Nicas Mtei
JF-Expert Member
- Dec 21, 2010
- 11,556
- 7,085
Movie inaendelea
Hahah halafu wanaanza na .........hakuibiwa na mwanamke!! Mh. unatumia nguvu nyingi sana kujisafisha kitu kinachozidi kutufanya tuamini yale tunayoyaamini. Kaa kimya tu ushasomeka.
Fiction?
Tangu sakata hili lianze mimi nilisema ingekuwa ni nchi za wenzetu walio makini POLISI angepandishwa cheo kwa ku-UNCOVER huu uongo wa Malima. Lakini nchi hii ya Wadanganyika huyo RPC Adolphina Chialo atapandishwa cheo kwa ku-COVER UP uongo wa Malima.
Lakini pia anapojaribu ku-cook up hii story ya Malima, awaapatie basi hata POLISI wenzake wajaribu kufukia fukia mashimo, kwani ina matundu mengi ambayo hata mtoto wa STD I atayachana chana vibaya
1. Vitu vilikutwa kwa mama Mdogo? Huyo mama Mdogo hatajwi jina wala sehemu anayoishi?!
2. Watuhumiwa tayari wamekamatwa, Majina yao na sehemu wanaoishi hayatajwi?
3. Aliyemuibia sio MWANAMKE! Ina maana mwizi wanamfahamu na atakuwa mawanaume, kwanini hawamsemi?
4. Nyao za mwizi zilikutwa nje ya dirisha la Malima,mwizi hakuwa na viatu, Asubuhi ya tukio nyao hizo hatukuziona!
5. Malima alikiri alikuwa na SMG, Kaimu kamanada amesema SMG haikuibiwa, RPC anasema hakuwa na SMG? Lakini pia hasemi ilikuwa ni bunduki ya aina gani?
Nchi hii kweli imejaa usanii, lakini kinachonisikitishwa kuna W.A.J.I.N.G.A tena wengi wanao buy hii cooked story!
A cooked story?
A cooked story?
Kwa sababu wazushi walisema kaibiwa na mwanamke, huyo mwanamke yuko wapi? wacheni majungu.
Ndio hayo, ya fulani hatumtaki lakini kwa tuhuma zipi? kimyaa!
Inaonekana alikuwa na bunduki kubwa lakini sio SMG, sasa ajabu alikuwa anaipeleka wapi hiyo bunduki????? Hajakanusha kuwa na bunduki ila amekanusha sio SMG
alikuwa anajifunza kuiba! Vp kuhusu smg naona kama maelezo ya kaimu kamanda yananichanganya huko mwisho.