwa kuacha dozi na mikikimikiki ya kwenda kwa babu,halafu wewe unauliza tatizo liko wapi?

Ni lini Babu alisema dawa yake ni ya kisayansi? Yeye alisema ni ya kiimani. Toka lini imani ikahusishwa na uhakiki wa kisayansi?
 
Babu alijigamba lini na wewe? Yule mzee hana majigambo kabisa. He has a very unassuming demeanor and he is very soft-spoken. Kusema eti alijigamba ni kumzushia. Babu hata matangazo ya tiba yake hakuwa nayo au more appropriately hana. Ni word of mouth tu ndiyo ilipaisha jina lake.

Kujigamba si lazima upige kelele kwenye ma loud speakers kwamba unafanya kitu fulani.Ile kusema tu kaoteshwa na Mungu na dawa yake inatibu magonjwa sugu yaliyoshindikana hospitali ni majigambo.Kwamba watu wamepoteza muda na fedha nyingi kufanya tafiti na bado wanaendelea kuumiza vichwa lakini bado hawajagundua tiba ya hayo magonjwa,then mtu mmoja out there anaamka asubuhi na kudai kawasiliana na Mungu,ana dawa.Haya ni majigambo.Dawa yake imeshajulikana kuwa haitibu ni changa la macho,sasa acheni wajanja waende mbele waka sue,hata kama ushindi mnao mezani tayari kama ulivyosema.


Serikali iliwasihi wagonjwa wote waliokuwa wanapata kikombe wasiache kutumia dawa zao za hospitali. Sasa kama waliacha watakuwa walifanya hivyo kwa hiari yao wenyewe. You can't hold Babu criminally or civilly liable for that.

Hilo la kuacha kutumia dawa ni moja.Lakini inasemekana kuna wagonjwa wengi walifia njiani au kwenye foleni ya kwenda kupata kikombe cha babu.Kuna wagonjwa hata walitoroka/walitoroshwa hospitali wakiwa katika critical condition na kuacha matibabu mengine muhimu pale yanayowafanya waendelee kuishi wakitegemea kuwa babu ana dawa ya kuwatibu wakapona,lakini matokeo yake wakafia njiani.If it was not babu,maybe hawa still tungekuwa tunaishi nao mpaka leo wakiendelea na palliative care.Sasa if babu has not committed any crime,let the court of law decide the fate na siyo kutisha watu kuwa hakuna kesi hapa.




Ni lini Babu alisema dawa yake ni ya kisayansi? Yeye alisema ni ya kiimani. Toka lini imani ikahusishwa na uhakiki wa kisayansi?

Sikuwahi sema Babu alisema dawa yake ni ya kisayansi.Dawa ya babu ni ya kiimani kama unavyosema,isipokuwa alikuwa anajua kuwa dawa yake ni magumashi kwahiyo akawa anacheza na chances tu,kwamba ana insist dawa inatibu magonjwa sugu at the same time anawaambia wagonjwa waendelee na dawa za hospitali.Unamuhakikishia mgonjwa kuwa dawa yako inatibu ugonjwa wake na atapona,possibility ni kwamba mgonjwa ataachana na tiba ya zamani ambayo ni ya kutuliza tu.Mgonjwa akishaitumia atajiamini kuwa ameshapona,kumbe ni placebo effect.
Mkuu siamini kuwa hawa watu ni wajinga.Watakuwa wamejipanga vizuri tu na hii kesi whether madai au jinai.Wewe kama ulivyosema nenda kamtetee babu huko mahakamani.Siye wengine 'tunawasikilizia' kwa hamu sana,ilimradi tu haki itendeke
 
Lizzy,
Naona umeamua kumsemea Babu, Mbona wakati anachukuwa pesa alikuwa asemi kama mtu hana imani asitoe pesa yake hapa, na ile tiba alisema kaoteshwa na mungu kwenye hiyo dawa.
Labda utusaidie mtu mwenye imani hanakuwaje ebu tupe sifa zake na dalili za mwenye imani

Walioenda kule ni watu wazima na akili zao...hivyo walipaswa kuuliza na kujua wanachofuata kule kabla ya kwenda na kulipa mia tano zao wakidhani babu wa watu anatenda miujiza.

Alisema imani ndio inayoponya hivyo kile kikombe kilikua kinaponya pale kinapokutana na imani thabiti ya mnywaji.Tatizo ni kwamba wengi mnadhani kitendo cha mtu kupanda gari tu na kwenda kwa babu pamoja na kulipia sh. 500 kwaajili ya kikombe ni imani tosha.Sivyo...wengine walienda wakiwa na nia ya kujaribu kuona kama itafanya kazi kweli...wengine walikua wakijiaminisha kwamba nao wanaamini ila deep down walikua kama wa kwenye kundi la kwanza tofauti tu ni kwamba hawakulitambua hilo...na kundi la tatu ni wale waliokua na imani kweli.

Kama kundi la tatu lisingekuwepo kusingekuwepo na ushuhuda toka kwa watu waliiona mabadiliko mazuri kwenye afya zao‘!
 
Tusidanganyane mara mbili inaponya dawa na sio imani. Imani ni sanaa babu aliyoingiza ktk magumashi yake kupiga hela, mapapa na mitume wamekufa na imani zao..

Manake na kanisa lake pia linahusika
 
Hawa watu wanao sema wanampeleka babu mahakamani ni wanafiki kabisa, tena wanaposema watu wa watumishi wa Mungu au viongozi wa dini walishabikia hebu wawe wakweli na kufafanua watumishi/ viongozi wa dini gani walishabikia tiba ya loliondo, kwani kwa masikio yangu na vyombo vya habari viliripoti kuna baadhi ya wachungaji kama Zachary Kakobe walikemea na kueleza jinsi ambavyo babu anafanya usanii watu wakampinga na kumkebehi kakosa waumini ndio maana acha wajiendee loliondo wakapate tiba leo wanatuletea hoja isiyo na mashiko eti wana mpeleka babu mahakamani kwani aliwalazimisha kunywa? si mlijipeleka wenyewe? Mimi nina mfano hai mama yangu amepooza na ndugu zangu wakaja juu kwa presha ya ajabu ooo lete pesa mama na babu waende loliondo nikawaambia mama katika hali kama hii sitoi hata shilingi ili aende loliondo kwani yuko katika dozi ya hosp na anaendelea vizuri, wakaniona mbaya wakaamua kuchangishana kisha kukodi gari mpaka loliondo, pia niliwaeleza mmeamua kuwapeleka huko akipatwa na shida muyamalize wenyewe,baada ya kikombe mama akawa hoi sana babu yangu baada ya kikombe akafariki , ikanibidi mimi kusafiri haraka mpaka mkoani kumuwahisha mama hosp akiwa na hali mbaya Mungu akasaidia mama anaendelea vizuri baada ya tiba hosp lakini babu nilimpoteza na mama kulingana na afya yake mpaka leo wamemficha hajui kama babu alifariki, ndugu walio wapeleka wakakimbia wote na kuniachia mama nina muuguza na mpaka leo huwasikii wana ongelea babu wa loliondo kwani na wao walirudi hoi kwa mateso makubwa. Hivyo watu wana takiwa kuwa makini sana wanaposikia kuna tiba mahali na kufanya utafiti wa kina bila kujali wanaumwa kwa kiwango gani kwani unaweza kujiletea matatizo makubwa kuliko ya kwanza ambayo pia yalimkuta mama yangu.TUJIFUNZE KWA MAKOSA YA WENZETU SIO MAKOSA YETU. Nina imani wote walio kutwa na mkasa wa babu wa loliondo na vikombe vingine wakati mwingine watakuwa makini.
 
Tort may be defined as a personal injury; or as "a civil action other than a breach of contract."[SUP][citation needed][/SUP]
A person who suffers a tortious injury is entitled to receive "damages", usually monetary compensation, from the person or people responsible — or liable — for those injuries. Tort law defines what is a legal injury and, therefore, whether a person may be held liable for an injury they have caused. Legal injuries are not limited to physical injuries. They may also include emotional, economic, or reputational injuries as well as violations of privacy, property, or constitutional rights. Tort cases therefore comprise such varied topics as auto accidents, false imprisonment, defamation, product liability (for defective consumer products), copyright infringement, and environmental pollution (toxic torts), among many others.
In much of the common law world, the most prominent tort liability is negligence. If the injured party can prove that the person believed to have caused the injury acted negligently – that is, without taking reasonable care to avoid injuring others – tort law will allow compensation.
However, tort law also recognizes intentional torts, where a person has intentionally acted in a way that harms another, and "strict liability" or quasi-tort, which allows recovery under certain circumstances without the need to demonstrate negligence.
 
kiendacho kwa mganga hakirudi:coffee:

Tatizo hizi methali hazifundishwi siku hizi mashuleni. Wanaopaswa kushtakiwa na wale wenye heshima zao katika jamii walioimarket na kuipigia debe hadharani, wachungaji, maaskofu na wanasiasa-hasa Lukuvi, Pombe etc
 
Jamani mbona kuna mtu namfahamu amepona saratani ya ubongo na madokta wamekubali kuwa amepona. Sielewi nisemeje! :C
 
Ohhh, hii ndio Tanzania zaidi tuijuavyo. Kwakweli nawapa pole sana wale wote waliopoteza muda na pesa zao kwenda huko Loliondo kupata tiba ya kikombe. Wanaosema swala la Imani wanakosea sana, babu na askofu Laizer hawakuwai kusema kwamba inabidi uwe na imani. Nakumbuka Askofu Laizer alisema eti wanaompinga babu wanafanya hivyo sababu biashara zao za hospitali na za maombezi zinakosa watu. Akasisitiza kwamba kanisa la Luthereni Ushirika wa Arusha (kaskazini) anouongoza una hospitali nyingi kama Seliani ambazo nazo zinapata hasara lakini yeye hapingi.

Nilikuwa maeneo ya fotikoma nje kidogo ya hifadhi ya Taifa ya Serengeti kikazi kwanzia mwezi wa tatu mpaka mwishoni mwa mwezi wa nne na niliona misururu ya magari iliyokuwa inakatiza pale kulekea geti la Ikoma kuingia hifadhi ya Serengeti wakiwa wanaelekea Loliondo. pale getini palikuwa panajaa watu mpaka vyoo vya pale getini vikawa havitoshi watu wakawa wanajisaidia njee ya choo. kulikuwa kuna uchafuzi mkubwa sana wa mazingira.

Kuhusu swala la Imani, nakumbuka iliwai kuonyeshwa kwenye Tv mtu aliyemwibia mkenya mmoja huko Loliondo akapigwa akawa kama amekuwa chizi, babu akamnywesha kikombe akapona mara moja, Je huyo nae alikuwa na imani??!!

Katika hili zogo lote, Napenda sana sana kulishukuru gazeti la RAIA MWEMA linalotoka kila Jumatano. Hili ni gazeti makini sana na nalipenda sana. lilikuwa na makala ambazo kama wale walikuwa na hamu za kwenda kule wangezisoma na kuzielewa wangeairisha kwenda huko. Specifically namshukuru sana Johnson Mbwambo, Magid Mjengwa na Padri Privatus Karugendo. Asanteni sana kwa kunielimisha. kuna mtu amepata PhD kwa kuelezea 'antiviral chemicals' zinazopatikana kwenye ule mti wa babu. TAFORI (Tanzania Forestry Research Institute) wanaonesha matumizi ya mti huo tangu zamani ambapo mizizi yake ilichemshwa kupata dawa ya gonorea. Leo baadhi ya Watanzania wanasema ina dawa ya ukimwi, kisukari, presha, pumu, nk. Babu mwenyewa alikuwa anajichanganya sana na hizo kauli zake, kuna siku nilimsikia kwenye kipindi maalum cha TBC anasema kwa msisitizo ile ni dawa na sio kinga, siku nyingine nikamsikia kwenye ITV anasema hajui kama ni kinga (vaccine).

Kama hiyo kesi itafunguliwa, itakuwa ya aina yake kabisa. Tusubiri tuone ila Watanzania tuamke sasa tuwe 'aggressive' na tuhoji vitu kwa undani sio watu wa kufuata upepo. kuhusu listi ya waliokunywa hicho kikombe ipo, sababu ofisini kwetu walioenda waliniambia gari likikaribia kumfikia babu, mnajiandikisha mliopo kwenye hilo gari na miatanotano zenu mnakabidhi msaidizi wa babu getini, then mnaenda kupiga kikombe feki cha babu baada ya safari yenye mateso makubwa. List hiyio ipo Mtikila na wengine wanaotaka kumshtaki babu waifuatilie.
 
BABU KORTINI

Na Makongoro Oging'
Baadhi ya wagonjwa wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi waliokunywa kikombe cha Mchungaji Ambilikile Masapile (pichani) mwaka huu katika Kijiji cha Samunge, Loliondo mkoani Arusha hatimaye wameamua kumburuza mahakamani kiongozi huyo kwa madai kwamba dawa yake haitibu kabisa na wamedanyanywa.

"Babu wa Loliondo amedanganywa na shetani na siyo kwamba alielezwa na Mungu, nashangaa viongozi wa dini wanaompigia debe wakati wao siyo wataalamu wa kujua kama dawa hiyo inaponya au la, ni ushabiki wa kidini usiokuwa na maana, lengo lao ni kuchuma fedha kwa wagonjwa.

Kwa nini wasiwaachie wataalamu kushughulikia suala hilo?

MAJIBU YA BABU KWA WASIOPONA
Mwandishi wetu wa Arusha wiki iliyopita alizungumza na msaidizi wa Mchungaji Masapile kwa njia ya simu, Paulina Lucas na kuulizwa kuhusu malalamiko hayo akasema wasiopona ni wale ambao hawana imani.

"Kama hawajapona siyo makosa yetu. Tuliwaambia kabla kuwa katika tiba hii kigezo cha kwanza ni kuwa na imani na hapa tuna uthibitisho wa kutosha wa watu walioponywa na maajabu ya dawa hii wakiwemo wagonjwa wenye Ukimwi," alisema Paulina.

Alidai kuwa kuna baadhi ya watu wanaoishi na Virusi Vya Ukimwi si wakweli kwani kuna uwezekano kuwa wamepona lakini wanashindwa kuweka wazi kwa malengo ya kukosa fedha wanazopewa na wafadhili.

Chanzo:BABU KORTINI - Global Publishers
.

Haya sasa wa bongo ngoma hiyo, huu ni ule mfumo uitwao mind control, mnapewa jambo lisilo la msingi ili kuwa keep bise msahau yaliyo ya msingi, mnampeleka hicho kizee mahakamani, mmesahau hao wanaokula pesa kibao zilizotolewa na wafadhili kwaajili ya kupambana na kuwasaidia wagonjwa wa ukimwi, Badala ya kupambana na hao wanaosababisha hospitali zina kosa dawa hata za magonjwa ya kawaida kabisa mpaka watu wanakimbilia Loliondo, badala ya kupambana na hao wanaosababisha nchi kuwa katika mgao wa umeme katika karne ya 21, badala ya kupambana na hao viongozi wanao ruhusu kununua magari ya kifahari na hospitali hazina magari ya wagonjwa, wagonjwa wangapi wamekufa wakisubiri operation zilizoshindikana kwa kukosa umeme, hakuna hata mafuta ya generator, JE TUNATAKA UKOMBOZI WA KWELI AU USHABIKI?
 
Hakuna imani wala baba yake na imani. Ilkuwa changa la moto laini. Wajinga ndio walwao. Babu kavuna sana
 
&lt;br /&gt;<br />
&lt;br /&gt;<br />
sentens yako aieleweki madokta wamesema then kuna alama ya kiulizo na bado uelewi cha kusema.
<br />
<br />
sorr ni kwamba madokta wamesema amepona! Sasa sijui anakuwaje wamepona wengine halafu wengine hawajapona.
 
Hii imenikumbusha alichosema TB Joshua! Kwamba wachungaji wengi (healing ministries) wanawaombea watu, wasipopona wanajitetea kuwa imani yako haba! Imagine mtu aliyeuza shamba akapata nauli kusafiiri kwa shida unamwambia imani yake haba! Kipimo cha imani ni nini?

Babu was either smart au huyo mungu wake alimpa tricky hiyo, au kulikuwa na brain nyingine behind Babu yeye akatumika tu!
Hapa ndipo suala lilipo. Imani juu ya nani? Imani juu ya nini?
Imani juu ya Mungu, Yesu, Babu?
Imani juu ya kikombe cha babu au tiba yoyote?
Ikiwa ni Imani kwa Mungu, kuna lazima gani kuwepo (babu) mtu wa tatu ndio ufanikiwe?
Ikiwa ni Imani juu ya Kikombe, kwa nini mtu asipone wakati amekubali kufilisika kwa kuuza vyake vyote, kukopa ili afike kwa babu? Imani tena gani zaidi ya kupoteza chako.
Babu, kama wajanja wengine wengi wa nchi hii, aliona mwanya akautumia, kama walivyoona mwanya huo DECI. Tusubiri mjanja mwengine aje kutunyoa badae tulalamike. Ndio zetu hizo! (Ni maoni yangu tu).
 
Back
Top Bottom