Michelle
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 7,621
- 3,514
- Thread starter
- #101
Maswali yako ni muhimu na yamekuwa yakisumbua wanawake makini! Wanawake wengi hawana muda wa kutaka kujua kusudi au dhumuni kuu la mwamme anayemtongoza, wengi huamini haraka na kuweka matumaini makubwa hata kama amekutana na mpenzi wake huyo ndani ya basi. wanawake wengi hawatambui kuwa wanaume wengi sio wakweli na ni fahari yao kudonoadonoa wanawake wanojirahisi kutokana na sababu zao kadha wa kadha. wakati mwanamke akiamini kuwa anampenzi wake anayempenda, kutokana na kuamini kuwa kila mara anatumiwa msg, au anatumiwa salio, au amepewa ofa, wanaume wengi hutumia vitu kama hivyo ili kuwapata wanawake wasio makini na wanaopenda ofa na kufadhiliwa. wanaume wengi hawana Upendo wa dhati ila wana kutamani ambako ndiyo kunasukuma kutaka kujaribu kila mwanamke ili mradi amejichanganya. Ukishasex na mwanaume wa aina hiyo ujue, huo ni mwanzo wake wa kujaribu pengine, wanaume wengi swala la kusex huweka kama burudani hivyo sio tatizo kwao kutafuta kiwanja chochote na kucheza mechi. Nilishawahi kutoa thread inayohamasisha wanawake kujua tabia za wanaume. Ukishazijua tabia zao hawatakusumbua. Maana wakati mwanamke anamapenzi ya dhati Mwanaume (wengi ) wamejaa kutamani na are not fit for women consumption!!!
Thank you very much Anold!