MKWEAMINAZI
JF-Expert Member
- May 28, 2023
- 930
- 1,299
Kwanza nitoe pole kwa kifo cha mchungaji mzee wetu mwaisapila "Babu wa loliondo."
Nije kwenye ajenda husika. Babu wa loliondo aliutangazia umma kuwa kaoteshwa na mungu dawa ya kutibu magonjwa sugu kama vile UKIMWI, pressure, kisukari n.K nilitarajia kusikia serikali imemtaka apeleke dawa zake zikafanyiwe utafiti kwanza kama kweli zinatibu ili apewe kibali cha kutibu.
Badala yake Wananchi walimiminika loliondo kwa misafara mirefu ya magari makubwa kwa madogo malori kwa mabasi licha ya ubovu wa barabara uliosababisha magari kukwama na wagonjwa kufariki kabla hata ya kunywa kikombe cha babu.
Kikombe kilichopatikana na kugawiwa na babu mwenyewe tu na hakuna aliyeruhusiwa kugawa kikombe baada ya kulipa sh.500/= tu
Kilichonishangaza ni serikali bila kujiridhisha kuwa dawa ya babu kama inatibu ilianza kukarabati barabara. Kingine kilichonishangaza ni ujio wa viongozi wa Serikali kushiriki unywaji wa kikombe cha babu huku wakijua tiba ya babu haijafanyiwa utafiti na serikali.
Swali ya kujiuliza
Kwanini serikali iliiamini tiba ya babu wa loliondo bila kuifanyia utafiti na ikawaacha wananchi kuitumia?
1. Je endapo ingetokea tiba ya babu ikaua wananchi mamia kwa maelfu lingekuwa kosa la babu wa loliondo wananchi waliokunywa au serikali kutokuifanyia utafiti?
2. Je ujio wa babu wa loliondo ulitengenezwa na kundi fulani la wahuni kwa kushirikiana na babu wa loliondo mzee mchungaji mwaisapila ili kujipatia fedha na kutupima ujinga watanzania?
Nije kwenye ajenda husika. Babu wa loliondo aliutangazia umma kuwa kaoteshwa na mungu dawa ya kutibu magonjwa sugu kama vile UKIMWI, pressure, kisukari n.K nilitarajia kusikia serikali imemtaka apeleke dawa zake zikafanyiwe utafiti kwanza kama kweli zinatibu ili apewe kibali cha kutibu.
Badala yake Wananchi walimiminika loliondo kwa misafara mirefu ya magari makubwa kwa madogo malori kwa mabasi licha ya ubovu wa barabara uliosababisha magari kukwama na wagonjwa kufariki kabla hata ya kunywa kikombe cha babu.
Kikombe kilichopatikana na kugawiwa na babu mwenyewe tu na hakuna aliyeruhusiwa kugawa kikombe baada ya kulipa sh.500/= tu
Kilichonishangaza ni serikali bila kujiridhisha kuwa dawa ya babu kama inatibu ilianza kukarabati barabara. Kingine kilichonishangaza ni ujio wa viongozi wa Serikali kushiriki unywaji wa kikombe cha babu huku wakijua tiba ya babu haijafanyiwa utafiti na serikali.
Swali ya kujiuliza
Kwanini serikali iliiamini tiba ya babu wa loliondo bila kuifanyia utafiti na ikawaacha wananchi kuitumia?
1. Je endapo ingetokea tiba ya babu ikaua wananchi mamia kwa maelfu lingekuwa kosa la babu wa loliondo wananchi waliokunywa au serikali kutokuifanyia utafiti?
2. Je ujio wa babu wa loliondo ulitengenezwa na kundi fulani la wahuni kwa kushirikiana na babu wa loliondo mzee mchungaji mwaisapila ili kujipatia fedha na kutupima ujinga watanzania?